Thread ya list ya wana JF wanaohama Tigo

Tigo sio wezi tu bali wanadrop calls pia ukipigiwa mara hupatikani, ukimpigia mtu ukiongea mara wanawakatia simu.....aaaaargh!
 
Tigo ni wezi wa kutupa. Hata promotion zao ni bogas kishenzi. Wakati wakipromote offer ya 100 sms kwa tsh 345 kama sijakosea, ukituma sms 100 zinakwena 18 tu. Zilizobaki zinakula pesa yako hadi ziishe! Nilijaribu for several times kumbe ni tabia zao za kudumu. Washenzi sana mimi nimeachana nao long time. Nawashauri JF wote tuhame ili wafe kifo cha mende.
 
Mimi nimeachana nao mwaka sasa....nilikuwa mteja wao wa postpaid...laki1 hadi 2 kwa mwezi nilikuwa nalipia,,,,,,,,
Toka nimeingia ZANTEL...sijajutia uwamuzi wangu......TiGo ni kinyesi kabisa period.
 
Mie natafuta ule mtandao wa WAPEMBA, hawaibi wale
kweli mkuu, me nawafaidi sana hawa WAPEMBA.. Njoo tupate huduma za simu zilizonakshiwa na marashi ya karafuu.!
 
mimi pia nahama.sijajua coverage ya huu mtandao wa wapemba,kule kwenye miteremko ya mlima kilimanjaro tarakea unapatikana?

Mkuu Zantel iko covered sehemu kubwa sana, me hua nasafiri sana Dar-Mwanza Zantel ndio mtandao ninaoutegemea.. Walichofanya hawa wapemba wameingia ubia wa kutumia minara ya voda, so popote penye voda WAPEMBA wapo, so hata huko tarakea itakuwepo tu! Karibu ktk ufalme wa marashi ya Karafuu..!
 
Haka kahuduma cha voice msg wamekaanzisha kinyemela kwa namna hata kama mtu hataki kuacha ujumbe wa sauti pesa itakatwa tu na mpigiwaji atapokea msg ya ujumbe hewa wa sauti. Kampuni ya TIGO ina njaa mpaka inachajisha wateja wakiwa wanapiga simu customer care kuomba misaada ya shida mbalimbali za kimtandao.
Kuanzia hivi sasa najitoa Tigo na line hii nitaitumia kama phone book.
Nachagua mtandao mwingone, TIGO mmezidi.
 

Mkuu nami naulaani kwa nguvu zote huu utaratibu wa kinyonyaji wa Tigo wa kulazimisha Voice mail au sijui ndo inayoitwa ujumbe wa sauti hewa. nabilashaka wanawakata wote - anayepiga na anepokea. Wizi huu waukomeshe mara moja. hatutaki hiyo voice mail - iwe ya hiyari mtu kujiunga au la
 
mi nilituma sms kwa jamaa yangu jana saa mbili usiku ime deliver leo saa nne asubuhi....sijui waliituma kwa basi
 
zantel wapo poa sana halafu ukiwapigia hausubiri hata dakika tatu unakuwa ushaunganishwa. hamieni ZANTEL.
Tukija wote huko zantel na wenyewe si watakusubirisha? labda uzungumzie ghalama ya kupiga
 
hata voda nao wamepandisha bei hadi sh 2.6/sec tena bila kuwaarifu wateja.
mimi kwa sasa natumia laini mpya ya ZANTEL raha sana kutumia huu mtandao. wanaJF twanga kotekote.

Huenda kuna ukweli fulani, lakini je wakiwa na wateja wengi hawa zantel hawataleta mbwembwe?
 
Thread nyingine bwana, utadhani kuna watu wametumwa na ZANTEL kufanya promo hapa.
Mitandao yote wako kwa faida hapa, musitarajie dezo
 
Sijui mtandao gani una nafuu kwa sababu wote wamepandisha kwa zaidi ya 50% ya gharama ya zamani, lakini mimi naona Airtel ni juu zaidi ya wote. TIGO mimi nafaidika sana na ofa zao hivyo sihami kwa sasa, labda baadae kama ofa zitaisha.
 
Huu ni wizi wa mchana na njia ya mkato ya kuwashughulikia ni kuhamia mitandao inayotoa ghalama ndogo.
 
mimi nililalamika sana nikifikjiri ni tigo peke yao, lakini nimekuja kugundua kumbe ni mitandao yote imepandisha gharama, sasa sioni haja ya kuhama tigo, kama kawa tunabaki hukohuko maana huko kwa kwenda hakuna unafuu wowote heri tusijeruka mkojo tukakanyaga vinyesi hivyo vya wengine
twabaki tigo sie
 
Call Quality ya TIGO ni uchafu mtupu.TTCL mobile ndio simu ya uhakika tatizo ni customer care tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…