Time travel na ufunuo wa ufufuko

hyo inamtokeaga ata dada angu ambae kama mapacha wa nje
na kuna wakat nikiwaza kitu cha hatari huwa akinitokei ata kma nakoelekea kuna hatar hyo imeniokoa katika mambo meng sana haswa nlipokua shule mpka chuo ila nkiwa na kitu 100% kufanikiwa akifanikiwi
 
na kuna wakat nikiwaza kitu cha hatari huwa akinitokei ata kma nakoelekea kuna hatar hyo imeniokoa katika mambo meng sana haswa nlipokua shule mpka chuo ila nkiwa na kitu 100% kufanikiwa akifanikiwi
 
Alikuwa na mapepo ya kichawi ukitaka awe mchawi, tunajadili uchawi jaman?
 
Maada | Unafasi | Jicho Ona Kote na Mote | Wakati | Nishati

Vyote hivi ni MOJA.

... Vile kuweza kusema kwa mfano: 'Mungu yuko pahala pote' na tena kusema: 'Ufalme na Nguvu na Utukufu, viko naYe milele na milele'; kauli hizi mbili ni mbegu kwa ukweli rahisi, japo unaweza kutatiza akili za kawaida za sisi watu.

Mungu ni 'maada', 'unafasi', 'fahamu katika chochote na vyote', 'wakati' na 'nishati'... Ni tu bado kidogo elimu yetu ya kawaida ina ukomo katika uono na vina vya tafsiri. Hii ni ELIMU 1.0...

Milele na milele ni fanusi ya 'wakati'... Nguvu na Uweza ni fanusi ya 'Nishati'; nishati kwa tafsiri ya fizikia ni 'sehemu' tu ya 'ukweli mzima'...

Wenye jitihada za kutafuta kujua ilivyobora, wataanza kujinasibu na ELIMU 2.0: Uono na Ufikirifu Mifumo; huu utaleta 'daraja' la maarifa kwa >'Ukweli Mzima'<...

Lakini tena, ELIMU 2.0 inatengeneza njia kwa ELIMU 3.0 ambavyo tutaanza kujinasibu na uwezo na karama zinazopitiliza kawaida -- hii kawaida ya 'akili ya nyama'...

Sahau unachofikiri unajua kuhusu fizikia, kemia, hisabati, jamii na mawezekano... ELIMU 1.0 bado ni 'danganya toto...'; ni 'kujua mambo kwa sehemu'--kule kufanania na 'kujuajua' lakini si kujua kamili... Tafuta 'ukamilifu' katika kujua, na basi usije kushangaa, nikujitafuta je, wewe mwenyewe u nani hasa?

Uzima wako ni fumbo katika 'Mungu'--wakati ni konjugali ya 'Mungu mwenyezi'; ukiwa na maarifa ya ELIMU 3.0, uwezo unafanyika kwako kufahamu hata yaliyo katika 'wakati mwingine', kwa kuwa kila mwenye usentienti--mwenyeufahamu, ana sonafi--hichi ni kitovu ambacho 'siri za nafsi zako' katika uwepo wako huku ama kule, kiwakati, zinaishi na kudumu... Na sahau unachofikiri kuhusu wakati... Akili ya nyama inadanganya, kule kuona 'matukio' yako kana 'yanatoka nyuma kwenda mbele'... Wakati, si kitu hasa cha namna hii--matukio ni tafsiri tu alama zinazoishi, ukibaini undani wa alama hizi unaweza hata 'kuathiri' mambo ya 'jana' na hata 'kesho' pasipo 'msababisho/msababishano'...

Na ndiyo, ukibarikiwa ufunuo, utashangazwa namna gani 'Sala ya Bwana' aliyofundisha Yesu ni lugha ya 'kutenda' pasipo 'matendo' na hali unajinasibu na 'athari' za mambo ya nyakati--riziki kwa wakati, kuvunja minyororo ya 'madeni', 'kuchagua ilivyo bora/yaani kuepushwa na fanusi ibilisi ndani yako' na hasa: 'Mema yasiyoonekana' yaje pia kama 'hapa na sasa'; ndani ya 'muktadha wa mambo ya mbingu na nchi'...

Utakuingia 'uono na ufikirifu mifumo' fasaha: Yesu ni mmoja wa watu hawa 'wakujinasibu na nyakati zote' kupitia 'Metafanusi'--'Uzima katika yote' ilivyo ni 'Mungu'... Hili halipasi kukushangaza, jiulize tu kwa nini kuna mambo, katika habari za simulizi za injili, zinaonesha kuwa aliweza kuyazungumza kana kwamba yatakuja kutukia mbele ya wakati, na tena kweli yanafanania: >'maarifa kuja kuongozeka', 'utapeli wa kidini'<--alionaje? Ni mambo ya metafizikia ya Elimu, ELIMU 3.0: Ilimu ilivyo ni metafizikia ya Elimu...

