TFF imekuwa kama Serikali ya Kagame vile, ukileta ujuaji unakwenda na maji

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
390
Reaction score
1,425
Mimi nilikuwa namshabikia sana Karia, niliona ana mwelekeo mzuri sana wa kusaidia kuinua soka letu mbele, lakini baada ya kufanya tathmini kwa kuangalia demokrasia naona Karia anajenga chuki miongoni mwa wapenda soka wetu.

Karia kwa haya anayofanya kupitia kamati zake ambazo naamini anazipa maelekezo nn cha kufanya zinamuondolea heshima.

Kila siku kufungia wachezaji, viongozi, makocha sio dawa wala haisaidii, hebu jiulize tangu ulipoanza kutoa adhabu kali umepata mafanikio gani zaidi ya kujenga chuki.

Umemfungia Shaffih Dauda, umemfungia maisha Wambura, unataka kumnyima leseni Jemedari Saidi, umeagiza atenguliwe, umempiga miaka mitano Mbwana Makata, umefungia maisha baadhi ya viongozi wa soka wa mikoa, hii inanipa wasiwasi kuwa hiv anayetoa adhabu za namna hii ni mtanzania kweli, mbona ana roho za kitutsi namna hii.

Marehemu Ndolanga aliwachosha watu kwa namna hii hadi akaondoka kwa aibu kwenye uchaguzi.This time, watu watakuwekea mikakati Karia utaondoka hapo TFF, unaua maoni ya watu kupitia adhabu.

Maoni ya wadau wa soka yaheshimiwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…