Washauri wajikite zaidi kwenye fani ya lundenga labda huko tunaweza fanikiwa kiasi....kwikwikwikwi.me nahisi mpira si fani yetu, nadhani tujikite zaidi kwenye riadha maana imeshaonekana mpira hata hela ikiwa nyingi na facilities zikiwepo bado hamna kitu mfano Canada, japan, qatar,na nchi nyingine hamna mpira huko lakini angalia Brazil mambo mswano
bila shaka jamaa ni mwanasiasahivi jamani, ishu ni kwa vile analipwa na serikali au? kwa wafuatiliaji wa soka, Maximo kazidiwa kidogo sana na Santana aliyetimuliwa South, ni aina ya makocha ambao wanatengeneza 'make-shift' like teams, au kwa wale ALCHEMISTS, kwamba anatengeneza dawa, tester mgonjwa!!!...kwa mwendo huu hatufiki..nionavyo mimi huyu bwana apewe timu za vijana, labda ndio atatengeneza timu...otherwise, itakuendelea kuwa ni shauku tu na si mikakati...
Kaka leo unaongea kidokta dokta sana. Mimi naogopa kufananisha kifo na maisha, unajua kwanini? Kifo kiko nje nje zaidi ya uhai zaidiUlinganisha uhai na kifo? Death and life are far apart!
..Kwa nini Simba isingewakilisha Tz kwenye challenge lazima wangerudi na kombe!!! Phiri yuko juu!!..utawasikia sasa hivi wale wa homa ya manjano!!!!!!!!!!!!!!
Anatabia zote za aliye mletaMaximo ni mpiga kelele anaendesha soka kiswahili-swahili kuliko waswahili wenyewe, nimeamini kweli wabrazil wengi ni matokeo ya biashara ya utumwa wa Afrika mashariki, yaani kitabia anafanana sana na ndolaga, Rage na Waendesha soka wengine hapa Dar es salaam aambiliki, ni kiziwi na mtu anayepigania sifa ambazo mwisho wa siku tumekua mabingwa wa kushinda mechi nyingi za krafiki kuliko za kimashindano.
Maximo hawezi kuleta jipya aliyoleta katika soka letu yanatosha kwa uwezo wake kiufundi ,kimawazo na kiakil.
Kwanza ni kichekesho kusema eti mtu kama Chuji hana uzalendo!!!!! tuacheni masihara jamani, hivi hapa TZ kuna mchezaji anayejituma uwanjani kwa kumuacha chuji mbali? ni uzalendo gani anaozunguzmia kwamba Chuji na Boban hawana uzalendo? Hivi ni utovu wa nidhamu gani uliovuka mipaka kiasi hicho alionao Chuji, Boban na kaseja kiasi kwamba wasiwe na thamani yoyote ile? inauma sana, na leo naomba bara watunguliwe hata 10, maana ni upuuzi huu! ndio, upuuzi? kwanini anataka kuwafanya wachezaji wawe wanacheza kwa tension? sio siri, siku hizi wachezaji wetu wanapenda sana kuchezea stars, lakini kwa upuuzi huu watashindwa kujiamini uwanjani kwavile wanajua wakifanya kosa tu, watatemwa kikosini. hivi ni wendawazimu kiasi gani kwa timu yetu isione umuhimu wa chuji na boban? Anyawa, mi sio mfuatiliaji sana wa soka la ulaya nikilinganisha na la hapa nyumbani. Hivi yule jamaa anayeitwa sijui Ruuni (Roney) sijui nani sijui, mbona limekaa kisharishari tu?hachezeagi england yule jamaa? Hivi Chuji au kaseja au boba amefikia kiwango cha Paul Ince? hivi yule jamaa alikuwa hachezei england yule? Hivi utovu wa nidhamu anaozungumzia maximo ni wa nje ya uwanja au ndani ya uwanja? naogopa usije ukawa ni utovu wa nidhamu wa kutaka kula anavyokula bosi manake nasikia hata Rijicard(spell it correctly, nishasema sijui lolote kuhusu soka ya ulaya, ila aka kajamaa kalikua kanufundisha barcelona, au manchester? lol) alim-mind yule jamaa wa kucheka cheka (sijui anaitwa Ronadinhyo) baada ya kumparamia binti yake , lol! ni utovu gani anaozungumzia maximo? Zanzibar, bamiza hao jamaa 10-0 ili tuhashimiane!! Hivi baada ya miaka 3 hii atajivuna nini? au kuipeleka CHAN? kama Sudan wasingefanya mchezo wa kuweka vijana wa shuleni unafikiri hata huko CHAN tungeenda? kama mara mbili mfululizo anashindwa hata kuleta Challenge, ataweza kombe gani huyu bwa mdogo? hivi ktk afrika hii kuna eneo lolote ambako soka ipo chini zaidi ya ukanda wa wana-CECAFA?Sasa kama kashindwa hata kuwa tishio kwa wachovu wenzetu, tutakuwa tishio kwa nani? Hivi, ni kweli kocha hawezi kuingiliwa maamuzi yake hata kama anaharibu? Hivi ni kweli soka limekua kutokana na ujio wa maximo au participation ya mkulu wa kaya na wafadhili kumeongeza morali? hivi miela yote inayomwagwa imesaidia nini? Pamoja na kwamba Patrick Phill simpendi kv anapenda sifa (jitu gani kila akiichukua simba inafanya vizuri, ebo!) naaamini Phill(sikupendi lakini) ni bora kuliko maximo! Hivi kweli huyu jamaa (maximo) alikuwa kwenye technical bench ya timu ya vijana huko kwao au ilikuwa ni timu ya vijana wa kike? Hapa alipo anatamani kishenzi kumuita Ivo, lakini anaogopa atalaaniwa kila mahali.Dah, nina mihasira na si ajabu nishatoka nje ya mada lakini NO EDITING especially znz piga hao wabara waje kula miharage huku!CECAFA imetuonyesha MAXIMO ni nani, WaTZ mnasemaje? Hii sio aibu ya nchi? Uzalendo na nidhamu anavyotoa kama vigezo vya kuwakataa wachezaji hawa mbona yeye vimemshinda? Ni jana tu amelimwa barua ya utovu wa nidhamu na CECAFA. Kocha gani huyu mhuni. Mie binafsi nimemuona kwenye TV baada ya mechi na RWANDA akimshambulia wazi wazi kwa matusi kocha wa Rwanda. Je, kocha wa Rwanda alikuwa anacheza au alikuwa Refa. Mpira umeisha matokeo yamipatikana kutokana na maelekezo yake au aina ya uchezaji alitaka. Sio hapo tu TZ ni timu iliyoonyesha nidhamu ya hali ya chini sana. Kufunga kumechangiwa na kuwa na wachezaji pungufu kutokana na wachezaji kutojua kuwa makosa au rafu zisizo na maana uwanjani zinaigharimi timu. Haya kila mechi TZ walikuwa wakimaliza mpira wakiwa pungufu. Jamani mnakubali kuwa refs walikuwa wanatuonea kama sio reflection ya quality ya COACH. PIMA NA TOA UAMUZI.
punguza hasira...na mchukie maximo siyo Taifa/Kilimanjaro star ila siyo siri weekend itakuwa imeenda vizuri kama Tanzania visiwani watashinda gemu la kesho..maana alisha waambia soka hawaliwezi leo hii wote wanatafuta mshindi watatu pamoja na kwamba yeye anapewa kila kitu..znz piga hao wabara waje kula miharage huku!