TFF rasmi imethibitisha Abdihamid Moallin kuwa kocha msaidizi namba mbili wa Yanga

TFF rasmi imethibitisha Abdihamid Moallin kuwa kocha msaidizi namba mbili wa Yanga

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limethibitisha kuwa klabu ya Yanga imekamilisha taratibu zote za kumtumia Abdihamid Moallin kama kocha msaidizi namba mbili wa kikosi chao ambapo ameanza kutambuliwa kikanuni katika mchezo wa leo Desemba 29 dhidi ya Fountain Gate.

Vilevile Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania imemuonya vikali Moallin kwa kosa la kuketi kwenye benchi la ufundi la klabu hiyo katika michezo mitatu (3) ya Ligi Kuu kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:17 ya Ligi Kuu kuhusu taratibu za Mchezo.

Snapinsta.app_471799952_1140046677740849_4329272320489664286_n_1080.jpg
 
Tff wasisahau Kuna mwaka Makonda akiwa Mkuu wa mkoa yeye na MO walikaa katika bench la Simba.
Nilishangaa Sana lakini kwa wengi ilionekana kitu Cha kawaida.
 
Tff wasisahau Kuna mwaka Makonda akiwa Mkuu wa mkoa yeye na MO walikaa katika bench la Simba.
Nilishangaa Sana lakini kwa wengi ilionekana kitu Cha kawaida.
matajiri hawagonbezwi!
 
Tff wasisahau Kuna mwaka Makonda akiwa Mkuu wa mkoa yeye na MO walikaa katika bench la Simba.
Nilishangaa Sana lakini kwa wengi ilionekana kitu Cha kawaida.
Hii tuikatie rufaa
 
Kwa hiyo alivunja kanuni mara 3 na hawakumchukulia hatua, wanakuja kumpa onyo baada ya kupata taarifa klabu imekamilisha taratibu za kumuwezesha kukaa kwenye benchi. Sasa hilo onyo la kazi gani?

Anyway, huyu anaenda kuchukua nafasi ya Saidi Kichwa mwezi February.
 
Kwa hiyo alivunja kanuni mara 3 na hawakumchukulia hatua, wanakuja kumpa onyo baada ya kupata taarifa klabu imekamilisha taratibu za kumuwezesha kukaa kwenye benchi. Sasa hilo onyo la kazi gani?

Anyway, huyu anaenda kuchukua nafasi ya Saidi Kichwa mwezi February.
Wanajitekenya, hahaha 🤣
 
Kwa hiyo alivunja kanuni mara 3 na hawakumchukulia hatua, wanakuja kumpa onyo baada ya kupata taarifa klabu imekamilisha taratibu za kumuwezesha kukaa kwenye benchi. Sasa hilo onyo la kazi gani?

Anyway, huyu anaenda kuchukua nafasi ya Saidi Kichwa mwezi February.
Boss anaombwa sio kufokewa..
 
Back
Top Bottom