Teuzi na Tenguzi za Viongozi Mabalimbali Zilizofanywa na Rais Wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (2005-2015)

Kikwete amteua Zitto kwenye kamati ya mikataba ya madini

*Itaongozwa na Jaji Mark Bomani,

* Pia wamo Cheyo, Mwakyembe
* Yapewa miezi mitatu kumaliza kazi
* Zitto asema atafanya kazi kwa maslahi nchi
Na Tausi Mbowe

RAIS Jakaya Kikwete amemteua Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe kuwa miongoni mwa wajumbe wa Kamati ya uangaliaji upya mikataba ya uchimbaji wa madini nchini.
Kamati hiyo yenye jumla ya wajumbe kumi na mmoja itakuwa chini ya uenyekiti wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mstaafu, Jaji Mark Bomani.

Wengine katika Kamati hiyo ni Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), John Cheyo, Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishina wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe.

Wajumbe wengine ni Mbunge wa Msalala (CCM),Ezekiel Maige, Peter Machunde kutoka Soko la Hisa, Dar es Salaam (DSE), Mkaguzi wa Mahesabu kutoka Kampuni ya Kimataifa ya Ukaguzi wa Mahesabu, PriceWater Coopers, David Tarimo ambaye ni mtaalam wa masuala ya kodi na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa, Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo.

Taarifa ya Ikulu iliyosainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo ilisema kuwa pamoja na mambo mengine, kamati hiyo pia itakuwa na kazi ya kuchambua mfumo wa kodi unaotumika katika sekta ya madini na kupitia mfumo wa usimamizi wa shughuli za uchimbaji mkubwa unaofanywa na serikali. Kamati hiyo iliyopewa kipindi cha miezi mitatu kukamilisha kazi yake pia inajukumu la kukutana na taasisi zinazosimamia madini na wadau wengine na kutakiwa kutoa taarifa yenye mapendekezo.

Pia Kamati hiyo itakuwa na jukumu la kupitia mikataba ya madini na nyaraka nyingine zitakazohusu migodi ya mikubwa nchini. Kuundwa kwa Kamati hiyo kunafuatia hoja binafsi ya Zitto Kabwe aliyoitoa bungeni kutaka kuundwa kwa Kamati Teule yakuchunguza mazingira ya kusainiwa kwa mkataba wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi huko Uingereza na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi Februari mwaka huu. Baada ya kuwasilisha hoja hiyo, Kabwe alifungiwa kuhudhuria vikao vya Bunge hadi hapo Januari mwakani. Hatua hiyo ya Bunge iliibua mjadala mkubwa miongoni mwa makundi mbalimbali wakihoji sababu za kumfungia mbunge huyo kijana.

Hivi karibuni wakati Rais Kikwete akihutubia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi katika Ukumbi wa Kizota , mjini Dodoma aliahidi kuunda kamati hiyo itakayojumuisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kuangalia mikataba mipya ya madini. Akizungumza na Mwananchi kuhusiana na uteuzi huo, Zitto Kabwe alisema kwamba amepokea uteuzi huo wa Rais Kikwete na atafanya kazi kwa maslahi ya Watanzania.

"Nimepokea kwa mikono miwili uteuzi, naahidi kufanya kwa umakini wa hali ya juu," alisema alisema Zitto na kuongeza kwamba uamuzi wa Rais unaonyesha jinsi alivyokomaa kidemokrasia tofauti na wabunge 274 wa Chama cha painduzi (CCM )walioko bungeni.
 
hapa ndio itabidi Zitto awe makini kabla ya kukubali huu uteuzi na ajue kabisa powerz zote za hii kamati na kile ambacho itafanya kabla ya kuingia mkenge
 
Tofauti ni kwamba pesa ya walipa kodi inaendelea kuteketea na wao safari ndio kwanza imeanza.

Mkuu Dua,

Mazingaombwe mengine hata watoto wanaona na kugundua.
Mwaka huu mengi yataonekana Tanzania.
 
kauli ya zito kuwatusi wabunge inaweza kumfanya achukuliwe hatua zaidi..'RAIS KIKWETE AMEONESHA KUKOMAA KIDEMOKRASIA ZAIDI YA WABUNGE WA CCM 274` ..kwa mujibu wa vifungu vya bunge,Mbunge anakatazwa kusema maneno ya uzushi,au yanayoweza kushusha heshima ya mbunge mwingine ktk jamii..
 
"Nimepokea kwa mikono miwili uteuzi, naahidi kufanya kwa umakini wa hali ya juu," alisema alisema Zitto na kuongeza kwamba uamuzi wa Rais unaonyesha jinsi alivyokomaa kidemokrasia tofauti na wabunge 274 wa Chama cha painduzi (CCM )walioko bungeni.

Zito bwana anajibu mapigo hapo kwa papo. Mimi sina wasi wasi na Zito kwa sababu, amekwisha onyesha umakini wake hadi hapa alipofika, huzuni yangu ni pesa ya walipa kodi jinsi inavyochezewa kama vile haina mwenyewe........Wenyewe wapo wabongo na hawa viongozi wamesinzia usingizi wa pono wanawakumbatia mafisadi katika kuimaliza.
 
