Timu za Tanzania hazitofika mbali Kimataifa

Timu za Tanzania hazitofika mbali Kimataifa

Mchochezi

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2012
Posts
10,962
Reaction score
7,830
Azam Fc kashinda 1-0 nyumbani lakini alizidiwa muda mwingi wa mchezo, Goli lenyewe walilopata ni la Offside. Jana Yanga nae akiwa nyumbani alitoa suluhu 1-1 dhidi ya Zanaco huku wakicheza katika kiwango cha kawaida sana.

Kwa mwenendo huu nadiriki kusema kwamba timu za Tanzania hazitofika mbali na timu zote Yanga na Azam zitaenda kutolewa kwenye mechi za marudiano.

wewe mdau nini mtazamo wako?
 
Mimi ni mshabiki wa Yanga baada ya kuwaona zanaco ni wazi kuwa kule hatutaweza kushinda kuna goli 3 pale naziona za kufungwa
 
Game bado ziko wazi. Timu zinahitaji ushindi wowote ugenini. Natmaini walimu wamejifunza kitu. na Azam wana nafasi zaidi kwani wana claen sheet....
 
AZAM haitotolewa kirahisi,kwani mpira wamecheza sana!

nilikuwa nafikiria tu kwa kasi ya MBABANE SWALLOWS, YANGA WANGEKULA NGAPI LEO?

AZAM FC,ndiyo club itayokuja kuitoa Tanzania kimasomaso kwenye michuano ya kimataifa!

Niamini mimi,IPO SIKU TU!
 
Viongozi wabovu wasio na mikakati wakiongozwa na baba yao Jamal Malinzi ndio wametufikisha huku
 
Tatizo la Yanga imekumbatia sana Uccm na ndo maana kilabuni kwao kuna bendera za ccm .wacha wakong'otwe huko Zambia.
 
naiwe hivyo tu maana timu zetu mpira bado wanasajiri kimazoea
 
Tukitolewa mabingwa tunacheza shirikisho...mikia fc jazeni uwanja tupige hela na nasikia mnataka wachezaji wa zanaco...tunawapa exposure kubwa
 
Tatizo la Yanga imekumbatia sana Uccm na ndo maana kilabuni kwao kuna bendera za ccm .wacha wakong'otwe huko Zambia.
Kwa hiyo wakiamua kuikumbatia CHADEMA mpira wa Yanga utabadilika ghafla ?

Unajua kwamba Mbowe ni Yanga wa kutupwa? Unajua marehemu mzee Sitta alikuwa Simba wa kutupwa? Je Rage yupo chama gani?

Ondoa issue za mpira kwenye siasa, utaumbuka mchana kweupe
 
Yanga ilikuwepo tangu 1935, CCM ni ya mwaka 1977 nivitu viwili tofauti. Usilete siasa kwenye mpira.
 
Kwa mimi naona Azam walicheza vizuri japo walizidiwa.Hawa wanaweza kusonga mbele kama wakiwahi kufunga ugenini.Yanga kwakweli ni kama imeshatolewa maana ina wachezaji wazito sana.Hata wakienda shirikisho wakikutana na timu yenye kiwango kama swallows basi wanapigwa nje ndani.Kila mara huwa nasema ligi yetu inauwawa na marefa wabovu ambao wao hutaka tu timu kubwa zishinde.Azam haikufunga kwa offside kama unajua mpira hili liko wazi offside ilishavunjwa.
 
Mkombozi wenu anakuja.. Simba sports club msiwe na hofu Watanzania
 
Tatizo la Yanga imekumbatia sana Uccm na ndo maana kilabuni kwao kuna bendera za ccm .wacha wakong'otwe huko Zambia.
Huo ndio ukweli kabisaaaaa! Hata mbinu za ushindi wanaigana!
 
Yanga imeshatokewa.hawezi kushinda kuke Zambia.Hii yanga imekuwa dhaifu sana.
 
Mwenyekiti ambaye ni mfadhili yuko lupango unataka wachezaji wafanye muujiza?
 
Back
Top Bottom