TFF na Azam FA

HIMARS

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2012
Posts
70,791
Reaction score
98,334
Haya mashindano mnayaharibu kwa kupanga timu za daraja lisilojulikana na timu za ligi kuu.

Ingependeza kuwepo kwa mchujo kabla ya kukutanisha hizi timu.

Yanga
Azam
Simba

Watafunga hata goli 30 kila timu
 
Huu mfumo ni mzuri. Maana hizo timu za madaraja ya chini, kuna kitu zinajifunza kwa kucheza na timu kubwa. Na hii ndiyo maana halisi ya FA Cup.

NB: Usisahau huu mfumo tumeiga kwa wenye mpira wao.
 
Hata uingereza upo hivi hivi na timu kubwa sometimes zinapokea kichapo. Tujikumbushe kuwa Simba alishawahi fungwa na Green woriorrs na Mashujaa fc katika michuano hii
 
kwa uk timu ndogo zinaanza hatua za mwanzo za fa cup, baadae kwenye 3rd na 4th round ndio utaziona za premier...
 
Hat-trick 6 ndani ya wiki moja. Kumbe makadirio ya Waziri kwenda WC 2030 ni mbali Sana.
 
Huu mfumo ni mzuri. Maana hizo timu za madaraja ya chini, kuna kitu zinajifunza kwa kucheza na timu kubwa. Na hii ndiyo maana halisi ya FA Cup.

NB: Usisahau huu mfumo tumeiga kwa wenye mpira wao.
Hii ni round ya ngapi?

Navyojua, utanisahihisha kama nimekosea, huko England, round za mwanzo timu ndogo zinaanza kuchujana wao kwa wao, halafu round za baadae kabisa ndo timu ndogo zinaanza kukutana na timu kubwa kubwa. Wanaenda hatua kwa hatua!




Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Hata huku nako ni hivyo hivyo. Hizo timu ndogo huwa zinakutana na timu za Ligi kuu katika hatua ya 32 bora, baada ya zenyewe kwa zenyewe kuchuana katika ngazi za chini. Baada ya mechi za juzi, zimebakia timu 16!
 
Hata huku nako ni hivyo hivyo. Hizo timu ndogo huwa zinakutana na timu za Ligi kuu katika hatua ya 32 bora, baada ya zenyewe kwa zenyewe kuchuana katika ngazi za chini. Baada ya mechi za juzi, zimebakia timu 16!
Majibu mazuri mkuu, hili limekwisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…