Nimewasili Tanga jioni kwenda kumshuhudia Che Malone ukuta wa Yericko pamoja na fundi wa mpira Fabrice Ngoma kwenye gemu ya ngao ya hisani trh 10 vs Singida, sasa hv niko mkwakwani naangalia mechi ya kirafiki baina ya Coastal Union vs Singida, uwanja ni mzuri sana, nyasi zimekolea ukijani hadi ng'ombe wanazitamani.
Shida nayoiona ni uhafifu wa taa, kucheza wanacheza lakini vivuli vya wachezaji vinaonekana jambo ambalo linaashiria kuwa taa hazina nguvu ya kutosha, TFF rekebisheni hali hii ili wale wenye chuki na nyie wakose la kusema.
Mtakuja kunishukuru