THRDC waunga mkono na kuifafanua kwa ufasaha movement ya Watanzania ya NO REFORMS, NO ELECTION inayoongozwa na CHADEMA

THRDC waunga mkono na kuifafanua kwa ufasaha movement ya Watanzania ya NO REFORMS, NO ELECTION inayoongozwa na CHADEMA

The Palm Beach

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2015
Posts
1,967
Reaction score
4,267

View: https://youtu.be/cQ8my9Fu7jU?si=8G2_TzDMHKYELqgD

➡Huyu hapa ni Mkurugenzi Mtendaji wa asasi ya kiraia ya kulinda na kutetea haki za binadamu - Tanzania Human Rights Defenders Coalition (THRDC) Bwana Onesmo Olengurumwa akifafanua dhana dhima ya kauli mbiu ya kudai mabadiliko ya kikanuni, kisheria na kikatiba yanayochagizwa na kauli mbiu ya NO REFORMS, NO ELECTION ili kuwezesha kufanyika kwa chaguzi huru, za wazi na za haki hapa Tanzania...

➡Amesema, NO REFORMS, NO ELECTION haina maana ya kuwa kusiwepo na uchaguzi. Bali chaguzi zozote zijazo ukiwemo wa mwaka huu 2025, ni lazima ufanyike baada ya mabadiliko (reforms) muhimu ya kisheria, kikanuni na kikatiba kufanyika ili kuwezesha chaguzi huru na za kweli kufanyika ili kila mpiga kura aanze kuona thamani ya kura yake kwa kuhesabiwa na ikahesabika....

➡Anasema, kama hakutakuwa na mabadiliko hayo muhimu ambayo ktk maelezo yake ameyafafanua kwa kina, basi kwa kweli hakuna haja wala sababu ya kufanya chaguzi (maigizo ya uchaguzi) kama yale ya mwaka 2019, 2020 na 2024..
 

View: https://youtu.be/cQ8my9Fu7jU?si=8G2_TzDMHKYELqgD

➡Huyu hapa ni Mkurugenzi Mtendaji wa asasi ya kiraia ya kulinda na kutetea haki za binadamu - Tanzania Human Rights Defenders Coalition (THRDC) Bwana Onesmo Olengurumwa akifafanua dhana dhima ya kauli mbiu ya kudai mabadiliko ya kikanuni, kisheria na kikatiba yanayochagizwa na kauli mbiu ya NO REFORMS, NO ELECTION ili kuwezesha kufanyika kwa chaguzi huru, za wazi na za haki hapa Tanzania...

➡Amesema, NO REFORMS, NO ELECTION haina maana ya kuwa kusiwepo na uchaguzi. Bali chaguzi zozote zijazo ukiwemo wa mwaka huu 2025, ni lazima ufanyike baada ya mabadiliko (reforms) muhimu ya kisheria, kikanuni na kikatiba kufanyika ili kuwezesha chaguzi huru na za kweli kufanyika ili kila mpiga kura aanze kuona thamani ya kura yake kwa kuhesabiwa na ikahesabika....

➡Anasema, kama hakutakuwa na mabadiliko hayo muhimu ambayo ktk maelezo yake ameyafafanua kwa kina, basi kwa kweli hakuna haja wala sababu ya kufanya chaguzi (maigizo ya uchaguzi) kama yale ya mwaka 2019, 2020 na 2024..

Huyu Ole Ngurumwa, Fr Kitima, Askofu Dk. Shoo, Askofu Dk. Bagonza, Sheikh Mruma na viongozi wengi wa dini na wanaharakati wa haki za binadamu kwa macho yangu; niliwaona wakishiriki nwanzo mwisho mabadiliko ya Sheria mbalimbali za uchaguzi ikiwemo ya Wagombea Urais na iliyounda Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ( INEC).

Sasa huwa siwaelewi Reforms zipi? Walianzia bungeni miswada iliposomwa kwa mara ya kwanza Novemba, 2023.

Kichwa kinaumwa kuna mtu ana Aspro? (Kwa sauti ya Baba wa Taifa na mwanahalisi wa taifa hili Julius Nyerere).
 
Ngurumwa anauma na kupuliza! Chadema inasema nyooka kama rula kuwa bila mabadiliko mwaka huu hakuna uchaguzi bali uchafuzi mwingine!
 
Back
Top Bottom