TFF naomba mkomeshe rushwa kwa waamuzi ili tupate bingwa anaestahili

44mg44

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2019
Posts
2,158
Reaction score
2,186
Naanza kwa kurejea mechi ya Yanga na Azam, hii mechi ilionesha wazi kuwa kuna rushwa kwa waamuzi. Mpira kuna kipind ulitoka nje kabisa halafu mchezaji wa Yanga akakimbilia na kuurejesha uwanjani hatimaye wakafunga goli ambalo si halali yao. Pia Azam walipata penati wakanyimwa, haya yote yanasababisha tunapata bingwa asiyestahili kabisa.

Kama inawezekana TFF iichunguze vizuri hiyo mechi ya Yang na Azam ione makosa hayo ya wazi kisha Yanga wapokonywe point.

Ligi ikiendeshwa vizuri pasipo na upendeleo wowote, pia rushwa ikakomeshwa tutapata bingwa halali na atatuwakilisha vyema kimataifa.

Ni aibu kubwa sana kwa timu ngeni kuja kutufungia nyumbani. Tujirekebishe pia tuamke, wakat ni sasa.
 
2 comments, 4 likes, hivi kwanini ADEN RAGE asijengewe sanamu lake pale JENGO LA MSIMBAZI kwa kazi nzuri sana kuwaita Mashabiki wa MAKOLOKOLO FC "MBUMBUMBU" [emoji848][emoji847]
 
TFF iwafungulie MAKOLOKOLO FC mashtaka na ifungiwe kabisa kucheza michuano yoyote ya ligi hapa TZ, haiwezekani MAKOLO ndiye apokee bahasha nyingi sana za rushwa kuliko timu zingine zote kwa kichapo cha mechi 3 kati ya 5 na mara ya mwisho MAKOLO kumfunga Bingwa YANGA wa NBC PL 2021 - 2022 ni 2019 [emoji23]
 
Mfano halisi wa Kubebwa Kwa Simba na Marefa pale Kibu Denis akiwa katika eneo la hatari langoni kwake alikataa kupigwa kanzu na mchezaji wa Azam aka amua audake mpira Ili asipigwe kanzu na refa alikataa kuwapa Azam pigo la penalty.

Mechi ya Simba na Geita ple Kwa Mkapa Geita walifunga Goli safi la kichwa maamuzi akalikataa Kwa madai Kapombe alisukumwa lakini kwenye marudio ya television hakukuonyesha mgusano.

Mechi ya Simba na prison Mkude Alifunga goli akipokea pasi kutoka Kwa Kibu ambaye alikua nje ya uwanja iki maanisha mpira ulisha toka.
Matukio ni mengi sana ila Kwa Sasa tuishie apo kwako studio.
Tukumbuke msimu uliopita Goli tatu safi za Mayele waamuzi walizikataa bila Sababu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…