TFF yamfungia maisha Wakili Revocatus Kuuli kujihusisha na soka. Uchaguzi Yanga kufanyika Januari 13

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kupitia Kamati ya Maadili limemfungia maisha kutojihusisha na soka aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati yake ya Uchaguzi, Wakili Revocatus Kuuli baada ya kukutwa na hatia ya makosa matatu ya kimaadili.

Mwenyekiti wa kamati ya maadili ya TFF, Wakili Hamidu Mbwezeleni alisema Kuuli akitambua nafasi yake ndani ya shirikisho hilo, alifanya makosa hayo matatu ambayo kimsingi yanastahili adhabu ya kifungo cha maisha kujihusisha na masuala ya mpira wa miguu.

Makosa matatu ambayo yamemtia hatiani Wakili Kuuli ni kusambaza nyaraka za shirikisho kinyume na kanuni na taratibu, kutoa maelezo yanayoonesha kuwa na mgongano wa kimaslahi kwa kuwapa watu wasiohusika na pia kufanya vitendo vinavyoshusha hadhi ya shirikisho.

"Uamuzi huu umechukuliwa kwa kufuata kanuni na taratibu. Hakuna aliyemuonea Kuuli niliweke hilo sawa," alisema Wakili Mbwezeleni.

Wakati huo huo, Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) kupitia Mwenyekiti Malangwe Mchungahela imetangaza tarehe ya Uchaguzi wa Klabu ya Young Africans utakaofanyika Januari 13,2019,nafasi zitakazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe 4 wa Kamati ya Utendaji
 
Kumfungia maisha maanayake nini? TFF inajishushia hadhi.
 
mtu alikwisha jiuzuru Leo mnakurupuka ooh tumeona tumfungie maisha kujihusisha na soka.kwani alipojiuzuru alisema badae atakuja kuitaka tena hiyo nafasi?
ki ukweli wasomali wao wanajua kuendesha ma benzi na mascania mpira hapana kwa kweli.
 
Kwa kweli TFF ya Karia ime-fail mapema mno, chuki, visasi na kuwapa kazi rafiki zake bila kufuata taratibu wakati huohuo (Mwakyembe na Tenga) i.e wizara na BMT wanamtazama tu. Lo! Tanzania!
 
hii taasisi ishakuwa shamba la bibi...anatoka afadhali anaingia potelea mbali! hapa serikali ichezeshe plan kama waliyochezesha kwa akina malinzi, hatutafika kwa style hii.
 
mtu alikwisha jiuzuru Leo mnakurupuka ooh tumeona tumfungie maisha kujihusisha na soka.kwani alipojiuzuru alisema badae atakuja kuitaka tena hiyo nafasi?
ki ukweli wasomali wao wanajua kuendesha ma benzi na mascania mpira hapana kwa kweli.
Any way Tff hongereni sana kwa hizi pini za maisha. Hongera pia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili kwa kujiona yuko peponi now.
.......
Naona anashindwa tu kuwatangaza kuwa Viongozi wa Tff Ni wa MAISHA pale TFF. Ila bado miaka kadhaa mtawapisha wengine hapo.
 
Who's next.....

1. Danstan Mkundi - Mjumbe wa Kamati ya Utendaji
2. Michael Wambura - Makamu wa Rais
3. Mbasha Matutu - Mjumbe wa Kamati ya Utendaji
4. Revocatus Kuuli - Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi aliyejiuzulu
5. ....................................
 
Kaka Watawala wanataka kuogopwa ili waongoze badala ya kushawishi. Watawala wanatumia Coercive Power. Ni dalili ya uongozi unaokosa ushawishi. Uongozi unaofeli.
__________________
Kiongozi mzuri ni yule mwenye charismatic powerna sio coercive power. Tuko dunia tofauti sana, tuko dunia ambayo huwezi kuwaongoza watu kwa kuwanyamazisha.
 
Kumfungia maisha maanayake nini? TFF inajishushia hadhi.
Maana yake wanachuki na huyo waliyemfungia. Yaani hawataki hata mawazo yake katika maendeleo ya soka hata baada ya wao kuondoka madarakani kama sisi wengine tunayahitaji. Wanajifanya Miungu wa soka.
 
TFF imekamilika kweli.
Rais ni Msomali, gaidi zoefu la vita vya kudumu.
Katibu Mkuu ni Mrundi, Mhutu mpenda vita.

Watanzania tujitathmini kuongozwa na foreigners.
 
dhambi ya ubaguzi Na ukabila waliyoonyesha baadhi ya wachangiaji humu si jambo jema
Hao wote ni watanzania wenzetu sasa tukianza kuchunguzana asili sijui Nani atakuwa msafi Kati yetu
Nadhani hayupi
 
dhambi ya ubaguzi Na ukabila waliyoonyesha baadhi ya wachangiaji humu si jambo jema
Hao wote ni watanzania wenzetu sasa tukianza kuchunguzana asili sijui Nani atakuwa msafi Kati yetu
Nadhani hayupi
Mkuu, labda useme Waafrika wenzetu lakini si suala la ukabila hili. Mtanzania anaweza kuwa Rais wa FA Somalia?
Je? anaweza kuwa Katibu Mkuu wa FA Burundi?
Alikuwepo Makamu Mwenyekiti wa FAt wakati ule. Aliumbuka baada ya kugombea Ubunge. Ikaonekana ni Mkenya hadi leo yupo kwao Kenya
 
Mbona yuko mtanzania ni mbunge pale Pakistan
 
Mbona yuko mtanzania ni mbunge pale Pakistan
Mbona Msomali Rage hakuna anayempigia kelele? Huyo Kidia ni mkimbizi, full stop. Karia ni hao hao. Sasa wanaongoza kwa mihemuko ya damu za kwao proper. Hawataki kupingvwa kwa lolote hata likiwa sahihi.
 
Tatizo lako unachanganya ukabila Na utaifa
Hivi ni vitu viwili tofauti mfano Obama ni kabila la kutoka Kenya Lakini ni mmarekani
 
Tatizo lako unachanganya ukabila Na utaifa
Hivi ni vitu viwili tofauti mfano Obama ni kabila la kutoka Kenya Lakini ni mmarekani
Siwezi kufika level ya chini kiasi cha kuchanganya utaifa na ukabila. Ndiyo maana nimekupa mfano wa Aden Rage na yule Mkenya aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa FAT wakati huo. Kidia ni mkimbizi. Hakuna cha zaidi. Na mkimbizi anabaki na uraia wa wazazi wake. Ni sheria ya kimataifa. Haina mjadala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…