Timu za Congo DRC Klabu Bingwa Afrika msimu huu hamna kitu

denooJ

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2020
Posts
18,509
Reaction score
68,228
Vita uji, TP Mazembe mtori, watu wanajinywea tu, wanatakiwa kutuliza vichwa wajenge upya vikosi vyao.

Vita kupata draw away kwa Al Ahly kumbe ilikuwa ni bahati tu, walitakiwa kufa sio chini ya goli nne ni vile tu washambuliaji wa Ahly hawakuwa makini, leo Vita katandikwa nyumbani kwake na muarabu 3-0.

Hao Mazembe nao mbele ya Mamelodi Sundowns hawana chao, wanahitaji muujiza kushinda away kwa wale wasauz wanaopiga mpira kama hawana akili nzuri, nionavyo viwango vya hizi timu mbili za Congo vimeanza kushuka.
 
Kuna mdau alishasema humu kwamba,msimu huu hawajasajili, As Vita wana ukarabati mkubwa wa uwanja wao,vilevile waliuza sana wachazaji wao. Tp Mazembe nao wana project kubwa pia msinu huu wamepromote wachezaji vijana ila msimu ujao watakuwa moto.
 
Kuna mdau alishasema humu kwamba,msimu huu hawajasajili, As Vita wana ukarabati mkubwa wa uwanja wao,vilevile waliuza sana wachazaji wao. Tp Mazembe nao wana project kubwa pia msinu huu wamepromote wachezaji vijana ila msimu ujao watakuwa moto.
Nilisikia mahojiano fulani kutoka Congo kabla ya mechi hii bt nimesahau chanzo ila nakumbuka fact...ni kwamba kwa TP Mazembe Katumbi ameshusha budget ya timu kutoka milioni 10 kwa wiki kufikia milioni 5...pia wamekuwa wakisajili wachezaji ambao ni average hata wakutoka nje ya nchi na hivyo timu kushuka kiuwezo.
 
Hapa kuna neno, nikimkumbuka yule wa Mbeya City jina nimelisahau kidogo, na Singano naona kuna point hapo.
 
Kuna mdau alishasema humu kwamba,msimu huu hawajasajili, As Vita wana ukarabati mkubwa wa uwanja wao,vilevile waliuza sana wachazaji wao. Tp Mazembe nao wana project kubwa pia msinu huu wamepromote wachezaji vijana ila msimu ujao watakuwa moto.
Ni kweli lkn sio sababu sana,cz hao al ahly pia wana pjrct ya viwanja vya michezo tena hicho kituo hadhi ya Olympic

Hizo timu zimeuza wachezaji wazuri wamenunua underground ,mfn Mazembe toka wauze, Ben malango,Jackson muleka,Meshack Elia hawajanunua mchezaji mzuri zaidi ,ya baleke,dje dje ,beya
 
Sawa sawa budget imeshuka imesajiri wachezaji wa kawaida Sana, djedje,baleke,tshibangu,beya ,kifupi lescobeaux /Mazembe na black dolphins/Vclubien hawana timu nzuri msimu huu

Katumbi kapunguza budget
Gen Tango four Siku hz hayuko na Vclubien km zamani ,timu iko kwa Madame
 
Kweli wasingeweza kusajili wachezaji kiwango cha Singano na Atupele! kwa namna ilivyokuwa TP Mazembe
 

Al ahly na Wydad Casablanca is my favourite team. Mmoja wao lazima abebe kombe hili, mnyama i know that hana chake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…