Timu inayokamia wako sahihi, ila nina shida na timu zinazofanya soka kuwa vita na kukomoa

Cashman

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2018
Posts
3,017
Reaction score
5,294
Kuna aina ya mchezo imeibuka nchini hasa baada ya wachambuzi ku conclude kuwa ili kuifunga Simba unahitaji kucheza mchezo wa kutumia nguvu kupita kiasi.

Mtindo huu umeonekana kuwapa matokeo baadhi ya timu hasa kutokana na waamuzi wetu kutofuata kanuni za mpira wa miguu na kuyaachia matukio ya kurukia kwa nia ya kuvunja miguu ya wachezaji yakizidi kutokea.

Kama mpira utakuwa wa mtindo huu unaoshabikiwa na wengi wa wachambuzi wa soka,wa kuvunja ikibidi ili usifiwe kama beki mwenye "roho mbaya",basi inaweza kufanya baadhi ya wachezaji waogope kucheza kwa viwango vyao na kutafuta ligi zenye ushindani wa kweli.

Timu zinapaswa kupania kupata ushindi dhidi ya timu kubwa ila si kukomoa kwa kujaribu kuwarukia wachezaji wenzao kwa namna za hatari kwa lengo la kuwavunja ikibidi. Hii haina tija kwa mchezaji anayefanya hivyo zaidi ya kujijengea uhasama tuna mashabiki na wachezaji wenzake
 
Simba anacheza mpira mzur sana na ndoo chanzo kikubwa yeye kuingia mara kadhaa ligi bingwa kwan hajihusishi na kukamian kijinga lakn hil kuisha ni pale ambapo leque itakua na sheria kali kuhusu utovu wa nidhamu kama kusimamishwa kucheza
 
Ni kweli, Sisi Simba tunacheza mpira maridadi sana paka Bayern Munich wanatuonea wivu, tunaomba tupewe ulinzi kutoka TFF ili angalau kila mechi wapinzani wetu waoneshwe kadi nyekundu.
 
Umeona jana mpira wa Algeria na Ivory Coast yule mchezaji mrefu ila kafunga nywele kama wanawake na kufunga mpira alivyokuwa anaumiza wachezaji wenzie. Nadhani huu ulimbukeni haukubaliki katika Soka. Mbona ulaya siyo Hivi?
 
Jaribuni kuleta maoni ya uanamichezo siyo haya ya dhana dhania Wakuu. Mbeya refa katoa Kadi nyekundu na Penati, mlitaka atoe Wachezaji wangapi wa Mbeya City ili mshinde?
 
Bado mnateseka na kile kimoja cha Nguruwe kutoka Mbeya?
Naamini una uwezo wa kutoa mchango bora kuliko huu,au kwa vile wanaofanyiwa hivyo ni timu unayoichukia? Tendo lolote linaloharibu ladha ya mpira na kuhatarisha maisha ya wachezaji wa timu pinzanani likemewe na wote wapenda michezo,siyo kila wakati tucomment kishabiki.
 
Kabla ya yote timu inayokamia ndio inakuwa inafanyaje? Kukamia ndio nini?
 
Sina shida na mechi ya mbeya,nina shida na tabia hii kuanza kuwa sugu.Ilianza mwaka jana,na sasa naona ndiyo imekuwa staili mpya ya kupambana na Simba.

Kipimo kizuri huwa ni mashindano ya kimataifa.Hapo ndipo utajua ubora wa timu yako.Ni muhimu timu zetu waache kucheza kwa nia ya kuvunja wachezaji wenzao hata kama wamelipwa kufanya hivyo.
Bingwa wa kweli atapatikana kwa ubora wa kikosi na siyo ubingwa wa kumdhoofisha mpinzani
Jaribuni kuleta maoni ya uanamichezo siyo haya ya dhana dhania Wakuu. Mbeya refa katoa Kadi nyekundu na Penati, mlitaka atoe Wachezaji wangapi wa Mbeya City ili mshinde?
 
Kama we si mwanasoka,subiri tukianza kujadili karata tukuulize nini maana ya mtoto wa kiume kuolewa kwenye karata
Kabla ya yote timu inayokamia ndio inakuwa inafanyaje? Kukamia ndio nini?
 
Aisee hawa jamaa wanatumizia wachezaji kwa mipango yao ya kucheza rafu ili kuwaridhisha waliowapa mchongo..ebu fikiria match ya leo na mtibwa tunawakosa wachezaji wawili muhimu (kibu na mkude)
 
Sasa nyie Makolo mmevunjwa miguu na Timu gani...?
Sema hamna Mpira na sio kukamiwa au kuvunjwa miguu,, kama vp na nyie si muvunje pia.

Tushawahonga hela [emoji383] tayari Mtibwa Sugar na kazi mnayo Leo hii dadeq
 
Aisee hawa jamaa wanatumizia wachezaji kwa mipango yao ya kucheza rafu ili kuwaridhisha waliowapa mchongo..ebu fikiria match ya leo na mtibwa tunawakosa wachezaji wawili muhimu (kibu na mkude)
Kwani nyie hamna miguu ya kuwaumiza pia... Leo kitombo kipo palepale dadeq
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…