Throwback Thursday: Juma Nature, mkali wa hizi kazi

Throwback Thursday: Juma Nature, mkali wa hizi kazi

matumbo

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2011
Posts
7,224
Reaction score
3,951
Wakati watu leo wako bize kuthrowback ishu mbali mbali ghafla nimemkumbuka mkali wa hizi kazi,Kibra Msitu wa vina a.k.a Juma Nature.

Nakumbuka mara ya kwanza namuona anachana kipindi hiko mie bwana mdogo ,anashika kipaza anapanda jukwaani na washikaji zake wawili mmoja Dolo mwingine simkumbuki mpaka kesho.

Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza naona msanii anabeba kijiji kinadata ...anapiga mistari ya kiswahilini hatari alafu watu wanamuelewa ,anakwambia wimbi la njaa matatizo umaskini chanzo cha nguo kupwaya kufunga na pini,,,watu heeeeeeee .

Baada ya hapo nashuhudia maajabu juu ya maajabu mara kachukuliwa na majani,mara katoa singo yake hili game ikaja jinsi kijana mpaka album nzima..Album haufowadi ata nyimbo moja..Huku sonia kule kigetogeto album ilipofika kanda ya ziwa ikaisha ndani ya week.

Akaja na album ya Ugali ikavunja rekodi ya mauzo bongo akaijaza Diamond Jubilee mpaka watu wakazuiwa kuingia.

Msanii wa kwanza wa bongofleva kumiliki Benz kwa mauzo ya muziki.Kawatoa wasanii kibao,kuna kipindi Tmk yote aliibeba yeye.

Kaimba karibu na kila msanii mkali bongo.Kama haitoshi akatumiwa na Ruge Mutahaba ,Sebastian Maganga na Joseph Kusaga kuokoa jahazi la Fiesta lililozama baada ya Lil Kim kuchemsha.

Kajenga nyumba mbili kwao uswazi na anaishi huko mpaka kesho.Bongofleva wa kwanza kuuza magazeti ya Shigongo kwa drama zake na mbongo muvi Sinta.

Hapo sijazungumzia maajabu yake, maana server ya JF haitatosha...Huyu ndio Nature, Bob Marley wa bongo fleva.

Nimejikuta namkumbuka kidogo leo.
 
Sema kweli kibra sijawahi kumwona live,ila miaka ya 2001 nikiwa la saba nilimkubali sana,halafu bhana ni mtu anayejali kila tabaka,huyu jamaa hana makuu,ngoma kama ya leo ni noma.

sasa angalia alivyo live hapa halafu kuna jamaa kaja kuzingua watu wamemind ila yeye kaja kuongea kishkaji kawatuliza.

hao mabaga fresh ndo wameniacha hoi kwa huo msamiati wao wa kumwomba dj alete biti jamaa akasema ''dj lete nyege''
http://www.youtube.com/watch?v=oVBJgSD0Cew
 
Uko sahihi kumkumbuka hvyo. I grew up with Nature kiburudani.
Kama vp lianzishwe THROWBACK BONGO FLAVOR ARTIST CHAMPIONSHIP.

Kama vp hata hapa Celeb tupige POLL. Gadmnt.
 
Album yake ya UGALI inatoka nilikuwa advance.., kuna ngoma kali mle, ila ilonikamata enzi hzo ni "kisa dem" , huh P funk alinyonga biti mule.

Nakwambia asikwambie mtu, nilikua primary na nilikua namudu kuimba mashairi ya nyimbo nyingi za Nature...
Sasa nikianza kuimba sitaki demu nilikua mpaka nakaa chini kwa hisia kama kidume vile...
 
Mtoto Idi,
Yaleo kali,
Tunafanya kazi alishirikishwa na mkenya,
Nakumbuka Tosamaganga kuna jamaa mwaka 2003 ,alikuwa amepewa jina la Nature aliimba kama yeye
 
Nakwambia asikwambie mtu, nilikua primary na nilikua namudu kuimba mashairi ya nyimbo nyingi za Nature...
Sasa nikianza kuimba sitaki demu nilikua mpaka nakaa chini kwa hisia kama kidume vile...

