The Wacko Jacko

The Wacko Jacko

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
062609mjred.jpg




Ndivyo alivyoitwa, kwa wake umaarufu
Kwa yale aliyopatwa, nyoyo zimepatwa ufu
Maini yetu yakatwa, kwa uchungu maradufu
Mola nae akulaze, pale unapostahili

Ni mengi uliyafanya, kupitia yako fani
Watu tukajawa chanya, leo twakukosa masikini
Wa rika zote wakumanya, kila kona duniani
Mola nae akulaze, pale unapostahili

Petu nchini ulifika, nyumbani kwako Afrika
Nasi tukahamasika, kwa namna ulivyotushika
Tulikupenda hakika, upendo usio mipaka
Mola nae akulaze, pale unapostahili

Kwa kweli yashangaza, utendaji wake mola
Weza dhani atukwaza, tuache tafuta hela
Hakika yote miujiza, jua Mola hana hila
Mola nae akulaze, pale unapostahilia

Wachache hawakukupenda, ninawaona wakicheka
Ni wale uliowapenda, haiba yao ukaitaka
Ila bado twakupenda, una damu ya Afrika
Mola nae akulaze, pale unapostahili

Dunia nzima yakutaja, kwa yote mema, mabaya
Na jina lako liwe tija, kwa yako ndogo kaya
Tuombe pasiwe mirija, ili wanao wasijepwaya
Mola nae akulaze, pale unapostahili

Hakika sitamalizia, nyoyo zauma dunia
Sauti nyingi zalia, macho yamevilia
Kifo sote twapitia, hakuna mbadala njia
Mola nae akulaze, pale unapostahili

Courtesy of mziwanda
 
Last edited:
Back
Top Bottom