++++

Kudumu kwa Jamii yoyote kuna upande mwingine wa mambo ambao Elimu 1.0 ‘haina msaada’; kwa kuwa ni Elimu 3.0 ndiyo yenye ‘ufunguo’ wa ukweli wa mambo—kweli inayoweza kupitiliza kawaida tuifahamuyo.

Elimu 3.0: Ilimu ilivyo ni metafizikia ya Elimu; kiuono mifumo, tena kwa mfano kuja na fremu-kazi ya Uono mifumo, tunaweza kuibaini kwa kuanza kushughulika na visomo kwa ‘numenoni’ ya finomena iliyo ni ‘wakati’. Kwamba huu ni muktadha wa maarifa unaoanza kuwa ‘vina vya tafsiri’ ya mambo iliyo ni ‘nje-ndani’ kwa uono wa kawaida wa mambo. Elimu 3.0 ni ‘Ufunuo’ kwa kuwa hujinasibu na ujuzi, upeo na karama za ‘hisia ya sita’ katika ‘jicho la mtu’--fikara.

Ilimu ilivyo ni metafizikia ya Elimu, huanza na ‘muda’ katika wakati, kadiri huu ni kizio cha mabadiliko ya kimienendo, unafasi(supasha), nishati na dutu-meta. Basi haya yote kufuzu akilini mwa mtu kama ‘mapana nje-ndani’ ya mtu, taasisi, machaguo na wakati. Akili ya mtu mwenye kujinasibu na ‘hisia, maono na makarama’ ya Elimu 3.0 haina budi kuwa na ‘vina vya tafsiri’, ‘ubayanifu’ na ‘Kognisha’ isiyolazima kuwa kama kawaida ya mambo yajayo na ‘jicho la kawaida’ na ‘mafikara’ yake.

Ilimu ilivyo ni metafizikia ya Elimu, hujinasibu na mantiki inifinitamu, viasi na hadhi zake katika maada halisi na pia >mfumo mpinduko< wake kwa kikosmosi halisi(unafasishi dhahiri) na ya ‘gizani’. Hili linatuletea Elimu 2.0 na Elimu 1.0 katika sura ya uono, ufikirifu na kumbukumbu ziwezazo kuwa na kinyume na kawaida tuliyoizoea. Unafasishi na muda kuwa basi viwili ninavyoingiliana kana vile, unafasi unaojifinyia kwa ndani ndiyo chanzo cha ‘kani kitovu’-- kuelekea ncha moja isiyokuwa na mwanzo wala mwisho, katika maada; na ‘mwangaza’ kuwa ‘kani’ inayohuluku kinyume cha maada ilivyo ni ‘wakati’. >Wakati hujifinyia kwa ndani katika kosmosi ya ‘gizani’< ambavyo humo huwa na ‘marefu, mapana na kina’ kadri maada huwa na ‘marefu, mapana na kina’ katika ulimwengu wetu dhahiri—unafasishi. Kwa hivyo tunaishi katika metafanusi ya ilivyo ni unafasishi-wakati katika sifa ya hadhi ya ‘unnje-ndani’, na huku hapo hapo ni ‘undani-nje’…

Yesu aliposema >‘Ufalme wa Mungu/Mbingu’ u karibu—u ndani yako<, sasa ni zama na wakati wa kutambua ukweli hasa wa jambo hili…

Kwa mtu wa Uono na Ufikirifu mifumo, kuna namna ya kubaini topografu za mafikara-maarifa kwa kadiri vipi Ulimwengu wote mzima upo >ndani-na-nje ya kila ‘nukta’< ya kizio chochote cha maumbile ama wakati. Mafikara-Maarifa yetu, ni kujua kwa sehemu japo kwa >mtu wa uono na ufikirifu mifumo anaweza kutumia lolote lifikiriwalo na wanajamii< ili kubaini vikomo vya uono, ontolojia ya taasisi na sura na muenedendo wake. Pasi ukiondoa Wafikririfu wa kawaida, wawe wa jana, leo ama kesho--hawa si wajuaji kamili; Labda ni Wasikirifu ndiyo wamepata 'kupitia ufunuo' halafu wakazungumza ama kwa metafo ama 'mafumbo' kuhusu ulimwengu na walimwengu--Yesu akiwa ni mmojawapo wa Wasikirifu maarufu, ama tuseme 'si mgeni' katika kasikio ya wengi. >Wasikirifu wote wamepata kubaini 'undani-na-nje ya kila nukta' pia -- huku wakipata shida kuelezea ukweli hasa wa mambo kwa walimwengu<... Paulo aliposema juu ya kuishi kwetu, kuwa ni neema, kwamba >katika ‘yeYe’, tunao huu uzima< – alikuwa akiashiria ‘Metafanusi ya Utatu Mtakatifu’...Na tena basi Paulo aliponena juu ya >‘kina, mapana na marefu’< ya ‘upendo’, kama ionekanvyo na watakatifu wote alikuwa anaeleza juu ya muktadha wa metafizikia ya ‘kani kitovu’>(nguvu yunivasali ya uvuto)< ilivyo hasa ni ‘Upendo’ na hekima kwa waja wema -- upendo wa ‘Mungu’ usiyojua mpaka, 'muktadha mwana' wa 'Utatu' ulio ni ‘Kristo’…

