habari zenu wapendwa, nasikia mitaa ya samaki - Dar kuna wazungu huwa wanauza vifaranga vya kuku ila kwa mwanzo wanakuja kuangalia mabanda yako kisha kwa mara ya kwanza wanakupa vifaranga bure na wakikuwa wananunua wenyewe ili mfugo wa pili ukanunue kwao, yaani kama wanafanya "PROMOTION FULANI" plz kwa yeyote anayejua kwa hili plz atujulishe.
Hawa mimi sijawasikia ila nitaulizia
ninavyofahamu kuna wakenya mradi wao unaitwa RIU search website yao hawa wanatoa vifaranga na matibabu au ushauri kwa kuku chotara/kienyeji wanaanzia kuku 300 kisha wananunua wao ila kwa bei ya 5000 mmoja au unauza na kuwarudishia gharama yao. Pia wanauza vifaranga kwa yeyote bei zao sio tofauti na za kina RETI humu ndani na kisha ukikosa soko wanakutafutia. Hawa wanaingia contract sio tu ya kufuga ila kuchinja, kuhifadhi na kufanya breeding ila tu sikufuatilia kwa sababu hiyo bei ya kuku chotara 5000 niliona ndogo.
Wameanza muda na walizinduliwa na Raisi Kikwete rasmi, walianzia mkoa wa Pwani wilaya zote, Hapa Dar pia wanafanya ofisi zao zipo Mikocheni jirani na Feza schools kuna barabara inaenda kulia ukitokea Kawe wapo jirani na ofisi za Save children (spelling) nadhani.
Ila mie nikiangalia mfumo wao ni kiasi cha mtu kukomaa tu ufikie walipo, vifaranga wa RETI niliochukua kwa pilot ni wakubwa sasa hivi na bei imecheza 12000 -15000 bado sikukuu haijaja. Sasa issue ni kuangalia soko wakiwa wengi na pia tufikirie zaidi ya kuuza kuku mzima na kuanza kufanya packaging na processing
1. mayai kuwa mayonnaise, hata kupikia keki etc
2. kuku kutengeneza sausages, minced meat, kupack parts, half, kupika etc