Sio tusi, kwani alichofanya Rais ndicho kilichomfanya Zito aitwe muongo na wabunge hao hao 274, kama unabisha kuwa hawa jamaa hawajakomaa soma tena bajeti ya serikali ya mwaka 2007/2008, halafu ujiulize ni nani aliipitisha!
 
Mwakyembe ni lazima ajitoe mojawapo ya hizo Kamati ili ziwe huru! Tunataka tuone kama Kamati mbili huru na zisizoingiliana zinapoangalia ushahidi ule ule zitaweza kufikia suluhisho moja?
 
The more akifungiwa, the more anapata umaarufu. sidhani kama wanaweza kumfungia tena. they've got a lesson
 

Mkuu Dua.

Kikwete anatapatapa right now. Aliwekwa ikulu na wezi na mafisadi. Mtoto wake anafanya kazi kampuni ya IMMA inayotetea na kulipwa pesa za mafisadi every other day! Kina Karamagi bado wanapeta tu wizarani, na leo anaunda kamati ya kina cheyo, bomani na mwakyembe?

Tanzania kweli ina pesa zaidi za kuharibu na Kikwete is the right guy kwa kufuja pesa za wabongo.
 
napendekeza mheshimiwa ZITTO ajitoe kwenye hiyo kamati ilikulinda heshima yake na upinzani kwa ujumla.kwenye hiyo kamati hakuna jipya zaindi ya kummaliza zitto na upinzani kwa ujumla.
 
i) Mpaka kieleweka et al.: Si kweli kwamba Issa Shivji na Tundu Lissu ndio watu pekee wanaoijua mikataba ya madini au wenye uchungu na Tanzania. Kwa hiyo mimi kutukuwepo hawa katika kamati sioni tatizo kabisa. Tuache kasumba ya kufikiri kwamba ni watu fulani katika jamii yetu wenye uwezo wa kufanya mambo, huo na ni utegemezi! Ile nchi ina watu mil 36 wenye vipaji mbalimbali. Watu wakipewa kazi, tuwasukumu na kuwatia moyo kuhakikisha wanafanya kazi ya vizuri.
ii) Ndio nasema kila siku kuwa nchi yetu ina uhaba wa mafanikio kiasi kwamba hata likitokea jambo dogo inabidi tushangilie kama mazuzu. Ndiyo tuliweza kubagawa hata Rashid kushinda mashindano ya BBA. Sasa na hili nalo sishangai. Lakini binaafsi, at the risk of being seen cynical, sioni cha kushangilia. Yaani mafanikio hapa ni nini hasa hadi tumsifu JK? Huyu mtu kuna siku tutamsifia hata atakapoamka mapema. Kosa la mikataba mibovu walifanya wao, sasa wanapochukua hatua za kurekebisha tena kwa shinikizo, sisi tunachosifia hapa ni kitu gani hasa? Tunamsifia baba kununua nepi za mwanae? Ndio kusema siku JK atakapoamua kuwatoa akina Karamagi itabidi tufanye maandamana ya kumpongeza, tuna wazimu au nini?
 
napendekeza mheshimiwa ZITTO ajitoe kwenye hiyo kamati ilikulinda heshima yake na upinzani kwa ujumla.kwenye hiyo kamati hakuna jipya zaindi ya kummaliza zitto na upinzani kwa ujumla.

Sidhani kama hii ni busara.Litakuwa jambo la kitoto na kishule zaidi kuliko utu uzima. ALichofanya JK ni kuunda kamati yenye sura ya multipartisan ili kuhakikisha talent mbalimbali anazitumia ndani na nje ya CCM. This is good na inaonyesha kukomaa na kukubali kwamba kuna watu wenye akili hata nje ya CCM. Actually, ningemshangaa na kumzomea sana Zitto kama angekata uteuzi, it would have been counterproductive and self-defeating. Anachotakiwa kufanya Zitto ni kuhakikisha kwamba yale mapendekezo yake aliyokuwa nayo yanaingia kwenye kamati. Pale ambapo hatakubaliana na baadhi ya vipengele na ikitokea kwamba wenzake wote wameng'ang'ania hivyo, basi anapaswa kuweka dissening opinion. Baadhi ya kamati kumaliza kazi yake, ahakikishe yale waliyokubaliana yanakuwa wazi. Wasikubali utamaduni wa kijinga kwamba tumeshawasilisha mapendekezo yetu kwa Rais halafu ni yeye pekee atakayoyatoa kwa wakati anaotaka.
 

Weka newz zaidi mkombozi kama unazo!
 

Kitila,

Heshima mkuu. Ni kweli kuwa Zitto inabidi aingie katika kamati hii na kuhakikisha kuwa mawazo yake hayabafungwi na spin master Mwakyembe!

Hata hivyo swali bado linabaki hapa! Wanaccm wengi hapa akiwemo mkuu FMES wameshasema kuwa mikataba iliyokwishasainiwa haiwezi kuvunjwa unless tunataka kuleta mambo ya IPTL!

