Thank you Madam Agness

Thank you Madam Agness

TUKANA UONE

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2018
Posts
2,345
Reaction score
6,970
Nikiwa shule ya msingi kuna mwalimu mmoja alikuwa anaitwa AGNESS, huyu alikuwa mjaluo kutoka huko mkoani Mara, kiukweli alikuwa mzuri wa sura na umbo, huyu mwalimu sitokuja kumsahau hadi naingia kaburini kwasababu alikuwa kisu kwelikweli, kwa leo ndiyo wanaitwa "PISI KALI".

Huyu mwalimu kuna siku aliletwa pale shuleni na gari aina ya Limoussine na akashushwa kwa madaha, kiukweli wakati huo kabla hata sijabalehe lakini nilikuwa nina ufahamu wa kizuri ni kipi na kibaya ni kipi!.

Miaka hiyo kutembelea Limousine haikuwa kitu rahisi kama mnavyodhani, ilikuwa unaonekana wewe ni tajiri kweli kweli!

Yule mwalimu alikuwa mzuri ajabu na wanaume wenye ukwasi walimsalandia kila mara pale shuleni, yule mwalimu alikuwa anaonekana mara 2 kwa wiki pale shuleni, siku nyingine alikuwa hapatikani, kwa bahati nzuri au mbaya alikuwa mwalimu wetu wa darasa.

Sababu ya yeye kutokuonekana ilikuwa ni wanaume waliokuwa wakimchukua wakishinda naye kwenye starehe.

Alikuwa mzuri sana na kiukweli huwa nikikumbuka namna alivyokuwa, huwa natamani siku zirudi nyuma nitamani kumuona tena😭😭


Daaah!!.

Juzi moja nilikuwa naongea na classmate wa shule ya msingi wa huko mkoani ananiambia huyo mwalimu alifariki kitambo sana kwa ugonjwa wa Upungufu wa kinga mwilini.

Kiukweli nimelia na kusikitika sana namna nikikumbuka alivyokuwa akiniachia madaftari nisahihishe mimi na mwanafunzi mwenzangu Monica ambaye naye ni Marehemu yaaani nabaki kulia tu 😭😭😭😭

Miaka hiyo ya 1993 namna madam Agness alivyokuwa mzuri halafu nimeambia amekufa nabaki najiuliza sana,laiti angeutunza uzuri wake leo angekuwa mtu mkubwa sana, kipindi kile najua alishawishiwa na gari za kifahari pamoja na fedha za wanaume akaingia mkenge kumbe alikuwa anajichimbia kaburi!😭😭😭😭😭.

Mwaka 1994 ulituharika kwako mimi na Monica hapo kwako kusherehekea Siku kuu ya Christmas, ulitupikia tukala nyama ya bata na pilau zuri kisha wewe ukaja kuchukuliwa na gari aina ya pigeout ukaondoka ukalala hatimaye ukaja kesho yake ukinukia marashi mazuri yenye kupendeza,ulitupatia mimi na Monica shilingi 200 ambazo tuligawana kila mmoja shilingi 100 na kiukweli tuliyafurahia maisha sana kwasababu hiyo hela ilikuwa kubwa mno!.

Ooooh Madam Agness I Cry for you & miss u so much,nitakukumbuka daima,umeondoka na uzuri wako!😭😭😭😭😭

THANK YOU MADAM AGNESS TUTAONANA ASUBUHI ILIYO NJEMA.
 
Nikiwa shule ya msingi kuna mwalimu mmoja alikuwa anaitwa AGNESS, huyu alikuwa mjaluo kutoka huko mkoani Mara, kiukweli alikuwa mzuri wa sura na umbo, huyu mwalimu sitokuja kumsahau hadi naingia kaburini kwasababu alikuwa kisu kwelikweli, kwa leo ndiyo wanaitwa "PISI KALI".

Huyu mwalimu kuna siku aliletwa pale shuleni na gari aina ya Limoussine na akashushwa kwa madaha, kiukweli wakati huo kabla hata sijabalehe lakini nilikuwa nina ufahamu wa kizuri ni kipi na kibaya ni kipi!.

Miaka hiyo kutembelea Limousine haikuwa kitu rahisi kama mnavyodhani, ilikuwa unaonekana wewe ni tajiri kweli kweli!