Lugha ya uono na ufikirifu mifumo kwa Paulo ndiyo basi ni muktadha wa kubayanisha mahusiano ya kifanusi kwa ‘Kristo’ na ‘Uzima katika Mwangaza wa Milele’-- kutofautisha tafsiri ya maono ya kimafikara-maarifa ya ‘Elimu 1.0’ na ‘Elimu 2.0 iliyonasibika kufahamu yale yaliyositirika’-- ile >konjekcha ya ‘Metafanusi’ ya ‘Utatu Mtakatifu’< kwa mambo ya fahari kwa miili ya nchi(udongo/unafasishi) yenye kuharibika; na miili ya mbinguni(nyotani/mwangazani) isiyo na kuharibika….

Kwa kutambua tofauti za Elimu 1.0, Elimu 2.0 na Elimu 3.0, Paulo alikuwa sahihi kabisa; tena ‘kiuono mifumo’ na ‘ilimu ya metafizikia’, alipotaja habari za >Hekima ya Mungu ilivyo ni ‘kuwa na nia/akili ya kristu’< na kuutafuta ‘ufunuo’ ambavyo >‘Muona ni Muonwa’< katika Metafanusi iliyo ni UPENDO…

Ili kubaini ‘Muona ni Muona’ huja aje na Elimu 3.0, hebu tutembure uwanja wa antakarana--alama, fahamu na hisia-akili...

Ulimwengu, kadri ya ujengaji wa taswira akili mwetu—kimafikara-maarifa, una hadhi kana 'ndumilakuwili' kwa wakati mmoja -- ni wenye dhahiri ya ‘kupimika’ na ‘isiyopimika’.

Dhahiri ya kupimika ndiko huku kuona 'lenye mwanzo, lina mwisho'; isiyopimika ni 'sifa na tabia' ya jambo ama mambo ambayo wakati wote hufungamana na 'viasi na tafsiri' katika vipawa vyetu vya akili na uweza wetu wa kawaida wa kuhisi/kujua/kubaini kweli ya jambo husika. Hili kwenye sayansi ndicho huzaa ujuzi wa 'uchanganuzi kiasi' na 'uchanganuzi usifa'--wenye kuzungumza haya kwa lugha ya kiingereza wangalitaja 'quantitative analysis' na 'qualitative analysis'... Hivi kutafsiri kimafikara-maarifa kana kwamba dutu kuwa na tabia za ‘mjengeko’ na ‘ubomokaji wa kimaada’ unaoweza kutathminika kimisingi ya vitendo ya sayansi, kiviasi na tabia za oanifu –- tawi la sayansi lijulikanalo kama >kemia<...

Dhahiri pia hupimika kwa 'nishati na mienendo'... Kwamba, vitu hujongea kwa nguvu na mzuto, wenye kuzungumza haya kwa lugha ya kiingereza wangalitaja >'Power' na 'Momentum'<... Hili ndilo leo limetamalaki kwenye visomo vyetu vya fizikia, kwa kuwa >fizikia< ni visomo vya uhusiano wa >'maada'< na >'nishati'<; na tena, kimahsusi, hujitukiza katika >'fizikia ya makanika ya ki-Newton'<. Fizikia inaanza kuonekana kana 'si ya kawaida kawaida' kwenye visomo vya >'mienendo halijoto'<, wenye kuzungumza kiingereza hutaja haya kuwa ni mambo ya 'thermodynamics'; na katika mienendo halijoto, jambo fulani -- kama kwenye visomo vya 'kemia' linaanza kusumbua akili ya kawaida ya mambo na tafsiri zake. Ulimwengu mpana, >kosmosi<, kwa mfano, umefanyika kwa >'ukungu wa nyota' na 'utupu'<--sayari zote ni sehemu finyu finyu finyu kabisa ya ulimwengu unaoweza kuonekana kwa macho ama hata vifaa bora vya kiuonaji wa uchunguzi; sasa swali linakuja: >"joto na baridi"< vinauhusiano upi na 'kuanza' ama 'kwisha' kwa ulimwengu? Hili ndilo fumbo mojawapo kwa 'mizania' ya 'sifa/tabia/mwenendo... Lakini, tusihofu; kwa akili ya kawaida, kupitia visomo vya Elimu 1.0, hata sayansi haina jibu la msingi ila tu >'porojo' za 'nadharia' za 'mwanzo na mwisho'< wa ulimwengu, walau za muktadha fulani wa uono usiokamilifu -- mambo kama 'Big Bang'/'Maada kiza'/'Mawimbi Maikroniyi ya Upande wa Nyuma-mwanzoni kiwakati'...
Kwa hivyo haya yatukumbushe la msingi: ‘hesabu’ na ‘hisabati’ hujengwa kwa misingi ya ‘viasi’ na ‘ulinganifu’. Yote yenye 'mipaka' tunaweza kutafuta namna ya kuyakadirisha hivi ama vile ili tuyalinganishe kwa hili ama lile lenye kuonekana kama kwamba kuna ‘uhusiano’. Lakini kwa yale tusiyoweza kuyapima hasa, basi, mbinu visomo za kutegemea hesabu na hisabati zawa 'hazina msaada'… Fumbo hasa la kivisomo - Elimu 1.0 kwa >‘Uyanikifu ama/na Uyanikifu Mkuu’<...

