TIGO na Deni La SMS!

BabaDesi

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2007
Posts
6,122
Reaction score
4,060
Bila kujua, bwana mdogo alisajili line yake ya Tigo kupata huduma ya Utabiri kutoka 15501. Alichokuwa hafahamu ni kuwa meseji hizo zinapoingia kwenye simu yako zinakula pesa kiasi cha shilingi 150. Simu yake ikiwa haina Credit message hizo haziingii lakini mara awekapo tu vocha message hizo hufululiza kuingia na kutahamaki simu inabaki haina hata senti tano huku akiwa hajapiga hata simu moja.
Amejaribu kupiga 100 ili kujiondoa kwenye huduma hiyo hajafanikiwa. Je anaweza kufanya nini kingine ili kujitoa kwenye huduma hiyo??? Msaada Tafadhali.
 
Mkuu mwambie aandike neno ONDOA kwa herufi kubwa atume kwenye hiyo namba 15501.
 
Wanawaibia sana watu hao ondoa weka zaoo hizoo.....zinakutumia tuuu hata kama huja request ukisema washa utakomaa.......
 
Yaani huu mtandao siku hizi unakera sana,kwa siku unaweza kupokea MSG kama 10 hivi za promosheni zao, eti oh"unahitaji kazi tuma msg" yaani ni kero tupu.Ila bado nipo nipo nao kutokana na gharama zao kuwa angalau nafuu kidogo.
Fanya kama alivyo kushauri Dmaujanja1.
 


...Nimemuambia bwana mdogo ajaribu ulichonieleza kisha aweke shilingi 500 aone kitakachoendelea. Amefanya hivyo na ameniambia kuwa hadi sasa hakuna msj iliyoingia na kula hela zake wakati zamani zingeishaingia kama tatu hivi na kuacha balansi yake Nil!!!
Kweli hakuna kisichowezekana JF! Amesumbuka na hiyo issue karibuni mwezi mzima huku mimi nikimkazania tu apige 100 ili kupata solution, wakati 100 yenyewe ni 'Bidhaa Adimu' !!
ASANTE SANA, Mkuu!
 
Yalinikuta hayohayo Zain
Nilituma sms kwenye namba waliyoipromoti kupitia sms kudownload habari za kimataifa. Lakini hawakupi the how to unsubscribe... Ilikuwa inafululiza kudownloada kila ahsubuhi na jioni. asa nikiweka mijivocha ili nimpigie nyumba ndogo natahamaki nimekwanguliwa yooote.

Lakini niliwatolea macho mpaka wakaitoa wenyewe

Kweli bongo shamba la bibi
 
ikiwa na shida yoyote na mtandao wako wewe niandikie pm utapata suluhisho ndani ya dakika 20 tu
 
duuh, Nilivyosoma heading nikajua mtu amekosea pahala pa kuanzishia thread. Pathetic imaginations my world....! πŸ˜‰
 
duuh, Nilivyosoma heading nikajua mtu amekosea pahala pa kuanzishia thread. Pathetic imaginations my world....! πŸ˜‰


Hujatulia. teh teh teh !! πŸ™‚
 
... Ilikuwa inafululiza kudownloada kila ahsubuhi na jioni. asa nikiweka mijivocha ili nimpigie nyumba ndogo natahamaki nimekwanguliwa yooote.

Kny bold....was this necessary here?
 
Nilikuwa Facebook, nikaona swali kwenye matangazo pembeni, nikalijibu, wakaniambia nimeshinda sms 100, ninachotakiwa kukifanya ni kuweka simu no. yangu, wakanipa kodi nikatia kwenye simu yangu. Wiki 1 imenila euro 15. kila wakati napata sms ambayo inachukua kama 2.50 euros. Nikaenda ofisi yao , wakasema lazima uende online ku-cancel. Nikienda online , kuna fomu wanataka details zangu zote, nami naogopa kuwapa , maana wanaweza kuzitumia kutengeneza contract,maana mimi sija omba huduma ya vitu wanavyonitumia(mms,nyimbo ku-download, nk) Sina njia nyingine , inabidi kubadili no. ya simu. Never again nimekoma!
 
All in all MAujanja huo ni wizi mtupu......... they dont tell us how to get out, they only tell us how to go in

tiGO wanakaDECi frani
MTM- nikweli mkuu wametengeneza Deci ktk liquid form siyo Sold form maana hawakulazimishi kujiunga but wana kusms ukikubali umeliwa.
Tatizo ninaloliona mimi ni hii Customer Care ya TiGo now dayz kama haipo vile maana # 100 kuna longolongo tu sijui tukashitaki wapi?
 
Nacho kushauli n kwenda na kurenew line upya apo ataepukana na hyo kero
 
Ukitaka kuwapata fasta wapigie TIGO huduma ya wateja unatozwa sh.100 tu piga 0713800800
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…