Mwalimu Demitria Gibure
Member
- Jul 27, 2022
- 94
- 134
Kuna namna nyingi binadamu wa sasa tunazitumia kuonesha thamani ya mtu.
Wengine tunamthamini mtu pindi tu tunapokuwa na uhitaji yaaani anakuwa na thamani pindi anaponipa huduma fulani ila ikiisha tu na thamani yake pia inapungua, inaisha ama inapotea kabisa.
Kuna Wengine tunawathamini kwa vipindi, yaaani wana thamani kwenye shida ama tunapohitaji michango yao kwenye shughuli zetu mbalimbali.
Ila tukumbushane tu ule msemo usemao "Thamani ya mtu huonekana pindi anapotoka katika mzunguko wako wa maisha/kazi" tuutunze uthamani wa kila binadamu tuliyeruhusu aingie katika maisha yetu.
Tuutunze uthamani kwa kujuliana hali, kutiana moyo, kushauriana na kuwasiliana mara kwa mara inapobidi ili tukikutana na uhitaji wa namna yoyote ile iwe rahisi kushikana mikono.
Hurka ya binadamu ni kukosea, kuna waliosema hata vikombe kabatini hugongana hivyo msamaha uwepo baina yetu ili tuendelee kutunza thamani ya kila mmoja wetu.
NAKUTHAMINI RAFIKI YANGU.
Wengine tunamthamini mtu pindi tu tunapokuwa na uhitaji yaaani anakuwa na thamani pindi anaponipa huduma fulani ila ikiisha tu na thamani yake pia inapungua, inaisha ama inapotea kabisa.
Kuna Wengine tunawathamini kwa vipindi, yaaani wana thamani kwenye shida ama tunapohitaji michango yao kwenye shughuli zetu mbalimbali.
Ila tukumbushane tu ule msemo usemao "Thamani ya mtu huonekana pindi anapotoka katika mzunguko wako wa maisha/kazi" tuutunze uthamani wa kila binadamu tuliyeruhusu aingie katika maisha yetu.
Tuutunze uthamani kwa kujuliana hali, kutiana moyo, kushauriana na kuwasiliana mara kwa mara inapobidi ili tukikutana na uhitaji wa namna yoyote ile iwe rahisi kushikana mikono.
Hurka ya binadamu ni kukosea, kuna waliosema hata vikombe kabatini hugongana hivyo msamaha uwepo baina yetu ili tuendelee kutunza thamani ya kila mmoja wetu.
NAKUTHAMINI RAFIKI YANGU.