Tisiogope fursa za mtandaoni

Qzam

Member
Joined
Mar 5, 2023
Posts
26
Reaction score
23
Hongereni kwa kazi.

Kumekuwa na nyuzi nyingi za maulizo na nyingine za kuhamasishana juu ya biashara na njia anuai za kuingiza kipato. Uwepo wa jambo hill unaashiria kiu lakini namba ya kuikidhi hiyo kiu ndo inakuwa ngumu, mashaka ni mengi.

Jambo moja tukubali kuwa tutake tusitake mabadiliko yamekuja na hatuwezi yazuia,ni ama twende nayo au tuachwe.

Biashara zote na kazi zote zinahamia mtandaoni. Wasomi wanaongezeka na ajira zinapungua, Automation au artificial intelligence inaondoa nafasi za kazi kwa kasi kubwa.

Ni lazima tukubali kubadili fikra zetu tuache kuishi kwa mazoea tuwekeze kwenye fursa zilizopo kwenye kijiji dunia.

Njia za uwekezaji au kazi za mtandaoni ni nyingi mno na zinazidi kuzaliwa kila uchao. Kwahiyo badala ya kulalamika tuchukue hatua.

Kwa wenye mtaji ziko fursa za uwekezaji katika makampuni ya uhakika unakoweza pata 14% na 28% kwa mwezi. Kama una m3 ukipata faida ya 28% kwa mwezi, huishi bila jasho mjini?

Tubadilike watanzania.


Nawasilisha.
 
Nyingi ni scammer
 
Hapo kwenye uwekezaji hapo ndio pabaya kwanza tujifunze kwanza tufahama watanzania bado tupo nyuma kwa mambo mengi mno sasa wajanja wanatumia fursa hiyo kutuumiza..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…