Shayu
Platinum Member
- May 24, 2011
- 608
- 1,655
Siasa za uongo na ulaghai zimeichukua taifa letu, lakini bado tunafikiri kwamba tumesimama katika sehemu imara, na ya kwamba miguu yetu kwamwe haitoteleza. Tunajidanganya. Hatuwezi kujenga taifa katika uongo na ulaghai tukadhani misingi yake itakuwa imara. Taifa likitupa ukweli na kukumbatia uongo linajifanya lenyewe kuwa pumbavu, katika taifa la namna hiyo kunakuwa hamna maono ujinga huwafunga na wasione mbele na maendeleo kwa taifa la namna hii ni vigumu kuyafikia. Lakini kuna mwangaza kwa taifa linalokumbatia ukweli na ambalo halifanyi jitihada kuupotosha. I am telling you there is great future for that country.