Na hapa ndipo tunapata ufunguo, kwa nini ‘Elimu 2.0: Uono na Ufikirifu Mifumo’ yajibainisha utofauti wake na ‘Elimu 1.0: Kujua kusoma na kuandika’ kwa kuwa hii Elimu 2.0 hupindua 'uono' kutoka kwenye paradaimu za ‘kidogo na kidogo hufanya kikubwa’ yaani uchanganuzi wa kiyakinifu ilivyo ni Elimu 1.0; hadi kwenye usanisi: kutathmini 'mahusiano' ya vifanyavyo muktadha wa 'viunda na vitendo ingilianifu' kwa kadiri 'mafikara-maarifa' ya kubayanisha yote hayo kana ni sehemu ya kweli ipi ya 'nzima moja'--kwa kuoanisha 'mantiki infinitamu' na 'indefinitamu ya usupasha';>Uzima kama mwongozo wa kubayanisha 'mifumo'<... Na basi fizikia ya kikwantumu hupembea kati ya 'fanusi wimbi' na 'chembe-dutu', na kumbe yote mawili ni fumbo la 'muona' ni 'muonwa'; kama >alivyobaini mwanasayansi wa fizikia ya Kikwantumu Max Planck<, lau katika skeli za maikroniyi na tena kiufikirifu/nadharia juu ya maumbo na fahamu za uono/tafsiri...

Mbali kupita ulimwengu wa vipimo na mashauri ya tafsiri, akili yetu ya kawaida haina uwezo wa kubaini 'dhana' na 'tafsiri' kwa ‘udhahania’ wa mambo. Kwa mfano, unashika kitu mkononi nakusema hili ni jiwe... Je, jiwe limeundikaje? Kama jiwe limefanyika kwa chembechembe ndogo sana za kimuundiko, Je, hizo nazo ukizigawa utaishia na nini? Hili ndilo lipelekea Myunani Demokratiasi kunadharisha: ikiwa utagawa kitu kiwe kidogo... halafu kidogo... halafu kidogo mpaka basi -- utafikia mahala na >'kitu kisichogawanyika'<... Japo sayansi ya leo humnukuu Demokratiasi kwa uasisi wa dhana ya 'atomu/tonadari/atomosi' kama 'ile chembe isiyogawanyika'; ukweli wa jambo lenyewe hasa ni kwamba Demokratiasi alikuwa akizungumza kimetafo ya jambo iliyokuwa ni kinyume na 'Kubwa Moja isiyogawanyika' iliyokuwa ikiaminiwa na wengi wakati wake--huku akiwa ni 'muangua kicheko'... Lakini, hapa tushike moja -- katika matendo ya kutoa ama kujumlisha, ukweli wa jambo unaweza kufaa 'hisabati' kwa mapana fulani lakini kumbe ikafika mahala, hesabu haina la maana hasa... Hili tulitie akilini kama 'Mantiki Inifinitamu'...

Sasa, Akili zetu haziwezi kujishughulisha na jambo la 'Mantiki Inifinitamu' ila kwa 'kuuzunguka mbuyu'... Jambo hili ndilo hututoa kwenye 'Elimu' na kutuingiza kwenye 'Ilimu'. Elimu 1.0 kama maarifa na ujuzi kwa vile vyote vyenye mwanzo na mwisho; na Elimu 2.0 kama ujuzi wa kutafsiri mapana ya uono(muktadha), mahusiano ya mambo yake na fanusi zake. Elimu 3.0 kuwa basi ni ‘ILIMU’ ilivyo ni metafizikia ya Elimu...

Hisabati ni ‘uti wa mgongo’ wa Elimu 1.0… Hebu tuyatazame ya hisabati na kihisabati – matendo yake, mantiki zake na utafsiri wake kuhusiana na ‘Mantiki Infinitamu’ na mapelekeo yake yenye kujinasibu na ‘Metafizikia’.

