TFF wamtafute shabiki aliyemrushia refa msaidizi chupa ya maji

TFF wamtafute shabiki aliyemrushia refa msaidizi chupa ya maji

GeofK

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2021
Posts
965
Reaction score
1,217
Katika mechi ya jana ya Yanga vs Tabora utd kuna shabiki alimrushia refa msaidizi (kibendera) chupa ya maji na kumfikia mgongoni, hii ilitokea baada ya refa huyo kunyoosha bendera kuashiria kuwa goli la Dube ni offside, na camera zilionyesha wazi ni wapi chupa imetoka hivo wanaweza kuifatilia clip hiyo ili hatua za kisheria zichukuliwe na kuzidi kukuza hadhi ya ligi kuu.
 
Aisee lile lilikuwa ni tukio la kuogofya sana na linapaswa kuchukuliwa seriously mno. Imagine ingekuwa ni chupa ya soda au jiwe ndio limerushwa pale kisha likatua kichwani, je Kuna mtoto yeyote ambaye angetamani kuwa referee???

HAPANA kwakweli nataka nione umakini wa TFF kwenye kuhakikisha usalama wa marefa wetu kupitia hili tukio.
 
Halafu mbaya zaidi sijaiskia hata club ya Yanga ikitoa tamko lolote kukemea tukio hili, wakati juzi tumeona mfano mzuri uko ulaya Real Madrid wakikemea vikali tukio la kibaguzi lililofanywa na shabiki wao kwa Yamal.
 
FB_IMG_17310088003139456.jpg
 
Na kwanini wasimtafute na yule mshabiki waishie kuadhibu club tu?
Timu ndio inalo jukumu la kumtafuta mhusika lkn adhabu ya utovu wa nidhamu kwa mashabiki hubebwa na timu.
 
Timu ndio inalo jukumu la kumtafuta mhusika lkn adhabu ya utovu wa nidhamu kwa mashabiki hubebwa na timu.
Nafikiri timu kushirikiana na mamlaka zinazosimamia masuala ya kinidhamu zinapaswa kushirikiana kuhakikisha kwamba yule muhuni anakamatwa
 
Utajaribu kuunda maneno wee upate japo faraja ila wapiiiii...
Tabora wamewang'ata ng'aaaaaa
Kawaida tu kwenye soka.

Kwani ulifikiri Yanga itashinda kila mechi?

Kuna timu ishawai kushinda mechi zote bila kufungwa kwa miaka yote?
 
Back
Top Bottom