Duh, hata wewe umerudi! Kweli Warriors waliwapa kifungo watu kibao humu ndani, mpaka hata kunusa tu thread ya Basketball walikuwa hawathubutu. Labda na
Raimundo naye atakuwa njiani, karibuni sana tena na safari hii nawaomba tafadhali sana mtulie, msije mkaanza tena zile hadithi zenu!
LeBron tulipomnyang'anya kwa mara ya kwanza, jamaa alilia kama mtoto mdogo hadi ikabidi tumtulize kidogo mwaka uliofuata kwa kumuachia angalau apumue kidogo. Hatukusita kumnyang'anya tena kelele zake zilipozidi ikabidi akimbilie kwa ndugu zetu Lakers. Huko nako hatukumpa hata nafasi ya kupumua...masikini LeBron!
Leo eti ushabiki wenu umehamia kwa Toronto! Watu kweli mna roho ngumu, who in the world are Raptors? Kahwi tuliyempiga akiwa San Antonio au Ibaka aliyeikimbia OKC bila kuaga baada ya kile kichapo! Mnasahau, eh! Mimi roho hata hainiumi, jina Warriors tu lilikimbiza watu humu na kubaki tu wakichungulia kutoka mafichoni. Acheni hizo...ha ha haaa!
...it aint over till it's over!