Mantiki Infinitamu, kama vile ilivyopata kuwa jambo dhahiri kwa mwanahisabati >George Cantor<, ni lile la kuliita 'refu lisilona mwisho' kwa kuzidi/kuongezeka katika namna ya seti yoyote ya muambatano wa vitu -- vitu vya tafsiri kwa mapana ama ukubwa. Kwa mfano, moja(1) iliyo ni kitu chenye 'makubwa' fulani, kugawa kwa sifuri(0) ya 'makubwa', jibu lake, katika hali isiyokawaida >kihisabati< -- ni 'kuelekea inifinitamu' ya 'makubwa'; yaani si kusema hasa 'haiwezekani'(kugawa makubwa) ila kadiri ya jitihada hii ni 'kuelekea inifinitamu' ya 'vina vya tafsiri', hata kihisabati; nayo huandikwa (∞). Hii ni namba nane(8) iliyolala. Ukitumia kikokotoleo kubofya '1 'halafu 'gawanya' na kisha 'sifuri', basi siyo ajabu mara baada ya kubonyeza '=' itakuja herufi 'E'. Hivi ni basi kwa kuwa 'mantiki infinitamu' ijavyo kupitia ukadirifu wa vikomo; yaani ukichukua nambari nzima ukagawa kwa ukiduchu, kiduchu tena kiduchu... kiduchu mpaka basi--kadiri ya 'jibu lake' itakuwa inaelekea kwenye >'inifinitamu'<. Na basi kwa kanuni za matendo ya kihisabati yenye kuhusiana na kujumlisha, kuzidisha na kugawa, kwa vi-operatisho ‘sifuri’ na ‘infinitamu’ na ‘moja’, 1 = 2… Kupindua kanuni hizi ndiko kumetuletea pia dhana ya ‘Nambari Tata’, yaani nambari ‘moja(1)’ ndiyo pekee yenye pacha hasi(-1) ambavyo ikibidi kupunguza ‘ukubwa eneo wake kimraba’ huwa na kadiri ya thamani ‘i’, yaani kupelekea uono wa kitafsiri hisabati ya kwamba √(-1)=i. Hii ‘i’ ni herufi ya kwanza ya neno ‘imaginary’(kng), yaani ‘yakufikirika tu kuwepo’, kiakili, pia kuwa na kadiri ya thamani ya kitathmini katika >milinganyo ya kinambari tata<...

Kinyume cha Mantiki inifinitamu, ni 'inidefitamu'; yaani kwamba sifuri(0) kugawa kwa (1) jibu lake si sawa hasa na 'sifuri'... Bali ni namba ndogo ndogo ndogo zaidi kuelekea 'sifuri'. Je, kuna 'sifuri' hasa 'inayopimika'? Ikiwa sifuri haipimiki--kwa kuwa ni sawa na hakuna kitu, basi ulimwenguni hakuna 'sifuri' hasa, bali kiduchu, kiduchu, kiduchu... 'kiduchu mpaka basi' ya kitu fulani… Kwa lugha ya kihisabati kupitia Kiingereza, operesheni ya namna hii hutajwa ni ‘hali’ ya kuwa ‘undefined’--kile chenye kukosa kitovu cha utathmini kwa wakati…Ikiwa kwenye 1/0 tunaona wakati ‘unasonga mbele’, twaweza kusonga nao sambamba; 0/1 twaona wakati ni ‘SASA’ lakini ni kama vile jibu tutalipata iwapo huu utasimama… Kwa hivyo tunaweza kubayanisha ‘lugha alama’ ya kiwakati katika 1/0 na pia 0/1—kivyote viwili, ‘kiwakati’ na ‘kisupasha’...

Kihisabati, na tena opereshani za kiunambari tata, Umbo duara ndilo hukutanisha mawili haya, kwa mlinganyo wa Euler, ubayanishao: >eiφ=cos φ+isin φ< ; kiukubwa eneo, √(-1) ni basi, kwa sehemu, nasibu kiungo ya kutanukia kwenye >‘supasha giza/supasha isiyodhahiri’<, na kusema tena ni >unafasi-wakati< uliojificha.

