TFF yaiomba Simba ufafanuzi juu ya kauli ya Haji Manara dhidi ya waamuzi.

Wazee wa kujipa ushindi kwenye ubora wao. Ni wakati muafaka sasa Simba kutafuta msemaje bora ili walinde heshima ya klabu. Kila zama na kitabu chake.
 
Nafurahi sana kuzidi ' Kujibizana ' na ' Popoma ' kama Wewe humu.
Tafuta elimu usitafute vyeti,tafuta maarifa usitafute kazi weee kikuna!!!sorry niko na wifi yako now Kama hauko bize njoo tu mkune Nazi pamoja.
 
Manara ana hoja za msingi. Tukiwa wakweli hatuwezi kupuuza hoja zake zote.

Tatizo lake anazidisha sana chumvi, kitu kidogo anataka kutuaminisha kuwa ni kikubwa kupita maelezo.

Ni kweli Tshishimbi na Yondani walishika, na refa angeweza kuamua vinginevyo. Tena kosa la Yondani ni dhahiri zaidi maana alizuia kanzu kwa mkono. Ni tuta bila kupepesa macho. Lakini refa naye ni binadamu, halafu hapati muda mzuri wa kuangalia marudio.

Kosa kubwa la Manara ni kumfananisha huyu mwamuzi kijana Herry Sassii na waamuzi wengine wapuuzi walioboronga huko nyuma. Hilo ni kosa kubwa. Huyu dogo Sassii ni nyota ya Tanzania, uwezo wake wa kumudu mchezo na kila kinachoendelea uwanjani ni wa kipekee sana
 
Haji Manara ana upungufu wa akili. Full stop.
Eti yeye mtoto wa mjini. Sijui wa shamba yuko wapi. Angezaliwa London, watu wasingekunywa maji.
 
Hivi kazi kawa maamuzi bora baada ya kuacha u refarii viwanjani. Akumbuke kuwa mwamuzi hakuwa na muda wa kuangalia slow motion ili ajue kama ni penalty au la.
Huyu Kazi ambaye alihongwa laki mbili kule Songea hadi akafungiwa maisha anapata wapi moral authority ya kuwahukumu wengine?
 
kila siku serikali inasema watu wenye mahitaji maalum tuishi nao kwa akili na ubinadamu
 

Manara anatuhumiwa kuwashambulia waamuzi waliochezesha mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya bao 1-1 na Yanga kuonyesha soka safi zaidi ya Simba hasa katika ushambulizi.

Sidhani hiyo sehemu ya pili ya timu moja kuonyesha soka safi kuliko nyingine ipo kwenye maelezo yake bali ni ingizo la mtu mwingine na kwa vigezo visivyoeleweka. Kigezo kimojawapo kingeweza kuwa based on match statistics including ball possession. Zilikuwaje? mengine kila mtu abaki na tathmini yake yaani it's not objective, but rather subjective.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…