Tijipime kwanza. Siyo vibaya.

ndayilagije

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2016
Posts
7,491
Reaction score
8,304
Kila kitu kina gharama yake wapendwa.
Kabla hujafanya maamuzi jipime kama utamudu.

Hakuna jambo lolote lisilo na wajibu.
Kabla hujaamua kuolewa/kuoa jipime kwanza Kama utaweza au japo kujitahidi tu kuwa mke/mume.

Kabla hujaamua kuanzisha biashara jipime kama uko tayari kukabili changamoto zake.

Kabla hjaamua kuzaa jipime kama unaweza kulea.na kuwa mzazi bora.
Kabla hujajikita kwenye kilimo fikiria kuhusu utunzaji wa shamba,palizi na mbolea.

Wengi tunatamani kupata mafanikio maishani,lakini hatutaki kusulubika... matokeo yake tunaangukia za uso na kuanza kuroga au kwenye maombi na maombezi.

Imeandikwa utavuna ulichopanda.
 
Watu wanaelewa hii kanuni sema wanapuuza tu au kuona kuna muda wa nyongeza
 
Watu wanaelewa hii kanuni sema wanapuuza tu au kuona kuna muda wa nyongeza
Labda! Ila naona kama tunaanza kuwa na vijimelea vya kutowajibika hivi. Nothing materializes from nothing, except may be God.
Hata ukipata bure utashindwa kusustain.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…