Timu ya Taifa ya Riadha kutuwakilisha All African Games, Ghana

Melubo Letema

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2020
Posts
416
Reaction score
414
Timu ya Taifa ya Riadha wameondoka leo na kuagwa na Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania Silas Lucas Isangi na Kaimu katibu mkuu wa RT Wakili Jackson Ndaweka katika uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro.

Wanariadha hao 8 wakiwemo wa Mbio za Uwanjani, Mbio ndefu na Mrusha mkuki, wameondoka kwenda Accra , Ghana kushiriki mashindano ya Afrika “All African Games” ambayo yanafanyika huko na yalianza toka tarehe 8 na yataendelea hadi tarehe 23 Machi 2024.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…