Kwa Kukusaidia tu hakuna Timu ambayo inaongoza kwa Kufanya Vurugu, Hujuma, Hila na Vitimbi iwapo Kwake ( Kwao ) kama Biashara United FC.
Na bahati nzuri ni Timu ya Mkoa wangu ( tena wa Kiasili kabisa ) tu ila imeshalalamikiwa na karibia kila Timu inayoenda Kucheza pale Kwao Karume Stadium.
Ukiona hadi Makocha Marafiki zangu ambao ni Wapole na Wastaarabu mno Kitabia akina Zuberi Katwila na Salvatory Edward wamewalalamikia Biashara United FC pamoja na Mashabiki wake wawapo Kwao Karume Stadium Mkoani Mara ( Musoma ) jua ni kweli na kuna tatizo Kubwa.
Kulalamika Kwao leo ni Kuzuga tu na kutaka Kutengeneza Mzani ( balance ) kuwa hata Wao pia wanaonewa kwakuwa wameshahidi kuna Kikao cha Kamati ya Nidhamu cha TFF kitakaa na kuna Adhabu Kali inaenda Kuwaangukia Biashara United FC ya Mkoani Mara ( Musoma )
Na kama kweli leo Polisi FC nao Wametembeza Kichapo Kwao Biashara United FC na Shabiki zao nawapongeza sana kwani huenda sasa na Wao ( Biashara United FC ) wakajitathmini na wakabadilika upesi. Mbona wanacheza Mpira mzuri sana tu hawa ' Mapoti ' zangu Biashara United FC sasa hizi Fujo zao ( hasa za nje ya Uwanja ) huwa ni za nini?