TFF chagueni wachezaji mwenye miili mikubwa

TFF chagueni wachezaji mwenye miili mikubwa

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Miili mikubwa ni kigezo muhimu Kwa mchezaji wa mpira. Hata mawakala wanatafuta wachezaji wenye vipaji, akili na miili mikubwa.

Mchezaji mwenye mwili mdogo ni rahisi Sana kukabwa, kuumizwa na kufanyiwa faulu nyingi.

Golikipa mwenye mwili mdogo anawatia hamu mafowadi kumshambulia hata Kwa mbali.

Wachezaji wenye miili midogo hawauziki sokoni
 
Mwili hauchezi mpira mkuu km kipaji hakuna, mwili unajengwa tu.

Ama unazungumzia kimo kama kimo si tatizo, xavi,zola,kante,, casillas, Pickford n.k n.k.
 
Vimo vikubwa vina nafasi yake kwenye soka, na wachezaji wenye miili midogo ukiona anauzwa ujue basi huyo ana kipaji cha ajabu sana (Kama Messi) ila mchezaji kama Ramadhan Singano hata ukipeleka sokoni kumuuza lazima utapata taabu.

Mpira ni fitness na watu huangalia na uwezo wa mwili kukabili mikimiki. Ramadhan Singano anakuwa beki 2 na unampa kazi ya kumzia mchezaji haina ya Lukaku.!!!!!!
 
Miili mikubwa ni kigezo muhimu Kwa mchezaji wa mpira. Hata mawakala wanatafuta wachezaji wenye vipaji, akili na miili mikubwa.

Mchezaji mwenye mwili mdogo ni rahisi Sana kukabwa, kuumizwa na kufanyiwa faulu nyingi.

Golikipa mwenye mwili mdogo anawatia hamu mafowadi kumshambulia hata Kwa mbali.

Wachezaji wenye miili midogo hawauziki sokoni
Mikubwa kama ya MESI, Tff wameuchukua ushauri wako...
 
Fact afcon tukiwapata john bocco watatu pale mbele lazima tuende robo fainali
 
Miili mikubwa ni kigezo muhimu Kwa mchezaji wa mpira. Hata mawakala wanatafuta wachezaji wenye vipaji, akili na miili mikubwa.

Mchezaji mwenye mwili mdogo ni rahisi Sana kukabwa, kuumizwa na kufanyiwa faulu nyingi.

Golikipa mwenye mwili mdogo anawatia hamu mafowadi kumshambulia hata Kwa mbali.

Wachezaji wenye miili midogo hawauziki sokoni
Mkuuu uko sahihi kwa asilimia 100, wanaobisha acha waendelee kutoka povu. Hivyo ndivyo vigezo vya soka la Ushindani hutaki utaendelea kucheza chandimu tuuu.
 
Ni Kweli
Kama wachezaji wawili wako sawa katika kipaji cha kucheza mpira,
Mwenye umbo kubwa atauzika mapema kuliko mwenye umbo dogo.
Mchezahi kama Ramadhani Kessi hawezi kucheza nafasi ya beki ktk timu zenye ushindani kama timu za Ulaya na America kwa sababu ya kimo chake tu
 
Mwili hauchezi mpira mkuu km kipaji hakuna, mwili unajengwa tu.

Ama unazungumzia kimo kama kimo si tatizo, xavi,zola,kante,, casillas, Pickford n.k n.k.
Kaka ukiwa na vimo kama vya hawa unaowasema lazima uwe na vitu vya ziada sana vya kuzaliwa navyo sio vya kufundishwa na mtu ili ufanye vizuri kwenye soko la mpira wa miguu. Watu kama hao sio wengi duniani
 
1. Lionel Messi
2. Juan Mata
3. Alex Sanchez
4. Ngolo kante
5. Robert Firmino
6. Felipe Anderson
7. Benard Silva
8. Luca Modric
9. Paul Dybala


Wote hawa ni wachezaji wenye maumbo madogo ila shughuli yao unaijua
 
Kaka ukiwa na vimo kama vya hawa unaowasema lazima uwe na vitu vya ziada sana vya kuzaliwa navyo sio vya kufundishwa na mtu ili ufanye vizuri kwenye soko la mpira wa miguu. Watu kama hao sio wengi duniani
Kwani Peter Crouch (Super Tall ) ana kipi cha kumshinda mchezaji mfupi Mbwana Samata ??



Mpaka hapo usipoamini kuwa maumbo hayana lolote kwenye mpira Basi wewe nimekushindwa
 
1. Lionel Messi
2. Juan Mata
3. Alex Sanchez
4. Ngolo kante
5. Robert Firmino
6. Felipe Anderson
7. Benard Silva
8. Luca Modric
9. Paul Dybala


Wote hawa ni wachezaji wenye maumbo madogo ila shughuli yao unaijua
Vivyo ni vipaji maalum ambavyo ni zaidi ya academy. Mimi naongea watu wanaofaa kuchuguliwa kufunzwa mpira. Unapomtaja Mess kwenye hili ni Sawa na kumfananisha Michael Jackson na Peter Msechu, au Bob Marley na Nganyagwa
 
Vivyo ni vipaji maalum ambavyo ni zaidi ya academy. Mimi naongea watu wanaofaa kuchuguliwa kufunzwa mpira. Unapomtaja Mess kwenye hili ni Sawa na kumfananisha Michael Jackson na Peter Msechu, au Bob Marley na Nganyagwa
Hueleweki unataka nini ,
 
Tatizo vijana wa Tanzania lishe duni , kwenye mpira umbo alina nafas sana, messi, aguero wafupi lakin wana msuli , stamina speed na akili ya mpira
 
Bernado Silva
Raheem Starling
Sergio Aguero
David Silva
Gabriel Jesus

Ndio wanaoongoza mashambulizi Man City.

Hebu tuone hawa
Messi
Mo Salah
Xavi
Iniesta
Andy Robertson
Luca Modric

Mwili kwa walinzi na mabeki tu. Kwingine hauhitajiki. Inahitajika kasi, akili na kipaji.
 
Kikubwa ni uwezo mbona messi ana mwili wa kawaida lakini anatandaza kandanda safi hadi kila mtu ansema ewaaaa!
 
Hueleweki unataka nini ,
Wewe ndo huelewi, ni kazi ndogo Tu tff waulizeni mawakala wa wachezaji kuwa ni aina gani ya wachezaji wenye sifa zipi wanahitajika kwenye soko la ulaya, watakuambieni. Ndiyo maana Maximo alimkataa Kaseja akamkumbatia Ivo Mapunda ingawa Sisi tulikuwa tunamuona anaweza sana. Wachezaji wetu wenye maumbo madogo ni hodari wa kukaba Kwa kusababisha faulu za kila mara
 
Back
Top Bottom