Tunafanyaje sasa kumrejesha huyu msela... Ngoma yake ya 'sonia' inatoka nilikuwa 5. Hakuna mobitel at that moment 2003...ndo bongo flavaour inachanua
 
Nakwambia asikwambie mtu, nilikua primary na nilikua namudu kuimba mashairi ya nyimbo nyingi za Nature...
Sasa nikianza kuimba sitaki demu nilikua mpaka nakaa chini kwa hisia kama kidume vile...
nye ndo wale masista du mlichaguliwa mje wilayani halafu mnakuja na swaga mnakimbiza wilayani mpaka vinyozi
 
Sema kweli kibra sijawahi kumwona live,ila miaka ya 2001 nikiwa la saba nilimkubali sana,halafu bhana ni mtu anayejali kila tabaka,huyu jamaa hana makuu,ngoma kama ya leo ni noma.

sasa angalia alivyo live hapa halafu kuna jamaa kaja kuzingua watu wamemind ila yeye kaja kuongea kishkaji kawatuliza.

hao mabaga fresh ndo wameniacha hoi kwa huo msamiati wao wa kumwomba dj alete biti jamaa akasema ''dj lete nyege''
http://www.youtube.com/watch?v=oVBJgSD0Cew

Nature alianza kuwa star town kabla ata hajatoa wimbo wake mwenyewe.. Kipindi hicho anapewa collabo tu na machizi kina Bwana mkubwa manduli kina Sapeto kina mabaga mji mzima nature nature.
 
Tunafanyaje sasa kumrejesha huyu msela... Ngoma yake ya 'sonia' inatoka nilikuwa 5. Hakuna mobitel at that moment 2003...ndo bongo flavaour inachanua

Thiiiijui....
 
nye ndo wale masista du mlichaguliwa mje wilayani halafu mnakuja na swaga mnakimbiza wilayani mpaka vinyozi

Sijakuelewa....
Mpaka vinyoz?
Tunawakimbizaje?
 
Mtoto Idi,
Yaleo kali,
Tunafanya kazi alishirikishwa na mkenya,
Nakumbuka Tosamaganga kuna jamaa mwaka 2003 ,alikuwa amepewa jina la Nature aliimba kama yeye

Mapato aka tunafanya kazi faida haijaoneka, umo Nature yumo na machizi K South toka Kariobange Kenya.

Dah usinikumbushe hiyo mwanangu naikumbuka ile bills ya kipindi hicho ukiingia ukitoka unanuka sigara mpaka socks. Nature anazipanga na Steve b live live club kinanuka mbaya. Raha zile sijui kama tutazipata tena kizazi hiki acha tu.
 
Tunafanyaje sasa kumrejesha huyu msela... Ngoma yake ya 'sonia' inatoka nilikuwa 5. Hakuna mobitel at that moment 2003...ndo bongo flavaour inachanua

Fela anataka kujaribu kumrudisha ila haiwezi kuwa kama kipindi hicho wakati wake ushapita. Ingekuwa rahisi kiivyo watu wangepigana Kibra arudi.
 
Sijakuelewa....
Mpaka vinyoz?
Tunawakimbizaje?
Mi nimesoma shule za mikoani,yaani vitoto vya dar vilikuwa vinakuja na swaga,shuleni wanaomba disko na kutoroka kwenda mjini kucheza disco,,,sasa school kwetu vitoto vikali vilikuwa vinatoka na vinyozi,ndo maana nikasema hivo
 
Mi nimesoma shule za mikoani,yaani vitoto vya dar vilikuwa vinakuja na swaga,shuleni wanaomba disko na kutoroka kwenda mjini kucheza disco,,,sasa school kwetu vitoto vikali vilikuwa vinatoka na vinyozi,ndo maana nikasema hivo

Mhu!
Inaniuma sana...😎
 
Dah! Long time sana hiyo... enzi ambazo ilikuwa kawaida sana kusikia mshikaji kala school fee ili aingie studio, bro kaharibu home, kenda south!! ukiwa mtoto mtii fulani hivi, full ku-make hamsini hamsini, hesabu ikitimia unakimbilia Kariakoo kununua tape ya instrument na empty kwa ajili ya kujirekodi huku mnachana!! Kibra kwa kupenda sifa, anapewa collabo kwa mara ya kwanza na Mabaga... duh, wacha aharibu hadi watu wakahisi pini ni la kwake yeye wakati kakaribishwa tu na wakati watu bado wanadondoka na vina vya kumuomboleza Mwalimu, ye ndo kwanza akaja na mistari "nenda mwalimu unaturushia stim kila msimu, njaa kali, jaabal, upuuzi!" Jamaa alikuwa hakosei...
 
Thiiiijui....

Mtoto Sonia mimi nimekuzimia...
Katika kukupenda mimi nimeonesha nia.×2
Sooonia (oooh sonia) mi nakupendaaa.
Huujui huu wimbo mumy? Mimi huniambii kitu kuhusu pini za enzi hizo..
Si unajua akili za kitoto tena?
Kitu hakibanduki akilini.
 
Back
Top Bottom