The Ventures Africa: Mohammed Dewji ni mmoja wa mabilionea 55 wa Afrika.

The Ventures Africa: Mohammed Dewji ni mmoja wa mabilionea 55 wa Afrika.

Ng'wamapalala

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2011
Posts
6,811
Reaction score
6,503
Gazeti la Pan-African linalipoti kuwa kwa sasa Afrika ina mabilionea wengi zaidi ya jinsi ilivyokuwa imeripotia. Kiasi cha 55 kati ya hao wana utajiri unaokisiwa kuwa zaidi ya dola bilioni 143 ambapo ndani yake kuna mwanamke Mnaijeria anayekisiwa kuwa tajiri zaidi ya mwanamke yeyote duniani.

Katika makala yake mpya iliyotoka week hii yenye kichwa cha habari kisemacho, "Move over, Oprah!" Mhariri Mkuu wa Ventures Afrika, Uzodinma Iweala amedai kiasi hiki cha pesa ni kisio la kiwango cha chini.

Kama ilivyotegemewa, repoti imebainisha kuwa Adiko Dangote ni tajiri anayeongoza barani Afrika akiwa na utajiri wa thamani ya dola bilioni 20.2. Kati ya mabilionea 55 walioorodheshwa, Wanaijeria wako 20.

Afrika Ventures limebainisha kiwango cha wastani wa utajiri wa mabilionea ni dola bilioni 2.2, huku wakiwa na wastani wa umri wa miaka 65.

Tajiri wa viwanda nchini Kenya, Manu Chandaria na pia raia wa Misri, Mohammed Al Fayed ambao wote wana umri wa miaka 84 ni mabilionea wenye umri mkubwa zaidi katika repoti hiyo.

Vijana mabilionea wenye umri mdogo kuliko Afrika ni Mtanzania anayeitwa Mohammed Dewji na Mnaijeria mfanya biashara ya mafuta anayeitwa Igho Sanomi ambao umri wao kila mmoja ni miaka 38.

Nigeria, South Africa na Misri zinaongoza katika Afrika kuwa na idadi ya matajiri wakubwa, ambapo tisa wanatoka South Africa, wanane wanatoka Misri na huku nchi za Angola, Algeria, Zimbabwe na Swaziland zikiwa na bilionea mmoja kwa kila nchi.

Repoti imebainisha kuwepo kwa mabilionea katika nchi 10 kati ya nchi 53 barani Afrika.

Repoti imeshangaza wengi kwa kumbainisha tajiri wa biashara ya mafuta, Folorunsho Alakija kuwa ndiye tajiri mwanamke anayeongoza duniani kwa kuwa na utajiri wa thamani ya dola bilioni 7.3 wakati Forbes Magazine lilikadiria Alakija's kuwa na utajiri wa dola milioni 600 huku Oprah Winfrey akiwa na dola bilioni 2.9.

Katika idadi ya matajiri 40 wa Afrika walioorodheshwa na The Forbes, kati yao ni matajiri 16 ambao wana utajiri unaofikia dola bilioni.

Iweala ameonyesha fulaha yake baada ya kugundua kuna Waafrika waliotajirika kwa njia ya uzalishaji viwandani na huduma za kifedha kitu ambacho kinaonyesha bara la Afrika linapiga hatua isiyotegemea uchumi wa mali ghafi.


Wasifu wa Folorunsho Alakija.

attachment.php

Married to Modupe Alakija who is the chairman of Famfa Oil and Gas Limited and blessed with four sons and a grandchild, Folorunso Alakija also owns a Christian-based charity called Rose of Sharon foundation, which gives out small grants to widows.

Africa's richest woman sits atop Famfa Oil, a Nigerian oil company that owns a 60-percent stake in OML 127, one of Nigeria's most prolific oil blocks located at Nigerian offshore Agbami deepwater field. Daily production at OML 127 stands at over 200,000 barrels per day. Alakija studied fashion design in England in the eighties, returning to Nigeria to found Supreme Stitches, a Nigerian fashion label which enjoyed patronage from the more successful women in Nigerian high society. One of her clients was Maryam Babangida, the wife to former Nigerian military President, Ibrahim Babangida. Alakija is believed to have ridden on the crest of this relationship to acquire an oil block in 1993 at a relatively inexpensive price. Famfa immediately entered into a joint venture agreement with Star Deep Water Petroleum (a subsidiary of Chevron and Brazil's Petrobas), ceding a 40-percent stake to the two companies. Famfa owned a 60-percent interest in the block until 2000, when the incumbent Nigerian president, Olusegun Obasanjo, forcefully acquired a 50-percent stake in the block, transferring it to the Nigerian National Petroleum Corporation – a government-owned oil company. Famfa Oil immediately went to court to challenge the acquisition in a case that dragged on for 12 years. In May 2013, the Nigerian Supreme court reinstated the 50-percent stake to Famfa Oil. Alakija also owns $200-million of real estate in the United Kingdom.


Africa now home to 55 billionaires, magazine reports | The Japan Times


NOTE:
Habari hii imeandikwa kwa lugha ya Malkia wa Uingereza na nimejaribu kuiweka kwenye lugha iliyoletwa Bariadi na watembezi kutoka Pwani ya Bahari ya Hindi.

Kiswahili na kiingereza siyo Lugha ya Baba wala Mama yangu!.

Kwa hisani Japanesetimes.
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    139.2 KB · Views: 865
Tanzania kweli hatuna mabilionea wengi?.

