The Manchester City (The Citizens) | Special Thread

Mkuu tupo 10point top of the table

Kupoteza game na westham kudrop point 3 ,man utd anaweza kucheza kwa high energy akijua point 7 si kitu bado tunamatch nae ...

Mim binafsi nitahesabu ubingwa tukimpiga man utd ,gap litakuwa limeongezeka atleast ,kupoteza saizi ni kuanza kucheza kwa pressure....


Kipind cha kwanza tulicheza vibaya sana ,aguero ,Torres Kule mbele walikuwa useless ,usifikili nilitype bila sababu timu ikiwa form mbaya lazima tuseme ....
 
Arsenal kanisimamishia lecister city

Chelsea akimsimamisha man utd nadhan tutakuwa tunazid kuongeza gap ...

Tuna game na

Man utd

Lecister city


Tukimaliza hizo game basi EPL itakuwa imefika city ....

Cityzen chairman
 
Mkuu achana na EPL kabisa ,ile table sio mpaka game ziishe ..

Nakumbuka wakati tunachukua ubingwa kwa point 1 dhid ya Liverpool ,alikuwa mbele kwa point 7 kama mistake ambayo tungefanya ...

Alijichanganya akatoka draw ya kizimbe na man utd ,akatoka draw na westham ,na game nyingine za hovyo huku akijihakikishia EPL anachukua ,! Pep alitembelea humor humo..!

Alikuja etihad akala 2-1 na ubingwa ulikuwa umeishia hapo ,alibaki anafukuza kwa point moja bila mafanikio .....

Kama tunataka EPL hakuna haja ya kupoteza saizi ,...!
 
KDB.
Amatoka majeruhi ,anahitaji dakika nyingi kucheza ili arudi kwenye form yake ..

Penetration pass nyingi anazopiga saizi zinakuwa blocked, labda uimara Wa westham ,...

Aguero sijajua tatizo ni nin, ila namuona akishindwa kugombania namba yake pale mbele foden anampiku kabisa , ,..

Saizi pep anacheza bila striker naona huo mfumo anaanza kuukubali ,sitoshangaa kuona aguero akiondoka mwishon mwa msimu huu ,najua anahistoria kubwa sana etihad but inaweza kuwa hivo ...!
 
Huyu jamaa ni fundi sana ila sijui msimu huu kaingiwa na pepo gani kama simuelewi elewi vile.
 
Timu haiwezi kucheza kwa form ile ile kila siku. Pia kuna wakati timu inaperform ovyo kwasababu ya tabia ya Pep ya kurotate wachezaji mara kwa mara. Cancelo na Bernardo ni wachezaji ambao wanaipa timu uhai mkubwa sana katika kushambulia na kukaba, lakini mechi ya West Ham walianzia benchi. Itafikia kipindi Pep anatakiwa awe na kikosi cha kwanza kinachotambulika, hii itasaidia sana, hasa kwenye mashindano yanayohitaji userious mkubwa.
Nikukumbushe tu, hata msimu uliopita tulitolewa UEFA kwasababu ya tabia ya Pep ya kurotate wachezaji, hii inaweza kutugharimu tena na msimu huu.
 
Kwa kuongezea tu, kwasasa Man City inamuhitaji zaidi Gabby Jesus kuliko inavyomuhitaji Aguero, mfumo wa sasa wa Pep unahitaji mshambuliaji ambaye anakimbia muda wote, iwe timu inaposhambulia au timu inavyokaba. Aguero hawezi kuifanya hii kazi.
 
Ni kweli kabisa,hii tabia yake sio nzuri kabisa alafu ni mziko hata kufanya sub. Moja ya mapungufu ya huyu kocha ni hilo kujifanya ni mtu asiyetabilika kuwa mjuaji sana kupitiliza.
 
Kufanya rotation knock out stage kwa game zenye pressure ni hatari sana...

Anafanya hivo kupumzisha wachezaji najua ,siku hizi baada ya siku mbili ni game ..
 
Wakati mwingine huwa ana makusudi ya kujua yeye tu aise.
 
Ni kweli kabisa,hii tabia yake sio nzuri kabisa alafu ni mziko hata kufanya sub. Moja ya mapungufu ya huyu kocha ni hilo kujifanya ni mtu asiyetabilika kuwa mjuaji sana kupitiliza.
Mi nafikiri tuache mihemko, wale ni binadamu walihitaji kupumzika pia. Kumbuka walitoka kucheza jumatano afu Jumamosi game na Leo jumanne kuna game pia. Kila baada ya siku mbili kuna game.
Tukumbuke pia kua tunahitaji vikombe vyote hivyo rotation ni muhimu ili pia kumuweka tayari kila mchezaji kwa mchezo.
NB. Kuwafanya Wachezaji wote wajisikie part ya timu kunahitaji rotation,, wale ni binadamu asipopata game time ni anaathirika kisaikoloji
 
Tunaelewa Broh.
Ila hauwezi kumuweka mchezaji wako bora benchi katika hatua ya mtoano UEFA.
 
Haland 2014 akiwa wembley na baba yake kwenye fainali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…