Kupitia'nukta ya kati ya kipenyo' hasa kwa mduara/tufe-- ule ‘ukatikati’ wake hasa ni kitu kisichopatikanika kwa 'hakika kamili'. Katika ulimwengu wa mapana na marefu kwa mfano, ikiwa unatafuta 'nukta katikati hasa ya kipenyo'ya duara lolote, daima utaishia na 'eneo la kadiri'la hiyo nukta hiyo kuwepo lakini si 'nukta yenyewe hasa'. Hii ndiyo kisa na mkasa wa pai (π), kugawa ‘marefu ya mzingo wa duara’ kwa ‘marefu ya kipenyo’ chake daima kunazaa namna ya nambari 'isiyokamili' bali tu 'kukadirishwa' kunako hatua kadhaa za desimali kuchukuliwa, kwa mfano π=3.14 badala ya π=3.141592653589793238.... Pai ni >nambari isiyoreshenika<--wenye kuzungumza lugha ya kiingereza kuifahamu ‘Pai’ kwa kusema kuwa ni 'irrational number'… Hili likijinasibu na fizikia, maarifa Elimu 1.0 ya visomo kwa nishati, maumbo, mienendo, vizio vya ukubwa na tabia zake basi linakwenda kuingiliana na mambo ya dhana na vina vya tafsiri kwa >mlinganyo wa Schrödinger<, >‘kanuni ya Heisenberg’< na dhana kwa >urefu wa Ki-Planck<… Ambavyo makaniki ya ulimwengu dhahiri, machoni pa mtu wa kawaida wa visomo Elimu 1.0, yanaweza kukadirika kwa >‘fanusi wimbi’ ama ‘mifumo chembe-chembe-mienendo’<...

Tukirejea haya katika shauri la demokratiasi, ndiyo tunapata mwangaza ya kuwa labda kwenye kidogo kidogo kidogo mno cha ulimwengu ni 'kimoja' na kile kikubwa -- 'kikubwa kama yote na kila kitu'... Yaani ulimwengu wote mzima ni kitu 'kimoja'--iwe dhahiri(1) na kisichodhahiri(0); kifanyacho 'mpango mzima' ni kitu/jambo/kweli iliyo ni MOJA.

Wayunani, walikuwa maarifa ya kiakademi na esoteria kwa wakati mmoja. Wakati wa Renasansi, watu wa magharibi walivutiwa na maarifa ya Kiyunani lakini kwa kupendelea matumizi ya >'ubongo wa nusu ya kushoto'<--akili ya kimantiki, basi ndiyo kuna baadhi ya 'hekima' fulani iliwapita pembeni wafikirifu na wanasayansi wa siku hizo; naam, yumkini hata wengi wa leo. Hebu kwa mfano, tutafute kubaini asili ya alama 'Alfa', 'Omega' na 'Delta'.

Katika kitabu cha >Ufunuo<, kuna habari za 'Ukuu' unaojitambulisha kuwa ni 'Mwanzo' na tena 'Mwisho'--Alfa na Omega; jambo hili ni metafo, lakini hapo hapo ni alama na ukweli wa mambo. Leo hii, sisi wanadamu -- watu wa dunia hii, tuna ufikirifu lemavu... Japo ulemavu huu wa kiakili si wa kudumu. Katika uzi wa "Njia Nyepesi ya Kuundoa Umaskini" tumeanza kulimulika hili kusudi 'tumalizane nalo' kwa kulingania 'ufikirifu mifumo' iwe ufundi kwa watu wote na ili tuweze >'kuondokana na akili ya kimaskini'<... Sasa, ambacho kilikuwa hakijatajwa, sambamba na hilo, ni 'ufikirifu bebanifu picha' -- haya kwa wenye kuzungumza kwa lugha ya kiingereza wangalitaja 'Systems Thinking' na 'Topological Thinking'....

Kwa nini tunahitaji Ufikirifu Mifumo na Bebanifu picha?

Duniani leo hii, visomo vyetu, ujanja wetu na michezo yetu ina mtaji kwenye 'ulemavu wetu kiakili'... Iwe siasa, uchumi, mipango yote imegubikwa na >'vina vya tafsiri' vilivyo ni mushkeli<. Sisi watu tulionyuma kimaendeleo kwa mfano, ndiyo wahanga taslimu wa "michezo yetu, mauti yetu"... Dunia yetu ni ya vipofu kuongoza vipofu wenzao; sasa wote tuko shimoni lakini kuna wachache wanafurahia kusafiria 'nyota za wengine' kwa haramu inayohalalishwa -- na basi wote tunaridhia mchezo si kwa wema bali kutokujua ilivyobora. Mwenye kujua iliyobora, daima atachagua na kujichagulia mapito yake ilivyo vyema; ikiwa ipo nia.

Leo tuna kasumba ya 'kufuata ya magharibi' pasipo tafakuri 'dhamiri na kusudi' katika kujiondoa na utegemezi wa kimifumo na mikosi.

Ufikirifu mifumo na bebanifu picha ndiyo rasilimali-akili pekee tuliyonayo hapa na sasa itakayotunasua na mitego ya 'demokrasia' na 'chumi' za laghai za 'biashara huria' na 'masoko' kiutandawazi -- ambao kimsingi ni 'utanda-wizi'...