Biashara zetu za chini ya meza zinasababisha hata kutokuwa detected siyo na watafiti kama The Ventures Africa peke yake, bali hata na vyombo vya usimamizi wa fedha kisheria.

Congrats and Good luck to Dewji lakini pia utajiri wake lazima uwe kioo kwenye jimbo lake la uchaguzi akiwa ni mwakilishi, mtunga sheria na msimamizi wa majukumu ya serikali.
 
Tanzania kweli hatuna mabilionea wengi?.

Biashara zetu za chini ya meza zinasababisha hata kutokuwa detected siyo na watafiti kama The Ventures Africa peke yake, bali hata na vyombo vya usimamizi wa fedha kisheria.

Congrats and Good luck to Dewji lakini pia utajiri wake lazima uwe kioo kwenye jimbo lake la uchaguzi akiwa ni mwakilishi, mtunga sheria na msimamizi wa majukumu ya serikali.

Mbona tunao wengi tu hapa Tanzania sema vyanzo vya mapato yao ndio tatizo.Wengi ni wauza sembe na wengine ni mafisadi kwahiyo wanagwaya kuanika utajiri wanaomiliki hadharani.
 
Mbona tunao wengi tu hapa Tanzania sema vyanzo vya mapato yao ndio tatizo.Wengi ni wauza sembe na wengine ni mafisadi kwahiyo wanagwaya kuanika utajiri wanaomiliki hadharani.
Mkuu TECH WIZ mbona na wewe unaongea kwa kujificha kama wanavyofanya biashara za chini ya meza "mabilionea" wetu wa Kitanzania.

Tutendee haki wanaJF kwa kuwataja na pia kama kuna uwezekano wa kuzifahamu estimate fortune zao.
 
Last edited by a moderator:
Tanzania haina mabilionea sababu sera za serikaili ya Tanzania ni kuwakandamiza watu wanaotaka kutajirika,mabilionea wanatengenezwa na sera za nchi,mfano mdogo ni nchi kama ya Vietnam,nchi ya Vietnam ilikuwa maskini lakini serikali ilitengeneza matajiri ili waisaidie nchi,tukumbuke tu sera ya serikali ya Tanzania ni ujamaa na kujitehemea siasa ambyo inapingana na ubebari
 
Mbona mi jina langu cjaliona?
Mkuu Ibada ya kwanza utalionaje jina lako kwenye The Ventures Africa wakati hata unalotumia JF ni fictitious.

Mimi na wewe tunaopambana kihoja hapa JF kwa kutumia false name hatuko tofauti na wale Watanzania wanaofanya biashara kwa kificho. Tofauti ni impact and magnitude.
 
Last edited by a moderator:
Tanzania haina mabilionea sababu sera za serikaili ya Tanzania ni kuwakandamiza watu wanaotaka kutajirika, mabilionea wanatengenezwa na sera za nchi,mfano mdogo ni nchi kama ya Vietnam,nchi ya Vietnam ilikuwa maskini lakini serikali ilitengeneza matajiri ili waisaidie nchi,tukumbuke tu sera ya serikali ya Tanzania ni ujamaa na kujitehemea siasa ambyo inapingana na ubebari
Maelezo yako yana ukweli ndani yake pamoja na kwamba siyo ukweli halisia hasa ikichukuliwa kuwa tayari kuna Mtanzania kijana wa miaka 38 ambaye ni bilionea katika thamani ya pesa za Marekani.

CCM wanatuambia Ujamaa na Kujitegemea ambao ni sera zake na nguzo na msingi kikatiba ni wa 'kisasa' ambao unaendana na 'wakati' kwa maana kwamba ni Ujamaa na Kujitegemea unaoendana na soko huria. (Usiniulize maswali zaidi).

Katika huo Ujamaa na Kujitegemea, ndiyo amepatikana kwenye vitabu bilionea Mohammed Dewji na ninatumaini wapo wengine ambao utajiri wao hauko kwenye 'vitabu'.
 
Wacha weee ! Hongereni sana wananchi mliomchagua , njaa ikiwajia mtagawana vya kwake !
 
Itamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote na yeye mwenyewe akiukosa uzima wa milele?
 
Maelezo yako yana ukweli ndani yake pamoja na kwamba siyo ukweli halisia hasa ikichukuliwa kuwa tayari kuna Mtanzania kijana wa miaka 38 ambaye ni bilionea katika thamani ya pesa za Marekani.

CCM wanatuambia Ujamaa na Kujitegemea ambao ni sera zake na nguzo na msingi kikatiba ni wa 'kisasa' ambao unaendana na 'wakati' kwa maana kwamba ni Ujamaa na Kujitegemea unaoendana na soko huria. (Usiniulize maswali zaidi).

Katika huo Ujamaa na Kujitegemea, ndiyo amepatikana kwenye vitabu bilionea Mohammed Dewji na ninatumaini wapo wengine ambao utajiri wao hauko kwenye 'vitabu'.

Inawezekana maneno yako ni kweli mkuu,huyo kijana bilionea mwenye miaka 38 itakuwa huo utajiri wake ameupata kwa njia ya panya,siasa ya ujamaa wanaotakiwa kung´ara ni wanasiasa tu,katika siasa ya ujamaa na kujitegemea wanasiasa ndio wanaotakiwa wawe matajiri,waogopewe,waheshimiwe nk,na ndio maana utakuta mawaziri na watendaji kazi katika serikali wananguvu kuliko raia wa kawaida........
 
Back
Top Bottom