Timu ya Geita Gold, imetwaa ubingwa wa ligi daraja la kwanza

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
GEITA GOLD MABINGWA WA LIGI SOKA DARAJA LA KWANZA...
Klabu ya Geita Gold ya mkoani Geita imefanikiwa kuutwaa ubingwa wa ligi soka daraja la kwanza Tanzania bara baada ya kuichapa Mbeya Kwanza bao 1-0.

Mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar Es Salaam haukuwa mwepesi kwa timu zote kwani hadi dakika 90 zinahitimika timu hizo zilikuwa zimetoshana nguvu kwa sare ya kutofungana.

Geita iliyoshiriki ligi daraja la kwanza toka kundi B ilipata goli hilo na la pekee katika kipindi cha kwanza cha dakika 30 za nyongeza.

Mbeya Kwanza ilikuwa imepigiwa chapuo ya kuutwaa ubingwa wa ligi soka daraja la kwanza lakini walishindwa kufua dafu mbele ya Geita Gold iliyojipanga vyema kwa ajili ya mchezo huo.

Timu zote mbili zimepata tiketi ya Moja kwa Moja ya kushiriki ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao.
 
Wajipange, Ligi kuu pa Moto, wasajili vizuri ili yasiwakute Kama anavyoteseka Ihefu fc.
 
Ligi kuu watachezea uwanja wa Nyankumbu Girls? Au watatafuta uwanja wenye ubora zaidi?

Nauliza hivyo maana mechi zao nyingi walikuwa wanachezea kwenye uwanja wa Nyankumbu Girls Sec School.
 
Ligi kuu watachezea uwanja wa Nyankumbu Girls? Au watatafuta uwanja wenye ubora zaidi?

Nauliza hivyo maana mechi zao nyingi walikuwa wanachezea kwenye uwanja wa Nyankumbu Girls Sec School.
Kama unafaa kwa matumizi ya ligi kuu watatumia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…