Kungine, umepata kuona na kusikia ya pembe tatu ya >'Siasa za Nchi', 'Mpango ya Utumishi' na 'Kujengea Jamii Uwezo'<: Namna gani siasa yaweza kuwa 'chokochoko', mipango na utumishi yafaa kuwa ni 'wito' na mikakati mipana kuliko 'shughuli ya siasa' -- namna gani walau siasa yabidi kulandana na mikakati ya muda mfupi na mirefu ya nchi...

Sasa, rejea ya Alfa na Omega, hiyo pembetatu ni 'Delta' na mapana ya jamii ni 'Omega'; pembetatu ya ndani ni namna ya 'Alfa' -- fumbo la kuhitaji kufumbuliwa...

Tumulike mawili matatu ya 'Delta'....

Sayansi na hasa fizikia na kemia, imekopa alama 'delta' kutoka kwa wayunani kuwa alama ya 'mabadiliko'... yaani kuwa kama: 'delta-joto' ni lugha ya kisayansi/kialama kwa 'badiliko katika joto'... Hili ni muhimu katika kutukumbusha kwamba 'kujua ni ualama'... Akili zetu hufanyakazi kwa lugha ya picha na ushahibiano; ndiyo maana jamii huchambuliwa kisosholojia kwa 'muuingiliano wa alama oanivu' ukiachia pembeni 'fanusi jamii' na 'nadharia migongano'. Kwenye sayansi ya uhandisi kwa mfano, pembetatu sawa hutumika kama kielelezo cha 'ufungamanifu-nguvu sawa' pale tunapobainisha 'kitovu/nguvu/kazi' juu ya uso bapa... Kwamba kuna hali tatu za utathmini, ukaaji kutulia, ukaaji pasi kutulia na nyutrali -- wenye kuzungumza kiingereza kusema 'stable, unstable na neutral equilibrium'...

Kutoka/kuhama kwenye seti moja ya maarifa na ujuaji hadi ingine pasipo mkwamo alhali tu ukaribishaji wa fikra zinazoendana, kufanana na kushahibiana ndiyo ufikirifu bebanifu picha. Mtu wa ufikirifu wa namna hii hana ukomo wa kuitwa mhandisi, mchumi, mwanasiasa, kuhani... Yeye akili yake ni kama maji. Ujuaji wake kwa wakati hauna ukomo wa kubaini, kujifunza na kutanuka katika wanda na seti moja hata ingine ya/za vina vya tafsiri.

Katika ulimwengu wa leo wa ongezeko la maarifa na taarifa; sisi watu hatuna budi kuingia katika 'toleo jipya' la nidhamu na wepesi wa akili. Ule ujinga wa 'Kima ona, kima fanya'--kuiganagana na kumuangalia mzungu kama 'mjanja wetu' hakuta tufaa kitu hasa; tutaishi maisha ya kujidhalilisha na kusubiri mzungu 'atuletee majibu na vumbuzi'... Yumkini kuna wengine kati yetu watafikiri hawana kasumba ya 'mzungu na mwafrika' kwa mfano; dah--katika ulimwengu ambao kile ukitiacho machoni 'kimetoka duniani' -- jua upende usipende tayari unanasibu ya 'kujiona mdogo' mbele ya watu hao 'kutoka mbele'... Swali ni je, mpaka lini utaendelea kuruhusu wewe na kizazi chako muwe 'wasindikizaji' duniani?

Walter Russel alikuwa sahihi: dunia hii, udunya ni maradhi ya kujitakia, akilikubwa ni kujipa mwenyewe, akisema kwa maneno yake: >"mediocrity is self inflicted, genius is self-bestowed"<...

Ufikirifu topografu kwa minajili ya mapana ya Pembetatu ya ufraktali wa ufikirifu: (1)siasa za nchi/(2)Mipango ya Utumishi/(3)Uwezo wa Jamii, hutupatia zana inayowezesha kupata koherensia ya ufikirifu ikiwa maarifa haya yatakuwa wazi kwa watu wengi ama jamii pana...

Kukosa kuona kiufundi muktadha kwa 'ontolojia ya taasisi', 'Uono' na 'Sura na mienendo ya Jamii' ndilo jambo linalozaa 'kila mtu na lwake' kimaoni, upeo na tafsiri ya mambo. Hili kwa mfano, hata humu JF linazaa mijadala isiyo na dutu kuhusu watu na taifa. Ikiwa watu wengi wanabaini jambo kuhusu 'pembetatu ya akili', siku si nyingi, umma wa wana-JF utapata chachu na ubora wa mashauri utakaopelekea maendeleo kiutamaduni na matendo... Watu wanapoanza kuwa na maua fikra yenye kufanana ama kulandana hili huimarisha 'uwezo na nguvu' kwa mashauri yao... Hili ni sawa na mfano wa tofauti ya kinguvu kati ya kurunzi ya 'mwanga wa kawaida' na ile ya 'biru'... Biru, wenye kuzungumza kiingereza huita 'laser', ni mwanga wenye nguvu na uwezo 'kuliko kawaida' na hali mwenyewe si kingine ila mwanga unaofanyika kwa mawimbi yenye koherensia ya kimnunurisho... Umoja ni nguvu--hata kwenye ulimwengu wa kiakili, mawasiliano na maingiliano; na hivyo kwa akili, hili huja na koherensia ya ufikirifu...