Yule mwalimu alikuwa mzuri ajabu na wanaume wenye ukwasi walimsalandia kila mara pale shuleni, yule mwalimu alikuwa anaonekana mara 2 kwa wiki pale shuleni, siku nyingine alikuwa hapatikani, kwa bahati nzuri au mbaya alikuwa mwalimu wetu wa darasa.

Sababu ya yeye kutokuonekana ilikuwa ni wanaume waliokuwa wakimchukua wakishinda naye kwenye starehe.

Alikuwa mzuri sana na kiukweli huwa nikikumbuka namna alivyokuwa, huwa natamani siku zirudi nyuma nitamani kumuona tena😭😭


Daaah!!.

Juzi moja nilikuwa naongea na classmate wa shule ya msingi wa huko mkoani ananiambia huyo mwalimu alifariki kitambo sana kwa ugonjwa wa Upungufu wa kinga mwilini.

Kiukweli nimelia na kusikitika sana namna nikikumbuka alivyokuwa akiniachia madaftari nisahihishe mimi na mwanafunzi mwenzangu Monica ambaye naye ni Marehemu yaaani nabaki kulia tu 😭😭😭😭

Miaka hiyo ya 1993 namna madam Agness alivyokuwa mzuri halafu nimeambia amekufa nabaki najiuliza sana,l aiti angeutunza uzuri wake leo angekuwa mtu mkubwa sana, kipindi kile najua alishawishiwa na gari za kifahari akaingia mkenge kumbe alikuwa anajichimbia kaburi!😭😭😭😭😭.

Mwaka 1994 ulituharika kwako mimi na Monica hapo kwako kusherehekea Siku kuu ya Christmas, ulitupikia tukala nyama ya bata na pilau zuri kisha wewe ukaja kuchukuliwa na gari aina ya pigeout ukaondoka ukalala hatimaye ukaja kesho yake ukinukia marashi mazuri yenye kupendeza,ulitupatia mimi na Monica shilingi 200 ambazo tuligawana kila mmoja shilingi 100 na kiukweli tuliyafurahia maisha sana kwasababu hiyo hela ilikuwa kubwa mno!.

Ooooh Madam Agness I miss u so much,nitakukumbuka daima,umeondoka na uzuri wako!😭😭😭😭😭

THANK YOU MADAM AGNESS TUTAONANA ASUBUHI ILIYO NJEMA.
R.I.P dada neema licha ya kunipita umri tulikua ni ndugu tulio elewana vyema sikuwai kua mbishi kwako.............

Ulikua pisi kali mrembo wa umbo na sura na uliwatoa udenda WANAUME wakwale....

I wonder ulizidisha sana kusaidia watu na kutoa michango ya kijamii na mara nyingi ulinichukua nikusindikize kwenye kaburi la mama ako mzazi kufanya usafi na ulikua ukisali Kwa hisia sana Mimi sikuwai kujua kama ulikua unaishi na VVU

Kifo chako Bado kilinipa mawazo na funzo kubwa sana pumzika Kwa amani Dada angu
 
R.I.P dada neema licha ya kunipita umri tulikua ni ndugu tulio elewana vyema sikuwai kua mbishi kwako.............

Ulikua pisi kali mrembo wa umbo na sura na uliwatoa udenda WANAUME wakwale....

I wonder ulizidisha sana kusaidia watu na kutoa michango ya kijamii na mara nyingi ulinichukua nikusindikize kwenye kaburi la mama ako mzazi kufanya usafi na ulikua ukisali Kwa hisia sana Mimi sikuwai kujua kama ulikua unaishi na VVU

Kifo chako Bado kilinipa mawazo na funzo kubwa sana pumzika Kwa amani Mkuuu usinilize mie
Umejua kuniliza mie mkuu,why lakini 😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭
 
Apumzike anapostahili mwl wako.
Nyako huwa sio wachoyo siku zote. Hiyo imepelekea mkoa wa mara hasa rorya kuwa ndio kinara wa maambukizi.
 
Umejua kuniliza mie mkuu,why lakini 😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭
Sorry mkuu,
Umenikumbusha dada angu yaan kipindi Fulani alizidisha sana ibada na kufanya Charity activities......

Siku wai kujua ni Kwa nini alifanya vile saidia sana watu toa michango Mingi sana Kwa jamii....

Ndio ivyo tena aliambukizwa maradhi sababu ya uzuri wake.....
 
