The FALL oF UDSM?

Kwikwikwi, hapo niko puzzled mkuu. Mtoto wa high school au first year hapa viwanja anaweza kuacha masomo na kuanzisha Microsoft, napter au facebook. Na mtu anaondoka na first class bongo anashindwa kutengeneza spoku ya biskeli.

Hapo sasa.....na ukifikiri sana mwishowe utarudi kulekule kwenye kauli mbiu yangu ingawa najua kwa wengi ni vigumu kukubali
 
Hilo ni kutokana na msukumo wa siasa uliopo. Ukiisha, hadhi ya UDSM itaendelea. UDSM ina historia ndefu na ningependa kila mmoja wetu apitie pale.
 

Hujajibu swali, ngoja nilirahisishe: Je, hizo State University hazipewi mshiko wa kufa mtu na Serikali zao/yao? Je, sasa haziweweseki pia kwa kuwa mtafaruku wa Uchumu dunianiani unasababisha hilo fungu lipungue? Je, vyuo vya Umma Tanzania venyewe havistahili ruzuku hiyo pia?

PS. Kama suala ni competition tayari kuna vyuo binafsi vya kumwaga Tz ambavyo vinastahili kuleta hiyo competition dhidi ya vyuo vya umma!
 
Hapo sasa.....na ukifikiri sana mwishowe utarudi kulekule kwenye kauli mbiu yangu ingawa najua kwa wengi ni vigumu kukubali

Mvumbuzi wa Mpemba Effect hawezi kutengeneza spoku ya baiskeli kama anavyodai Zakumi? Halafu first class wangapi anawajua kuwa hawawezi? Kaulimbiu yako inabidi irekebishwe na kusomeka hivi: MIAFRIKA NDIVYO ILIVYO INAPOKUBALI KUWA KAMA ILIVYO MAHALI ILIPO!
 

Jana kuna jamaa mmoja ali graduate UD aliniambia kuwa katika kozi yao ya miaka minne, vitabu ambavyo walimu waliwashauri wasome katika ngazi mbalimbali vilikuwa ni zaidi ya arobaini. Ila mpaka anamaliza alisema vitabu visivyozidi vinne. Hakuwa kuingia library kluazima kitabu chochote maana nyenzo pekee ilikuwa madesa.
Wanafunzi wa aina hii baadae kwa kutumia GPA zao za madesa ndio wanakuwa walimu. Tutegemee nini? Kama wakisogea mpaka wakawa maraisi au wabunge au makatib wakuu tutegemee nini?
Guys elimu yetu yote ina kasoro kubwa tusijidanganye kuwa mambo yako sawasawa. Vinginevyo tuendelee kujenga majengo mengi na kutengeneza wataalamu ambao sio wabunifu na wasio na msaada wowote kwa Taifa hili.
Mfano wa madudu ya kisomi tunayofanya ni Research center inayoitwa REDET> Duuu! Kama vile hawajasoma
 

Poleni sana
 
Chuo kimeshindwa kutoa product tulizotegemea miaka 50 no improvement tunatoa watu ambao hawana msaada kwa taifa zaidi ya kulinyonya taifa wameshindwaje kujisimamia miaka 50 kwa nin serikali isifikirie kuwekeza sehem ambayo inafikiri itakuwa productive kuliko kuendelea kumlisha ng'ombe ambaye hatoi maziwa tunayo yataka? wanafanya research ambazo hazina effect katika jamii yetu wanaweka makabatini tu.mtoto miaka miaka 50 hatembei.saiz ana mdogo wake ndio anayestahili msaada zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…