Tff mpeni timu ya taifa stars Kocha Nabi

craq

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2017
Posts
859
Reaction score
1,866
Kwanza anawajua wachezaji wa kiAfrica na anafahamu kuwaongoza.

Pili ni kocha na mwalimu wa Mpira ni genius kwenye mifumo na mbinu


Tff kazi kwenu

 
Nikiwa shabiki kindakindaki wa Simba nakubaliana na wazo lako mwana utopolo kuwa huyu profesa Nabi akabidhiwe timu yetu ya taifa ili izo pasi 978 walizopigiwa dodoma jiji zihamie kwenye timu yetu pendwa ya taifa
 
Acheni uchawi wenu. Mmeona Yanga inainuka sasa mnataka muiangushe kwa kumuiba kocha. Hamtakagi kabisa wana jangwani kua na furaha. Mpeni pablo hiyo timu yenu ya taifa.
 
Why we think of everything by results?

Ukiulizwa useme kwanini apewe Timu ya Taifa, utajibu kwa sababu Yanga inafanya vizuri, utadhani ni guarantee kwamba na Taifa stars itafanya vizuri!

Very quick to conclude.
 
Kipofu kaona mwezi,Dah,,mashabiki wa Uto wanatuaibisha kwakweli.
Kumfunga mgogo ndo mshamuona kocha wenu Zagallo?
Hivi angefungwa Al Ahly au Zamaleck tungekunywa maji ndugu zangu?

Kabla ya kumpa timu ya taifa Nabi kumbuka timu aliyotoka ni Al marrikh ya Sudan alifukuzwa kazi kwa kutoa draw na Simba CAFCL group stage.
 
Sisi kama wana yanga ni kiri tu kuwa tumefikia hatua mbaya sana kwa mawazo haya

Chenga mbili tu tayari tushaanza kumuona kama neymar?
Kolo ww.. Ngoja Leo uzamishwe nyama na Azam
 
Kipofu kauona mwezi. Hizi goli 4 mbona jambo la kawaida Sana kwenye mpira? Utopolo mwenyewe alishawahi kula kichapo cha 4 kutoka kwa mnyama. Hili ndilo tatizo la kuzoea kagoli 1
 
Ilikuwa lazima afukuzwe. Anawezaje kutoshinda kwa Simba
 
Nikiwa shabiki kindakindaki wa Simba nakubaliana na wazo lako mwana utopolo kuwa huyu profesa Nabi akabidhiwe timu yetu ya taifa ili izo pasi 978 walizopigiwa dodoma jiji zihamie kwenye timu yetu pendwa ya taifa
Wachezaji wangapi wa Yanga wanaweza cheza timu ya taifa/Taifa Stars
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…