Tigo na makampuni mengine ya simu njooni mjibu tuhuma hizi kabla hatujawakimbia

S.M.P2503

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2008
Posts
2,421
Reaction score
4,344
Kuna madai yaliyo tolewa huko London mahakamani kwamba Tigo muliwapa watu fulani data za kumfuatilia Tundu Lissu. Mbona mmekaa fofofo hadi sasa hamseki kitu? Mpaka sasa hamja kanusha kwamba ni ya uongo- kama ilivyo lipotiwa: Firm disclosed phone data of shot Tanzanian politician, UK tribunal hears

watu wenu wa vitengo vya public relation mbona wako kimya hata sasa tangu madai haya yaseme au ni kweli kwamba huwa munatoa data za wateja wetu bila idhini yao?

Ni utaratibu gani huwa munafuata mkitaka kutoa hizo data kwa mamlaka?

Kesi ya London imezua taharuki kubwa kwa sisi wateja wenu, mbona bado mko kimya? Sisi wateja wenu tuwaeleweje?

Njooni public mujibu tuhuma hizo kabla hatujaanza kuwakimbia.

Mwisho, mamlaka yenye dhamana- Mbona na nyie mko kimya? Kwa ni nini msiwachukulie Tigo hatua kali za kisheriab ili iwe fundisho kwa wengine?
 
 

Attachments

  • FB_IMG_1727368868627.jpg
    57.3 KB · Views: 3
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…