TFF wanaipendelea Simba SC, ukweli huu hapa

Kinumbo

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2019
Posts
3,039
Reaction score
5,560
Kabla ya yote niseme tu mimi binafsi sina ushabiki wa usimba wala uyanga nimeamua kuandika ki michezo tu nikiwa mdau wa mchezo. Kwahiyo mm sio shabiki wa Yanga wala Simba.

Kitendo cha klabu ya Simba kuondoka nchini siku ya Jumatatu Mei 11, 2021 ni dhahiri kuwa hawa jamaa wanabebwa ama kupendelewa sana na TFF.

Klabu ya Simba iliondoka Mei 11, 2021 nchini kuelekea Afrika Kusini kwaajili ya mchezo wa robo fainali ya michuano ya klabu bingwa Afrika. Siku hiyo hiyo ilikuwa icheze mchezo wa ligi kuu Tanzania dhidi ya Coastal Union ya Tanga. Swali linakuja kwann Simba ilishindwa kucheza na Coastal Union kisha ndio ikaelekea Afrika Kusini?

Ikumbukwe kuwa Mchezo kati ya Kaizer Chiefs dhidi ya Simba SC utachezwa Mei 15, 2021. Kutoka Mei 11 mpka Mei 15 kuna siku 5 hapo, Simba ilishindwa nn kucheza mchezo na Coastal Union?

TFF wanaipendelea sana simba maana wao ndio waliruhusu huu mchezo wa ligi kuu Tanzania bara usichezwe kwa kisingizio kuwa simba inaifuata Kaizer Chiefs kwenye hatua ya robo fainali. Hiyo ni hoja ya kipumbavu sana na isiyo na mashiko kabisa. Why Kaizer Chiefs Mei 12 alicheza mchezo wa ligi kuu Afrika Kusini, Simba alishindwa nn?

Simba alishindwa nn kucheza hiyo Mei 11 kisha Mei 12 akaelekea Afrika Kusini?

TFF mnatukosea sana sisi wadau wa michezo.
 
Acheni upumbavu wa akili nyie utopolo tengenezeni timu lenu bovu shindeni mechi zenu,,..
Mlivyokua kileleni mlikua kimya sasaivi kila siku mnakuja na mpya.

Nikuambie tu hiki kilichofanyika ni mipango mikubwa ya kinchi kuhakikisha Simba anatinga nusu hata fainali..
Kaizer chief toka Juma lilopita wapo hapa nchi kutaka kuangalia hizi mechi mbili za mwisho za Simba wajue current form,streghth na weekness za Simba,nikueleze t haya yalofanyika wamepigiwa chenga ya mwili na yamewachanganya vibaya hawajui hata wataingia na plan gani zidi ya Simba..
Simba ikifanikiwa kufika nusu ni faida kwa mpira mzima wa nchi alaf we unataka tucheze na coast.
 
Mkuu Kama Nakuelewa Hivii
 
Lakini kumbuka pia kuna vipimo vya korona na mchezaji akikutwa anatkiwa kukaa karantini kwa siku tatu then apimwe upya Sasa hebu fikiria Simba akiondoka tarehe 12 then akutwe na tatizo atfanyaje na siku tatu zinakuwa zishafika. Unapotoa hoja jitahidi kuelezea kwa mapana mkuu siyo kuwaza ndani ya box fikiria hata nje ya box
 
Pamoja na malalamiko yako yasiyo na tija lakini ujue kuwa TFF wanaisaidia Simba pia kuboresha brand ya soka la Tanzania. Huo ndio ukweli.

Ligi yetu ya Tanzania inapanda viwango kwasababu ya Simba kufanya vizuri Africa sasa kwanini TFF isifanye kila liwezekanalo kuisaidia Simba kuendelea kufanya vizuri as long as hakuna sheria zinazovunjwa na wala hakuna upangaji matokeo?

Utopolo acheni majungu matokeo mazuri ya Simba ndio yanawabeba na nyie mshiriki kwa mgongo wao huko CAFCL.
 
Nikadhani Simba wamepewa point tatu bila kucheza,

Kama mchezo umesogezwa mbele anayeumia zaidi ni huyo Simba kwa kuwa na mavipolo mengi ambayo yanaweza kuja mchachia huko mbele ya safari.
 
Sijakuelewa hapa unacholalamika ni nn? Kwamaana tff wanaipendelea Simba nakuihujumu kaizer au nivip? maana naona kama hofu yako ni Simba atashinda dhid ya kaizer kutokana nakupendelewa na tff kwakutocheza mechi ya ligi na kaizer alicheza. Sasa ww nakaizer mpo vp mpaka ulalamike kwaniaba yao?
 
Daaaah yaaani hii inaweza kuwa post ya mtu kilaza wa mwisho hapa JF. Simba ile ile iliyofanya Tanzania kupeleka timu 4 kwenye mashindano ya CAF mwakani! nyie Utopolo kupigania nafasi ya pili ili mwakani mpande ndege halafu unasema Simba inabebwa! Wahi Milembe uchunguzwe wewe una tatizo kubwa sana, au yale Mayai Viza mnayokula kila mechi yameanza kujibu!
 
Unamaanisha wanaipendelea ili ifanye Vizuri Kimataifa si ndio??au kwa kufanya hivyo inaisaidia Simba ichukue ubingwa Bara??Kama Simba na Yanga zote zingekuwa zinashiriki kimataifa halafu moja ndio ikakubaliwa kusafiri bila kucheza Na nyingine ikakataliwa hapo si ndio ingekuwa sahihi kusema team moja inapendelewa??Sasa ktk Hili mwenzako anacheza kimataifa wewe wa hapa hapa tu unalalamika nini?hujagundua tatizo ni we we kuwa wa hapa hapa?
 
Sasa timu inatangaza nchi kimatatifa, wataachaje kuipenda bana!

Hata ungekuwa wewe, timu inafanya vizuri kimataifa utaacha kuipenda kweli? Kwani kinachofanya mchezaji Samatta kupendwa zaidi ya wachezaji wengine wa ki Tz ni nini hasa? Ni mchezaji mzuri na zaidi anatutoa kimasomaso huko "majuu, sio?
 
Umemuweza huyu nyani utopolo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…