Nikiwa shule ya msingi kuna mwalimu mmoja alikuwa anaitwa AGNESS, huyu alikuwa mjaluo kutoka huko mkoani Mara, kiukweli alikuwa mzuri wa sura na umbo, huyu mwalimu sitokuja kumsahau hadi naingia kaburini kwasababu alikuwa kisu kwelikweli, kwa leo ndiyo wanaitwa "PISI KALI".

Huyu mwalimu kuna siku aliletwa pale shuleni na gari aina ya Limoussine na akashushwa kwa madaha, kiukweli wakati huo kabla hata sijabalehe lakini nilikuwa nina ufahamu wa kizuri ni kipi na kibaya ni kipi!.

Miaka hiyo kutembelea Limousine haikuwa kitu rahisi kama mnavyodhani, ilikuwa unaonekana wewe ni tajiri kweli kweli!

Yule mwalimu alikuwa mzuri ajabu na wanaume wenye ukwasi walimsalandia kila mara pale shuleni, yule mwalimu alikuwa anaonekana mara 2 kwa wiki pale shuleni, siku nyingine alikuwa hapatikani, kwa bahati nzuri au mbaya alikuwa mwalimu wetu wa darasa.

Sababu ya yeye kutokuonekana ilikuwa ni wanaume waliokuwa wakimchukua wakishinda naye kwenye starehe.

Alikuwa mzuri sana na kiukweli huwa nikikumbuka namna alivyokuwa, huwa natamani siku zirudi nyuma nitamani kumuona tena😭😭


Daaah!!.

Juzi moja nilikuwa naongea na classmate wa shule ya msingi wa huko mkoani ananiambia huyo mwalimu alifariki kitambo sana kwa ugonjwa wa Upungufu wa kinga mwilini.

Kiukweli nimelia na kusikitika sana namna nikikumbuka alivyokuwa akiniachia madaftari nisahihishe mimi na mwanafunzi mwenzangu Monica ambaye naye ni Marehemu yaaani nabaki kulia tu 😭😭😭😭

Miaka hiyo ya 1993 namna madam Agness alivyokuwa mzuri halafu nimeambia amekufa nabaki najiuliza sana,l aiti angeutunza uzuri wake leo angekuwa mtu mkubwa sana, kipindi kile najua alishawishiwa na gari za kifahari akaingia mkenge kumbe alikuwa anajichimbia kaburi!😭😭😭😭😭.

Mwaka 1994 ulituharika kwako mimi na Monica hapo kwako kusherehekea Siku kuu ya Christmas, ulitupikia tukala nyama ya bata na pilau zuri kisha wewe ukaja kuchukuliwa na gari aina ya pigeout ukaondoka ukalala hatimaye ukaja kesho yake ukinukia marashi mazuri yenye kupendeza,ulitupatia mimi na Monica shilingi 200 ambazo tuligawana kila mmoja shilingi 100 na kiukweli tuliyafurahia maisha sana kwasababu hiyo hela ilikuwa kubwa mno!.

Ooooh Madam Agness I miss u so much,nitakukumbuka daima,umeondoka na uzuri wako!😭😭😭😭😭

THANK YOU MADAM AGNESS TUTAONANA ASUBUHI ILIYO NJEMA.
Umeniaminisha kuwa tabia ya kupenda wanawake huanza kwa mwanaume akiwa kinda!

Miye ilinitokea nikiwa dogo kabisa nadhani nikiwa na miaka7 darasa la kwanza kumpenda kifara mwalimu wa darasa wa kike!

Nadhani asingelihamishwa, huenda ningelibadili madarasa bila ya kuelewa chochote cha maana hasa cha somo lake!

Alikuwa ni mwalimu wa "mwandiko", akiingia akili zangu zina"staki",hazifanyikazi nikibaki kumshangaa yeye kwa uzuri wake!

Kuna siku aliniadhibu wakati najifunza kuandika, lakini sikusikia maumivu!

Nilikosea akanifinya masikio na kunikoa kwenzi, cha ajabu nilisikia raha badala ya maumivu!

Sasa nilikuwa najiuliza siku zote mwanaume yanakutokeaje hayo kabla ya balekhe?

Kupitia kwako nimepata majibu kuwa "mtoto wa nyoka hafundishwi kuuma"!
 
"hili swali najiuliza kwa kijana kama mimi, najikinga vp na sura nzuri zimevaa ukimwi?" mwisho wa kunukuu
 
nilibahatika kupendwa na maticha wa kike na pisi za shule(wanafunzi wa kike) ila hii kichwa ilikuwa busy na kupiga msuli nikikumbuka dah......
 
Back
Top Bottom