Tishio la kuadimika samaki Ziwa Victoria wananchi wamkumbuka Luhaga Mpina

Tishio la kuadimika samaki Ziwa Victoria wananchi wamkumbuka Luhaga Mpina

SULEIMAN ABEID

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2013
Posts
390
Reaction score
385
Taarifa za kuadimika kwa kiasi kikubwa cha Samaki katika Ziwa Victoria zimewashitua wakazi wa Kanda ya Ziwa Victoria na wengi washauri kurejewa kwa utaratibu uliotumiwa na aliyewahi kuwa Waziri Mifugo na Uvuvi nchini, Luhaga Mpina.

Soma kwa kirefu tishio hilo la kuadimika kwa samaki katika Ziwa Victoria.

View attachment CamScanner 04-19-2022 17.42.pdf

uvuvi.JPG
 
Hali inatisha Kanda ya Ziwa

Mwaka mmoja wa uvuvi haramu watikisa uchumi, watishia kuliua Ziwa Victoria

Makokoro, nyavu hatari kutoka Uganda, Burundi vyaingizwa kwa fujo

*TAFIRI wakiri, watega nyavu kwa saa mbili ziwani na kuambulia samaki mmoja

Na Alex Kazenga

Amini usiamini, samaki wanakwisha ndani ya Ziwa Victoria, hali inayotishia afya, uchumi na hata amani kwa mamilioni ya wananchi wanaolizunguka ziwa hilo; JAMHURI linaripoti

Tishio hilo linatokana na uvuvi haramu ulioshamiri kwa takriban mwaka mmoja sasa, ukifanyika mchana na usiku bila hofu ya kuwapo kwa serikali

Akizungumza na JAMHURI, mkazi mmoja wa Kanda ya Ziwa anasema: “Hali hii (uvuvi haramu bila hofu) imeanza tangu mwaka jana.

Si hapa tu, ipo na inaonekana wazi katika wilaya za Muleba, Sengerema na Ukerewe.”

Ni aina hii ya uvuvi ndio unaozuiwa kisheria.

Ndio umesababisha kuadimika kwa samaki wa kila aina ndani ya Ziwa Victoria

Uvuvi ndio shughuli kubwa ya kiuchumi kwa Kanda ya Ziwa na kudorora kwake kunazua hofu kwa wengi.

JAMHURI linafahamu kwamba kwa takriban miezi mitatu sasa samaki maarufu aina ya sato na sangara wameadimika ziwani na kusababisha ugumu wa maisha kwa watu waliojiajiri au kuajiriwa katika sekta ya uvuvi

Chanzo Gazeti la Jamhuri Aprili 19, 2022
 
Wavuvi haram wadhibitiwe haraka,

Ndio samaki pekee waliobakia nchini kwa ladha ya kipekee
 
Taarifa za kuadimika kwa kiasi kikubwa cha Samaki katika Ziwa Victoria zimewashitua wakazi wa Kanda ya Ziwa Victoria na wengi washauri kurejewa kwa utaratibu uliotumiwa na aliyewahi kuwa Waziri Mifugo na Uvuvi nchini, Luhaga Mpina...
Aisee!
Hatari..
 
Taarifa za kuadimika kwa kiasi kikubwa cha Samaki katika Ziwa Victoria zimewashitua wakazi wa Kanda ya Ziwa Victoria na wengi washauri kurejewa kwa utaratibu uliotumiwa na aliyewahi kuwa Waziri Mifugo na Uvuvi nchini, Luhaga Mpina.

Soma kwa kirefu tishio hilo la kuadimika kwa samaki katika Ziwa Victoria.

View attachment 2194630

Yaani hadi Mpina ana Chawa wake !

Haya rudisheni vipimo vya rula

FB_IMG_1648499814063.jpg
 
Taarifa za kuadimika kwa kiasi kikubwa cha Samaki katika Ziwa Victoria zimewashitua wakazi wa Kanda ya Ziwa Victoria na wengi washauri kurejewa kwa utaratibu uliotumiwa na aliyewahi kuwa Waziri Mifugo na Uvuvi nchini, Luhaga Mpina.

Soma kwa kirefu tishio hilo la kuadimika kwa samaki katika Ziwa Victoria.

View attachment 2194630

Mmeamua kutisha watu
 
Ni ukweli usiopingika kuna upungufu mkubwa sana wa samaki katika Ziwa Victoria na hasa sangara. Upungufu huu umetokea na hasa siku za karibuni. Ikibidi Serikali ichukue hatua za haraka na ielezee wananchi wanaozunguka Ziwa Victoria sababu ya upungufu huu wa kutisha.
 
Acha wapungue tu tunapenda na kuendekeza anasa sana kwa kula Samaki wakati nyama ipo bwerere tu.
 
KWAHIYO KWAKO WEWE KULA SAMAKI NI ANASA??
Siyo kwangu ni kwenu. Mnapendapenda kuendekeza anasa. Kwanini? Huo mda wa kula samaki mnautoa wapi? Huo uthubutu tu mnautoa wapi? Wakat hali ya uchumi ni mbaya mfumuko wa bei.

Jitathmini jombaaa!

Sauh'waaa?
 
Wavuvi haram wadhibitiwe haraka,

Ndio samaki pekee waliobakia nchini kwa ladha ya kipekee
Walipozuiwa kuvua samaki wadogo
Mkapimiwa kwa rula watu walilalamika,sahv samaki wameadimika mnashangaaaa?

Eh

Ova
 
Hao watakuwa Sukuma Gang tu.

Waende wakazikwe na marehemu wao Chatoo kama wanampenda sana.

Sisi tupo busy kulamba asali, wasitusumbue.
 
Back
Top Bottom