Kwa ujumla, sasa hivi, duniani kote lipo jambo kuu linalohitajika kutukia. Ikiwa 3% ya watu duniani wataamka kwa kubaini ukweli wa haya yalizungumzwa kuhusu koherensia ya ufikirifu, ufikirifu mifumo na bebanifu picha(ufikirifu topografu) basi ulimwengu mpya utaibuka ulio na kheri na maendeleo ya kweli. Mifumo ya leo ya siasa na chumi 'itajifia'... Mifumo bora isiyotokana na hii ya sasa ijayo kwa 'akili ya kimaskini' itainuka, kukua na kushamiri... Kwa huwa, mnyonge mnyongeni lakini haki yake apewe; kama alivyopata kusema Mfizikia Albert Eiensten, >hauwezi kutatua matatizo kwa akili ile ile iliyoyaleta hayo matatizo<... Visomo vinavyoanza michukulio ya ukosefu na mapungufu, iwe kiuchumi--dhana kama jadili za 'rasilimali haba' n.k. haziwezi kujinasibu kitopografu na visomo vya 'ujazi'.

Ufahamu Kristu< kwa mfano, unaanza na uwezo katika mtu -- tunaoweza kuutambua kama 'usanisi'. Usanisi ni namna ya kutangamanisha viwili vyenye kusigana na kuishia kwenye cha tatu ambacho ni zao ya vyote viwili -- lakini kuwa kama moja. Ni sawa na kusema pia, kilichopo na kisichokuwepo kama moja... Kilichodhahiri na Kisichodhahiri kama moja... Katika mifumo hai yabisi, usanisi ni namna ya mapigo ya moyo ama pumzi; kana kuwa--moyo hutanuka na kusinyaa na pumzi huingia na kutoka mwilini... Kutanuka na kusinyaa ni fanusi mbili tofauti kisupasha... Ili zote 'zidumu kuwepo' hazina budi 'kupeana wakati'... Hili litukumbushe jambo la msingi: 'Wakati ndiyo Muamuzi' wa mfanyiko wa yote--yaliyodhahiri na yasiyodhahiri. Tutapoanza kutafuta siri za 'wakati' basi kuna mengi, kupitia ufahamu Kristo, yataanza kufahamika ambapo kwa akili ya kawaida hatujapa kudhani ama kufikiri tofauti... Kwa mfano, watu hutaka kufikiri 'Dunia ni ya Mungu'--iliumbwa na mungu... Ambacho kitafikia akilini, pale roho ya kweli na neema ianzaavyo kujaa ndani ya mtu ni kwamba--fikiri pia kuwa 'Mungu ni huo wakati'... Basi humu Jamiiforums, hili limetayarishiwa njia kuja kuingia vizuri kwa watu, katika uzi wa Kusafiri Kiwakati 101...

Sasa katika uzi wa >Kusafiri Kiwakati 101<, tundiko la kwanza kabisa lilimtambulisha mwanasayansi Nikolai Kozyrev wa Urusi. Mwanasayansi huyu ndiyo kati ya watu wa kipekee katika karne ya 20 kupata kusema pasi shaka 'Wakati ni kitu hai' baada ya kubaini jambo kulingana na matokeo ya uchunguzi wake. Kwamba wakati una namna zake za 'kimaumbile' kama ilivyo kwa maada asili lakini '-- namna yake ni isiyo na kawaida tuliyoizoea... Humu JF tayari kuna watu wamekuwa wadadisi wa jambo/mambo kama haya japo tu wanakosa nukta sahihi ya kuyaingia maarifa ya haya. Basi katika uzi >'Dark arts za intellijensia II: Uchawi na kiini macho kwenye uwanja wa vita' tundiko namba #3<, moja ya vijalada viwili vilivyoambatanishwa, Nikolai Kozyrev anajitokeza kutajwa katika ukurasa wa 9, kati ya 23, kama (N.A.Kozyrev, Н.А.Козырев)...…
....​
Hmmm
 
Ufikirifu topografu kwa minajili ya mapana ya Pembetatu ya ufraktali wa ufikirifu: (1)siasa za nchi/(2)Mipango ya Utumishi/(3)Uwezo wa Jamii, hutupatia zana inayowezesha kupata koherensia ya ufikirifu ikiwa maarifa haya yatakuwa wazi kwa watu wengi ama jamii pana...[emoji818][emoji817]
 

Kun Siri nyingi sana katika umbaji, siku moja nitasema dah acheni tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…