TETESI: Wema A Sepetu amtosa Diamond

TETESI: Wema A Sepetu amtosa Diamond

Mkasika

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2010
Posts
391
Reaction score
155
miss-wema-abraham-sepetu.gif


Ni habari ambazo zimezagaa hapa mjini kuwa ma-super stars hawa wametosana!
Wenye taharifa kamili tunaomba data.
 
Ni habari ambazo zimezagaa hapa mjini kuwa ma-super stars hawa wametosana!
Wenye taharifa kamili tunaomba data.
Siku nyingine ukitaka UDAKU nenda Globo, utashiba. Hizi habari zimeshapitwa na wakati!


Na Musa Mateja
2.jpg
Mastaa wa Kibongo waliowahi kuwa wapenzi na baadaye kutemana, Miss Tanzania 2006/07 anayefanya vyema kwenye tasnia ya filamu, Wema Abraham Sepetu na Charles Gabriel Mbwana ‘Chalz Baba’, wamerejesha rasmi mapenzi yao upya, Risasi Jumamosi linakuwa la kwanza kuibumburua.

TETESI ZAENEA, RISASI JUMAMOSI LAINGIA MZIGONI

Mei 7, mwaka huu, rafiki wa karibu wa Chalz Baba aliling’ata sikio gazeti hili kuwa, kuna kitu kinaendelea kati ya wawili hao.
wemanachalzbaba.jpgChanzo hicho kilidai kuwa, Chalz Baba amekuwa akipokea meseji kwenye simu yake kutoka kwa Wema akiomba warudiane.

“Ukiachilia mbali meseji, kuna siku Wema alimpigia simu Chalz Baba nikapokea, akadhani anaongea na jamaa, akaanza kumuomba warudiane,” kilimalizia chanzo hicho na kukabidhi majukumu kwa Risasi Jumamosi.

Gazeti hili lilizama mzigoni ambapo Mei 11, mwaka huu saa 9:00 usiku, Chalz Baba alinaswa akiwa na mrembo huyo nje ya nyumba ya akina Wema maeneo ya Sinza-Mori, Dar es Salaam.
Bila kuwashtua ‘shushushu’ wetu aliwafuatilia hatua kwa hatua ambapo walionekana wakiwa wameweka mapozi mazito ya kimahaba huku wakijadili jambo fulani na kulumbana kiaina.

WEMA AMPA CHALZ BABA WARAKA WA MAPENZI
Katika harakati za kuachana kwa lengo la kwenda ‘kumbonji’, Wema alimuita Chalz Baba na kumtaka amgeukie.

Jamaa alipotii alichoombwa, Wema alionekana akimkabidhi zawadi ya kitambaa kilichopambwa na waraka wa maandishi ya kimapenzi ambayo Chalz Baba alisika akiyasoma kwa sauti na kuyafurahia kabla ya kukumbatiana na ‘kudendeka kishkaji’.
Risasi Jumamosi lilimtafuta Chalz Baba ili kuthibitisha kama kweli amerudiana na Wema ambapo bila hiyana, alifunguka:

“Siwezi kusema tumerudiana lakini ni kweli tumekuwa na mawasiliano ya karibu sana kwenye simu na kukutana naye mitaani kama marafiki wa kawaida.
“Unajua huwezi kuachana na mwanamke halafu mkashindwa hata kuwasiliana.”
Paparazi wetu ‘alipomtaiti’ juu ya kuwepo kwa ushahidi wa mawasiliano yao ya kimapenzi, Chalz Baba alitambaa na mistari:

“Ni kweli katika siku za hivi karibuni Wema amekuwa akiniomba sana tuonane kwa ajili ya mazungumzo.

“Siku hiyo baada ya kutoa burudani pale Billz (Bilicanas) nilimfuata Wema nyumbani kwao (Sinza-Mori) kwa kuwa aliniomba sana na sikuwa na ugomvi naye.

“Tulizungumza ‘fresh’ na baadaye kila mtu akaenda kulala kivyake.

“Siwezi kukutamkia kwamba sisi ni wapenzi ‘coz’ hatukukubaliana chochote kilichohusu uhusiano wetu wa kimapenzi.

Juhudi za kumpata Wema ziligonga mwamba lakini zinaendelea, akipatikana atafunguka ‘laivu’ juu ya ishu hiyo na tutawaletea ripoti kamili.
 
Binafsi huyu demu namuona kama hana akili nzuri! Iweje ashindwe kuvumilia hata mwezi baada ya kupigana chini na mwanaume, yaani ina maana hawezi kuvumilia kabisa. Nilisoma dazeti moja la kidaku juu ya habari ya Wema kupigana chini na Diamond kisha wakaweka picha hii hapa chini.View attachment 30157
 
Wema kakanusha tena kwa Kiswanglish cha ukweli. Ni raha tupu kumsikiliza demu akiongea. Damn! She sounds really sophisticated and soo self-confident!

ZAMARADI
 
Wema kakanusha tena kwa Kiswanglish cha ukweli. Ni raha tupu kumsikiliza demu akiongea. Damn! She sounds really sophisticated and soo self-confident!

ZAMARADI
Ukiokiondoa udhaifu wake mwingine ktk kitu nampa big up wema ni njinsi anavyojua kuongea na media,anajipanga,hakurupuki,halopoki,anajua aongee nn na wapi na nani.maoni yangu diamond hafit kwenye viatu vya wema,he is not her type
 
du kimsingi demu amejichokea na maisha ameaamua kubadili vijana kama nguo
 
Back
Top Bottom