Hii kamati utofauti wake ni nini na ile ilokuwa inapitia mikataba wakati Karamagi na Lowasa wakisaini mkataba wa Buzwagi!
 
heeh, hongera JK, hongera Zitto !

nasikia harufu ya kitu kimoja kufikia EXTINCTION !!
 

yeye ni kama nani ajibu hayo maswali ? hakunegotiate chochote, yeye kazi yake ni kudeal na before na aftermath ya matukio na hakuwemo katika hilo sakata !

mtafute karamagi muulize, mpigie simu uongee nae !
 

Well, mimi nafikiri kazi kubwa ya hii kamati ni kutafuta ukweli juu ya mikataba yetu ya madini. Je, ni kweli kwamba mikataba ndiyo tatizo au tatizo ni usimamizi wa mapato yanayotokana na madini yetu? Kama mikataba ndiyo,tatizo basi kamati inabidi itoe mapendekezo ya radical changes. Utekelezaji wake ni wa hao tuliowakabidhi nyenzo za kufanya maamuzi.

Angalizo ambalo akina Zitto lazima waliangalie ni ukweli kwamba wale wazungu wenye makampuni ya madini watawafuata sana kuhakikisha kwamba hawapendekezi radical changes. Sasa akina Zitto wana options mbili: kuamua kuibuka matajiri for once and all kutokana na mapesa watakayopewa na hawa wazungu ili kuhalalisha yasiyohalalishika yaliyopo kwenye mikataba, au kufanya kazi ya maana kwa utaifa ili kuibua ukweli wa mambo na kupendekeza radical changes zitakazotufanya nasi tufaidi kasehemu kadogo kaliko baki kwenye yale mashimo-na kwa kufanya hivyo waibuke mashujaa wa taifa in the rest of their life. Mimi siwajui sana wengine, lakini nina imani ya kutosha na Zitto. Lakini hatuwezi kufumbia macho ukweli kwamba hawa wote walioteuliwa ni wanasiasa, sasa don't forget the three enemies of a politician: money, sex and an insatiable thirsty for power!
 
Zitto kajinyamazisha mwenyewe! J.K tactics will work if you consider practical guidelines of forming a committee for instance....
the government has affirm its confidence in the integrity of members who are appointed to serve on this committee:- By appointing a bipartisan committee. To say the committee has a vacuum of akilimali is to say You have no confidence in the Presidents decision ! Yet an affirmation of the integrity of these mambers....
Conflict of Interest
Because of the nature of the work of such committee, those who serve on them must be especially sensitive to conflict of interest situations and the appearance of impropriety.

A conflict of interest occurs when an individual's personal or private interests may lead an independent observer reasonably to question whether the individual's professional actions or decisions are influenced by considerations of significant personal or political party interest, financial or otherwise. And to say it was bipartisan! I think there is a need to think wiser.
Confidentiality
There is also the issue of confidentiality you know a good committee member need to maintain a high degree of confidentiality regarding the committee’s discussions, both oral and written.
Mind you committee members need to feel free to speak frankly in a closed session, knowing that their comments will not be repeated outside that room, and that they preserve the right to speak for themselves outside of that closed session.
Here ziito will find himself in a dillema...with his glamourized tactics and also mamber of such commitee he might be bound with both hands and feet!
When it comes to KUPIGAMAKELELE there are Guidelines on publicity which members might not reveal or publicize any confidential information learned through service on the committee; nor should they make such confidential information available to non-committee-members(kama vile mwanakijiji)LOL.

Members of the committee who run or participate in social networking web sites(we see Zitto here sometimes) or software, including blogs, wikis, electronic discussion lists, and the like, should not engage in any discussions about their committee work, or about the status of commitees work during their term of committee service. Will Zitto adhere to such?
Once they sign of such a guideline their work is only known to His Excellency J.K And in such it is likely Zitto might go green!
source:Google/Wikipedia/
 
Watanzania ni rahisi sana kudanganywa kama watoto kwa peremende,eti kamati ya kuangalia upya mikataba ya madini? na kwa akili zenu mnaamini kabisa hapo kuna mikataba itabadilishwa kutokana na mapendekezo ya hii kamati,yaani ni kichekesho kweli kweli mpaka inatia huruma
 


Umeeleza vyema Atanaye,
Hata hivo ushauri wa bure kwa Zitto ni kwamba hapa kapewa turufu ya hatma yake ya baadae kisiasa sasa ni ama:

Ajimalize mwenyewe kwa kukubali kunyamazishwa na 'kuturn green' kama ulivo sema,

Ama asimamie upande wa haki ili kungalisha turufu yake kama ilivo anza kuchanua.

Ukweli ni kwamba kila mtu atafatilia sana kamati hii hasa kwa mategemeo makubwa kwamba Zitto sasa ata tumia nafasi hii kuweka wazi na kuanzisha kile ambacho kimewavuta watanzania wengi juu yake! Natumaini he will not go that much cheap kwa ajili ya mafanikio yake ya mbele na mapenzi ya taifa letu kwa ujumla.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…