The internet is still undefeated

The internet is still undefeated

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Mwishoni mwishoni mwa hotuba ya Rais Samia kazungumzia mambo ayaonayo mitandaoni.

Mambo ya kizushi, ya kuchonganisha, na kila aina ya uzandiki.

Ni jambo jema. Ni jema kwa sababu linaonyesha haishi peke yake kwa kujitenga kwenye puto alimo yeye tu mwenyewe.

Anafuatilia kinachoendelea na kinachojiri kupitia yale wayasemayo watu awaongozao.

Ila, haya mambo inabidi awe makini nayo sana. Ni mara kadhaa ameyazungumzia haya yajiriyo kwenye mitandao.

Ni kana kwamba naye ‘anademka’ kwa yale yajiriyo huko.

Natumaini hataendelea kuyapa umuhimu kivile, la sivyo ataishia kucheua tu kwani the internet is still undefeated.
 
Mkuu heshima kwako,
Internet isn't that bad..
Mazuri acjukue ayafanyie kazi, uzush na uzandiki awaachie..
Kusema aachane na internet ni kujidanganya..
Kuwasikiliza wanasiasa pia wengi wana uzandkki na uzushi na maslahi...
She should w'man up enough to know the difference
 
Mkuu heshima kwako,
Internet isn't that bad..
Mazuri acjukue ayafanyie kazi, uzush na uzandiki awaachie..
Kusema aachane na internet ni kujidanganya..
Kuwasikiliza wanasiasa pia wengi wana uzandkki na uzushi na maslahi...
She should w'man up enough to know the difference
She shouldn’t pay them that much attention, at least not publicly.

By talking about them publicly and on several occasions, she gives the internet warriors, thugs, and activists, the satisfaction of knowing that they are in her head.

Not a good look.

She will never win going against what is said on the internet.
 
Mama nimemwelewa sana kuhusu watu wanaosema hayati alipewa sumu
Ni kama alilenga kuwaambia naona,na najua mnachofanya!
As alienda direct kwenye point hiyo tu!
The msg was indeed sent!
Viva mama
Kazi na iendelee
 
Samia anakuwa na tabia kama za Magufuli anashindana na technolojia,anatakiwa kuwa kama Kikwete ya mitandao ayaache kama yalivyo aendelee na kazi zake.
Yaani sasa hivi wale jamaa wa Jamhuri ya Muungano wa Twitter na Ufipa wanajua kuwa wanamkera huyo mama.

Hahahaa aache kudemka na ngoma wazipigazo.
 
Binafsi mimi pia nimeshangaa sanaa mama kuzungumzia mambo ya mitandaoni tena uzushi na umbea wa mitandaoni. Inaonekana ni mambo yanayomkwaza na hawezi kuyamezea yakapita.

Kwa mtindo huu basi mama atakwazika sana na mambo ya mitandao maana uzushi hauishi, ni kila siku watu waibua uzushi.

Mambo mengine anyamaze tu yapite. Kiongozi mkubwa wa nchi kuanza kujadili mambo ya mitandaoni tena ya uzushi ni ajabu sana.
 
Alishasema Rugeley, tumwogope Mungu na Teknolojia . Ko mama anaanza na Kigogo sasa au Veronica???
 
Chukua zako tano. Anarudia makosa yale yale ya Magufuli. Haya mambo akitaka yaishie hewani asiyape umuhimu wowote kwenye hotuba zake. Kama anasoma ayaache huko huko. Na ujinga zaidi ni kujaribu kuwasaka wanaondika. Huku ni kupoteza muda bure.
 
She shouldn’t pay them that much attention, at least not publicly.

By talking about them publicly and on several occasions, she gives the internet warriors, thugs, and activists, the satisfaction of knowing that they are in her head.

Not a good look.

She will never win going against what is said on the internet.
Yee. Kwa mfano aliyemzungumzia leo nadhani ni yule wa Facebook anayejiita ''Veronica France'' anayesema Magufuli kauawa na Kikwete. Rais anajishushia heshima kujaribu kulumbana na mtu kama yule. Kwanza kwa mtu mwenye weledi wa kusoma between the lines unajua kabisa huyo ''Veronica'' ni kilaza mmoja tu asiye na upeo wowote. Rumours za viongozi wanafariki kuwa waliuawa au kufa katikati mazingira fulani zipo siku nyingi tu. Hata Sokoine, Nyerere, Kolimba nk kuna nadharia nyingi za bla bla kuhusu vifo vyao lakini viongozi wa enzi hizo walikuwa wanazipuuza.
 
Hata mimi nimeitazama na kusikiliza hotuba yake mwanzo mwisho...

Ni hotuba nzuri, lakini akaharibu hapo mwishoni...

In my opinion, kukerwa kwake na "rumours" nani au nini kilimuua Mwendazake zinazovumishwa kwa kasi sana mitandaoni, ni ishara kuwa kuna ukweli hawataki ujulikane juu ya kifo cha JPM...

As you've said, internet can never be defeated..

Sasa ni kama amechokoza nyuki. Zitatoka ktk mzinga na kumrarua kila aliye mbele..

Asingeng'aka hadharani kwa hili..
 
Naamini lengo lake lilikuwa kuwajulisha hajali wanachosema, so regardless na kelele zao anaendelea kupiga kazi, na wale wanaopigiwa chapuo na hao jamaa kwenye mitandao ili wapate teuzi ndio wasahau kabisa.
 
Mbona hukuona ajabu sana jiwe alipokuwa anaongelea mambo ya mtandaoni??
Binafsi mimi pia nimeshangaa sanaa mama kuzungumzia mambo ya mitandaoni tena uzushi na umbea wa mitandaoni. Inaonekana ni mambo yanayomkwaza na hawezi kuyamezea yakapita.

Kwa mtindo huu basi mama atakwazika sana na mambo ya mitandao maana uzushi hauishi, ni kila siku watu waibua uzushi.

Mambo mengine anyamaze tu yapite. Kiongozi mkubwa wa nchi kuanza kujadili mambo ya mitandaoni tena ya uzushi ni ajabu sana.
 
Back
Top Bottom