THRDC yakemea Mwandishi wa Habari kukamatwa kwa kupiga picha Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwembe wakisoma chini ya mti

THRDC yakemea Mwandishi wa Habari kukamatwa kwa kupiga picha Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwembe wakisoma chini ya mti

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Baada ya andiko la Mwandishi wa Habari wa The Guardian kudaiwa kushambuliwa na Walimu, THRDC imetoa tamko, kusoma ilivyokuwa bofya hapa ~ Mwandishi wa Habari wa The Guardian anadai amepigwa na Walimu baada ya kupiga picha Wanafunzi wakisoma chini ya miti.

TAARIFA YA KUKAMATWA KWA MWANDISHI DICKSON NG’HILY
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) unakemea kitendo cha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kumkamata Mwandishi wa habari ambaye pia ni mhariri wa Biashara na Mkuu wa Kitengo cha Mtandaoni (Digital) kutoka Gazeti la the Guardian pamoja na walimu kadhaa ambao idadi yao bado haijafahamika kutokana na mwandishi huyo kuwapiga picha Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwembe waliokuwa wanasoma chini ya miti.

Katika ujumbe wake aloutuma kwa njia ya WhatsApp, mwandishi huyo amedai kuwa amepigwa sana na kuumizwa kwenye mkono na simu yake imevunjika kioo.

Taarifa za awali zinaonyesha kuwa mwandishi huyo alipelekwa ofisi za Serikali ya Mtaa na kwasasa anashikiliwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) unafuatilia kwa ukaribu sana suala hili Lakini pia THRDC inaamini kwamba Mwandishi wa habari ana haki ya kutafuta na kusambaza habari kwa umma kwa mujibu wa ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kupiga picha ni jambo la kawaida.
Wito wetu.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) unatoa wito kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kumuachia mandishi huyo mara moja kwani Mkuu wa Wilaya hana Mamlaka Kisheria ya Kumkamata mwandishi huyo kwa vyovyote vile.

Imetolewa na,
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),
Julai 10, 2024 Dar es Salaam, Tanzania.


Majibu ya Serikali ~ Madai ya Wanafunzi kusomea chini ya mti Shule ya Msingi Kwembe (Dar), Serikali yasema walikuwa katika programu maalumu
 
Hizo shule ziko nyingi na serikali ya CCM inafanya maksudi sio kwamba hawaoni bali lengo ni kuendelea kutengeneza rundo la wajinga ili kuendelea kubaki madarakani maana wanajua wakiboresha elimu watu wataelimika na wajinga watapungua hivyo kupelekea amsha amsha kama za Gen Z kule Kenya.
 
Hao THRDC wameona watoe tamko la nini hapo? Kuficha umasikini au ile dhana ya mama anaupiga mwingi
Wewe umeelewa chochote kwenye hii post kweli? THRDC ndio wanaopinga muandishi kupigwa kwa sababu ya kupiga picha hao wanafunzi
 
IMG_3035.jpeg

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) unakemea kitendo cha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kumkamata Mwandishi wa habari ambaye pia ni mhariri wa Biashara na Mkuu wa Kitengo cha Mtandaoni (Digital) kutoka Gazeti la the Guardian pamoja na walimu kadhaa ambao idadi yao bado haijafahamika kutokana na mwandishi huyo kuwapiga picha wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwembe wanaliokuwa wanasoma chini ya miti.

Katika ujumbe wake aloutuma kwa njia ya WhatsApp, mwandishi huyo amedai kuwa amepigwa sana na kuumizwa kwenye mkono na simu yake imevunjika kioo.

Taarifa za awali zinaonyesha kuwa mwandishi huyo alipelekwa ofisi za Serikali ya Mtaa na kwasasa anashikiliwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umesema unafuatilia kwa ukaribu suala hili Lakini pia THRDC inaamini kwamba Mwandishi wa habari ana haki ya kutafuta na kusambaza habari kwa umma kwa mujibu wa ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kupiga picha ni jambo la kawaida.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umetoa wito kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kumuachia mandishi huyo mara moja kwani Mkuu wa Wilaya hana Mamlaka Kisheria ya Kumkamata mwandishi huyo kwa vyovyote vile.
 
Khaaa hiyu ana kiburi cha kaka wa imani anaganya atakalo anajua wataonana nsikitini haguswiii awamu hii .....kaka wa imani ???
 
Hao THRDC kazi Yao Huwa ni kukemea tu.kwa Nini wasichukue hatua ya kufungua kesi dhidi ya aliyevunja Sheria?
 
View attachment 3038979
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) unakemea kitendo cha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kumkamata Mwandishi wa habari ambaye pia ni mhariri wa Biashara na Mkuu wa Kitengo cha Mtandaoni (Digital) kutoka Gazeti la the Guardian pamoja na walimu kadhaa ambao idadi yao bado haijafahamika kutokana na mwandishi huyo kuwapiga picha wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwembe wanaliokuwa wanasoma chini ya miti.

Katika ujumbe wake aloutuma kwa njia ya WhatsApp, mwandishi huyo amedai kuwa amepigwa sana na kuumizwa kwenye mkono na simu yake imevunjika kioo.

Taarifa za awali zinaonyesha kuwa mwandishi huyo alipelekwa ofisi za Serikali ya Mtaa na kwasasa anashikiliwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umesema unafuatilia kwa ukaribu suala hili Lakini pia THRDC inaamini kwamba Mwandishi wa habari ana haki ya kutafuta na kusambaza habari kwa umma kwa mujibu wa ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kupiga picha ni jambo la kawaida.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umetoa wito kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kumuachia mandishi huyo mara moja kwani Mkuu wa Wilaya hana Mamlaka Kisheria ya Kumkamata mwandishi huyo kwa vyovyote vile.
Mpelekeni mahakamani mshenzi huyo DC. Unlawful confinement
Protecting the Individual against the State through False Imprisonment Actions:"Wrongful confinement", which is very similar to the tort of false imprisonment in re elements, is an offence under s. 253 of the Penal Code (Cap. 16).
 
Back
Top Bottom