Tigopesa MasterCard imemeza pesa zangu

Tigopesa MasterCard imemeza pesa zangu

rashid2025

Member
Joined
May 14, 2024
Posts
5
Reaction score
3
Habari Wana Jukwaa,

Mimi ni mhanga wa tatizo ambalo linahusisha TigoPesa MasterCard. Niliafanya muamala kwenda Alibaba kwa ajili ya manunuzi. Mara ya kwanza nilifaulu kununua bidhaa bila matatizo. Baada ya mwezi mmoja, niliweka tena pesa kwenye TigoPesa na kufanya muamala wa pili tarehe 13.06.2024.

Hata hivyo, pesa haikufika. Nilipowasiliana na Tigo, walisema kuwa muamala umefanyika. Nilipowasiliana na Alibaba, walisema kuwa muamala haujafanikiwa na kama pesa imekatwa, niwasiliane na mtoa huduma ili pesa irudi.

Nilirudi tena kwa Tigo ambao walinipa masaa 72 kushughulikia muamala huo. Leo ni siku ya 17 na bado wanashughulikia muamala. Niliwasiliana na Dawati la Malalamiko la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na kuwapa maelezo yote. Baada ya siku mbili, walinitumia barua pepe kwamba walishawaambia wahusika watatue suala hili haraka.

Leo nimeingia kwenye app ya TigoPesa kuangalia kadi yangu na kugundua kuwa wameisitisha kadi.

Naomba ushauri wenu wanajukwaa maana dola 35 ni nyingi mno kwangu.

Je, inawezekana kuwaburuza mahakamani? Maana wahanga wa tatizo hili ni wengi.

Tafadhali niambieni taratibu za kufuata na nipeni ushauri wenu.

Asanteni.
 
Habari Wana Jukwaa,

Mimi ni mhanga wa tatizo ambalo linahusisha TigoPesa MasterCard. Niliafanya muamala kwenda Alibaba kwa ajili ya manunuzi. Mara ya kwanza nilinunua bidhaa bila matatizo. Baada ya mwezi mmoja, niliweka tena pesa kwenye TigoPesa na kufanya muamala wa pili tarehe 13.06.2024. Hata hivyo, pesa haikufika. Nilipowasiliana na Tigo, walisema kuwa muamala umefanyika. Nilipowasiliana na Alibaba, walisema kuwa muamala haujafanikiwa na kama pesa imekatwa, niwasiliane na mtoa huduma ili pesa irudi.

Nilirudi tena kwa Tigo ambao walinipa masaa 72 muamala huo. Leo ni siku ya 17 na bado wanashughulikia muamala. Niliwasiliana na Dawati la Malalamiko la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na kuwapa maelezo yote. Baada ya siku mbili, walinitumia barua pepe kwamba walishawaambia wahusika watatue suala hili haraka.

Leo nimeingia kwenye app ya TigoPesa kuangalia kadi yangu na kugundua kuwa wameisitisha kadi.

Naomba ushauri wenu wanajukwaa maana dola 35 ni nyingi mno kwangu.

Je, unaweza kuwaburuza mahakamani? Maana wahanga wa tatizo hili ni wengi.

Tafadhali niambieni taratibu za kufuata na nipeni ushauri wenu.

Asanteni.
Tigo wezi, huduma zao mbaya.
.Mimi mwenyewe nina kesi nao.
 
Kama ni hivi ni bora watu watumie prepaid cards za bank
 
Tigo ni wahuni, hata usingefanya huo muhamala wangekuja kusepa na hela siku usiyotarajia.
 
Sina hamu na malipo ya mtandao hasa hawa Tigo!
 
Mimi card ya tigo toka juzi naona haifanyi kazi
 
Back
Top Bottom