TFF yakanusha kuhusu Tanzania kuwa hatarini kuondolewa AFCON 2025 baada ya kukiuka kanuni za Shirikisho la Soka la Afrika (CAF)

TFF yakanusha kuhusu Tanzania kuwa hatarini kuondolewa AFCON 2025 baada ya kukiuka kanuni za Shirikisho la Soka la Afrika (CAF)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeeleza kusikitishwa na taarifa zinazozagaa mitandaoni kuhusu uhalali wa mchezaji Muhamed Ame kuchezea Timu ya Taifa (Taifa Stars).

TFF imefafanua kuwa Ame ni miongoni mwa wachezaji 23 walioorodheshwa rasmi kwa mechi dhidi ya Guinea, na alikaguliwa pamoja na wachezaji wengine na timu pinzani pamoja na Kamishna wa mechi kabla ya kuruhusiwa kucheza.

Pia, Soma: Tanzania hatarini kuondolewa AFCON 2025 baada ya kukiuka kanuni za Shirikisho la Soka la Afrika (CAF)

Mechi hiyo ya mchujo ya AFCON, iliyochezwa jijini Dar es Salaam, ilimalizika kwa ushindi wa 1-0 kwa Taifa Stars, ushindi uliowahakikishia nafasi katika fainali za AFCON 2025.

TFF imeongeza kuwa haina taarifa yoyote rasmi kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuhusu madai ya kutokuwa halali kwa ushiriki wa Ame katika mechi hiyo.
1732202193412.png
 
Tff mkianza kujibu Kila hoja ya Kilaza ntapata taabu Sana, Igeni uongozi wa Yanga Kuna vitu vina jijibu vyenyewe.
 
Tff mkianza kujibu Kila hoja ya Kilaza ntapata taabu Sana, Igeni uongozi wa Yanga Kuna vitu vina jijibu vyenyewe.
Jambo la kitaifa hili au ile 700M imeshagawanywa ?🤣🤣🤣
 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeeleza kusikitishwa na taarifa zinazozagaa mitandaoni kuhusu uhalali wa mchezaji Muhamed Ame kuchezea Timu ya Taifa (Taifa Stars). TFF imefafanua kuwa Ame ni miongoni mwa wachezaji 23 walioorodheshwa rasmi kwa mechi dhidi ya Guinea, na alikaguliwa pamoja na wachezaji wengine na timu pinzani pamoja na Kamishna wa mechi kabla ya kuruhusiwa kucheza.

Pia, Soma: Tanzania hatarini kuondolewa AFCON 2025 baada ya kukiuka kanuni za Shirikisho la Soka la Afrika (CAF)

Mechi hiyo ya mchujo ya AFCON, iliyochezwa jijini Dar es Salaam, ilimalizika kwa ushindi wa 1-0 kwa Taifa Stars, ushindi uliowahakikishia nafasi katika fainali za AFCON 2025. TFF imeongeza kuwa haina taarifa yoyote rasmi kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuhusu madai ya kutokuwa halali kwa ushiriki wa Ame katika mechi hiyo.
 
Sasa hawa TFF watapewaje taarifa wakat Guinea hawajafikisha malalamiko na wao TFF kutakiwa kujibu.

Wasubiri watapata hiyo taarifa, si kuna saa 72 za kukata rufaa
 
Kinacholalamikiwa sio kumchezesha Ibrahim Ame, bali ni Ame kuvaa jezi namba 26 badala ya 24 iliyokuwa inamtambulisha katika orodha ya wachezaji wa Tanzania.

Je, huyo alieingia ni kweli Ame au ni shabiki wa mpira? Isije ikawa waliingiza William Saliba jezi namba 26.
 
Back
Top Bottom