Timu za Afrika zinapaswa zijifunze kutoka Morocco

zandrano

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2017
Posts
7,893
Reaction score
8,816
Baada ya timu ya Morocco kutolewa Jana na Ufaransa lakini ni ukweli usiopingika kuwa timu ya Morocco imeithibitishia Dunia kuwa haikutinga fainali kwa kubahatisha.

Lakini pia wameithibitishia Dunia kuwa hawakwenda kushiriki bali walikwenda kupambana.

Ahsante Morocco kwa kupambana kufa na kupona, hakika wanastahili pongezi nyingi sana kwa mchezo mzuri walio unonyesha dhidi ya Ufaransa, pamoja na kutolewa lakini wameithibitishia dunia kuwa hawakufika nusu fainali kwa bahati bali ni kwa bidii na maarifa na uzalendo wa hali ya juu.

Pongezi kwao kwa kuliwakilisha bara la Afrika kikamilifu na kufikia rekodi kuwa timu ya kwanza kutoka Afrika kifika nusu fainali kombe la dunia 2022.

Timu za Afrika na haswa Timu yetu ya Taifa Tanzania ianze maandalizi sasa ya kwenda kushindana kombe la dunia mwaka 2026 huko Kanada, inawezekana endapo tu tutaamua.
 
Hivi muambiwe Mara ngapi Morocco ni Waarabu ndio mtaelewa? Angalau ukisema imewakilisha waislamu utaeleweka.

Ufaransa imeingia Fainali lakini haiwakilishi Ulaya, inapigania Ufaransa, na hata wale watu weusi kwenye timu ya Ufaransa wanapigania Taifa lao la Ufaransa.

Acheni huu upuuzi Mara moja.
 
Acha ubaguzi wewe.
 
J2 nitabet hapa nawaza nabet team ipi? Argentina? Mmh embu mseme chochote hela yangu isije liwa bure
 
Matola acha mawazo ya wahuni mtaaani UBAGUZU WA NINI? TENA PUNHUZA MAKASIRIKO TANZANIA NYIE BADO SANA MKUUU
 
Kuna bwana mdogo anaitwa ounahi, namuona mbali
 
Waafrika wa Tanzania tutaendelea kujifunza kwa Cameroun, Senegal na Ghana! ambao kwa nyakati tofauti walipambana vilivyo kwenye hayo mashindano, kiasi cha kubakia hatua chache tu kuingia nusu fainali.

Na siyo kwa nchi ya Kiarabu kama Morocco! Nchi za Kiarabu na Kiislam kama Iran, Qatar, Saudi Arabia, Misri, Tunisia, Algeria, nk. Ndiyo zina cha kujifunza kutoka kwao.
 
Maumivu kwa waarabu na waislam siyo kwa waafrika, nitasimama tena na crotia kwenye tatu bora.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…