Mi nimeamua kuanzia Leo siangalii Tena mechi za Simba kubebwa kumezidi hadi inatia kichefuchefu Singida BS wameonewa Sana Leo, walistahili ushindi , kila faulo inaenda kwao, goli lao la wazi wamenyimwa Ili kuipa Simba nafasi ya kufunga na kuongoza ligi. Mchezaji wa Big Stars hakuwa offside maana alisharudi ndani na nyuma yake walikuwa mabeki wa Simba na mpira ulishachezeka iweje awe offside , Sheria namba ngapi ilitumika? Othman Kazi hebu njoo uchambue lile goli na lingekubaliwa Simba ingelala leo. Hawa marefa wa msimbazi hawafai, wanashusha ladha ya boli na kuharibu uwekezaji wa Azam kuonesha mechi live Africa nzima , hii ni aibu kwa taifa, yule lines man niliona kama ni Mzee, Hana akili na hafai kuwa kibendera , haya ni madudu ya Mr Karai kung'ang'ania uongozi wa TFF Ili mkakati wake Simba kuchukua ubingwa ufaulu. Na hatoweza kufanikiwa maana Yanga tutamkanda Simba ndani nje na kuchukua points 6 na kazi yote ya kuibeba Simba itaishia hapo!
Kwa mazingira haya timu nyingi zikicheza na Simba hazitoshinda hata wajitoe vipi na inavunja moyo sana mtu unammudu anabebwa hadi inaboa sana!