The Rise and Fall of Marcio Maximo...Discuss.


Mkuu, with all resorces and support given to him, he is waste.
 
Kazi ya mwalimu ni kumfundisha mwanafunzi mpk aelewe na akae ktk mstari husika.
Mwalimu wenu huyu aliyekuwa anachoma chapati Brazil ni tofauti na walimu wa soka tuliowaona hapa duniani.
Mwalimu wenu huyu yeye amekuwa mtu wa kwanza kuwakataa wanafunzi wake ambao wamekuwa na upungufu wa nidhamu.
Mwalimu wa kweli asingediriki kuwatosa kina Juma, Othman na Haruna.
Bali mwalimu wa kweli angewaita na kuwafundisha mpk wakanyooka.
sasa yeye anakwenda kula kiapo kuwa hatokuwa radhi kuwaita wachezaji hawa eti kisa utovu wa nidhamu,, sasa na yeye alichokipata mechi na kwenye kombe la chalenge kilikuwa ni kitendo cha nidhamu?

Mi naona kama ni nidhamu basi yeye ni 'Gagulo na hao anao wakataa ni Sidiria'...zote nguo za ndani
 
Usimsahau na 'Kapu' vilivile yumo katika hao wababaishaji wa soka.
Hint:KAPU=TENGA
 
Mwanzoni wakati mheshimiwa anaukwaa urais aliwaahidi wa tz kuwa atawaletea kocha wa kimatiafa na mwenye utaalam mkubwa wa soka. Na kweli muda si mrefu Maximo aliwasili. Siku za mwanzoni wakati Maximo alipokuwa anawapa mazoezi wachezaji wa taifa stars katika uwanja wa taifa na mheshimiwa naye alikwenda kushuhudia mazoezi. wakati mheshimiwa anaondoka uwanjani aliongea na vyombo vya habari, Aliongea nini? namnukuu ambapo nilimsikia live katika itv nadhani hata humu jamvini kuna watu wanaweza kukumbuka kauli yake, alisema:" kocha amenifurahisha sana, huyu kocha yuko uwanjani anafundisha huku anatumia laptop! hii ni tofauti kabisa na makocha wetu wa hapa, huyu kocha yuko makini na kazi kwa sababu anatumia laptop" kwa upande wangu hii kauli ilinipa wasiwasi sana kuona mkuu wa nchi anastaajabu juu ya laptop, hapo ndipo nikasema ama kweli watz wameingia mkenge kumchagua kwa kufata upepo!
 
Tunamuomba Maximo aondoke atuachie timu yetu mpunga alioula umeshamtosha..........arudi kwao akafanye mambo mengine....mpira wa TZ umeshamshinda kama anapenda kuishi TZ atafute kazi Kaole .......ila si kocha wa Taifa stars
 
Very interesting hii story ina ukweli?
 
aisee hapo gambler umenena, hiyo kitu hata mimi nakumbuka alisema, ni ulimbukeni kwa president kushangaa na laptop
 

he he he, nafikiri tunaweza kuichukua hii ikatufungia mwaka ktk jukwaa letu la michezo.... -"kheri mimi sijasema"!!
 
aisee hapo gambler umenena, hiyo kitu hata mimi nakumbuka alisema, ni ulimbukeni kwa president kushangaa na laptop

Mkuu unaamini Rais ni limbukeni? unaja siasa?
 
as long as boss wake bado yupo basi hatoki ng'o...
 
maximo.....hana jipya! anapenda kukaa tz...tu...sasa tukubali aendelee kuishi nchini ila timu ya taifa hasipewe tena...kama kikweta anamtaka basi tukifungwa tena tutakuomba kikwete ujiuzuru urais maana unatuwekea uozo ambao watanzania wote wamechoka nao...nchi ni watu kikwete hakuna maendeleo bila kusikiliza wananchi wanataka nini!!!! muondoe maximo haraka sana kabla mwaka 2009 ujaisha.
 
Imenisikitisha sikuwahi kuisikia kweli jamani. Ila sasa watanzania muwe na subira atatolewa tu wala haina objection but not like that. kumfukuza mtu kama mbwa.
 
Very interesting hii story ina ukweli?
Ni kweli hata mimi nilimsikia JK...Maximo alikuwa akitaja majina ya wachezaji aliokuwa amewachagua akawa anasoma kutoka kwenye laptop badala ya mikaratasi kama wengi wanavyo fanya basi kitendo kile kilimfanya JK amwamini kuwa Maximo ni mbongo la kocha kumbe ni mbonge la msani kama yeye..
 
Bora tenga alivoamua
sasa tusubiri huyo kocha mpya..
Sijui watamtoa wapi...
Wangekuwa na akili
wangetafuta kocha kutoka uholanzi
 
Huyo atakaekuja nae sijui ataletewa fitna..maana bongo da!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…