Tishio la ugaidi Mandera: Polisi wakaa kwenye tahadhari kubwa

Tishio la ugaidi Mandera: Polisi wakaa kwenye tahadhari kubwa

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Polisi katika Kaunti ya Mandera, Kaskazini Mashariki mwa Kenya wapo katika hali ya tahadhari, baada ya kuripotiwa kuwa washukiwa 20 wa Al Shabab kutoka nchini Somalia walikuwa wameonekana katika eneo hilo.

Ripoti zinasema kuwa, magaidi hao walionekana katika maeneo ya Bale-Ilman Mala na Kutulo Ijumaa iliyopita.

Haya yanajiri wakati huu miili ya maafisa 11 wa polisi waliouawa Jumamosi iliyopita huko Garissa wakati gari lao lilipokanyaga kilipuzi kilichotegwa ardhini ikirejeshwa jijini Nairobi.

Kenya imeendelea kuwa kwenye vita na kundi la Al Shabab tangu mwaka 2011, ilipotuma wanajeshi wake nchini humo.
 
Al shabab sio magaidi, tengua hiyo Kali. Kikao cha UN council Sept 2019 kilibainisha hivyo. Hiyo taharuki ni no honor among thieves wamepiga dili mahali wameshidwa kugawana
 
Al shabab wanauwa wanavyotaka
Hivi wakenya mnapata faida gani na hii vita?
 
Back
Top Bottom