TLS [2024]na Mawakili wapoteza mvuto kwa Jamii

TLS [2024]na Mawakili wapoteza mvuto kwa Jamii

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776
TLS-Chama cha Mawakili wa Tanganyika , -Zanzibar wana Chakwao, kimekuwa kikipoteza mvuto na haiba mbele ya jamii kila uchao.
Sababu zinazosemekana kupoteza mvuto kwa jamii:
  1. baada ya Uongozi wa Fatuma Karume na Tundu Lissu kumalizika , TLS iliuawa, Edward Hosea na Sungusia ni kama walikuwa Mamluki waliokuja kukiua hicho chama cha Wanasheria, sijui kwanini waliamua kukiua.​
  2. TLS kukaa kimya uminyaji wa haki za binadamu, mawakili kupewa kesi na kuruhusu mahakam, vyama na mashirika kutoa huduma za kisheria tena kwa kuweka matangazo mitandaoni na kwenye Tv huku mawakili wakinyimwa, hiyo mtu anaweka tangazo pale salender bridge kuwa anasajili kampuni kwa laki tatu na wakili anasajili kwa 1.5 m , mteja aende kwa nani?​
  3. Mawakili kuwekwa lupango kama wauza magendo bila sababu na wawekaji kutowajibishwa, na wakili akionekana anaenda kwenye mahojiano huwa wanacheleweshwa ili wakate yamaa na kumuacha mteja.​
  4. Ada za TLS kuwa juu na tuhuma za rushwa ambazo kwenye mikutano ya mawakili kutopatiwa majibu na wanao hoji kuonekana wametumwa na chama cha siasa.​
  5. DAFT- mawakili wanakufa na ugonjwa, njaa ila hakuna mkono wa TLS ila akifa na kuzikwa ndugu wanapewa milioni 6.​
  6. Uchaguzi wa TLS president kukosa mvuto kwa 95% na sasa huenda ukawa kama wa chama cha waendesha mikokoteni.
  7. Kuamishwa kwa mikutano ya TLS toka Arusha kwenda DODOMA MWAKA 2024. Wasichojua TLs ni kuwa watu wengi , wanakwenda Arusha as adventure, wanakwenda kutalii na kupumzika kwenye hoteli za kitalii na kutembele mbuga za wanyama, kula mbuzi kwa mromboo na mambo mengine mengi. Mawakili wa serikali ambao wameanzisha chama chao kipindi cha JIWE ili TLS ikose nguvu hata wao japo si wanachama wa TLS lakini huwa wanakwenda mikutano ya TLS maana wanaipenda TLS KULIKO CHAMA CHAO .Huko Dodoma hawatakwenda, kutadoda.
  8. Kamati ya maadili ya mawakili imekuwa kama kisu kwa mawakili, yani huko badala member atetewe wao ndio kwanza wanamfungia, mfano Shangazi Fetty na wengine wengi. Kila chama, kuanzia cha majaji, mahakimu, walimu, madereva , umoja wa madereva bodaboda, wanatetea haki zao na wana wivu kweli na mwanachama wao ila TLS wao wanaangamiza wanachama wao!
Bali sasa Ujio wa Boniface Mwabukusi kwenye uongozi wa Chama hicho ni sawa na Ufufuo na Uzima, japo huenda akaenguliwa, kuna siasa nyingi .
 
Nimeona Jana ilibidi wasogeze mda mbele ili kupata wagombea
Nikajiuliza ni hii hii tls au!? Nikajua something is wrong in that wakili house
 
Hv Mwabukusi anagombea kama ni kweli Afadhali sana.

Jambo la pili kitu ambacho TLS hawaelewi ni kwamba mawakili wamekuwa wengi wananyang'anyana kesi chache zilizopo. (Uwakili sio dili siku hizi ni ubangaizaji tu)

Wapunguze ada za uwakili wanakuwa kama hawajui kanuni za demand na sapply

mawakili wengi kazi chache wao wanachoangalia ni michango yao tu.

Jambo la tatu. Kama hujahuisha leseni ya uwakili wanakuchorea haruhusiwi huko mtandaoni ukishachora hivyo mawakili wanakosa wateja ambao kimsingi wanapatikana kwa manati

Alafu ukija kupata fee zao unawalipa hata kipindi ambacho walikuwa wamekuchorea huruhusiwi waache huu upuuzi maramoja.

Otherwise chama kinazidi kupoteza mvuto na wamakili wengi wanazidi ku default

Alafu kitu kingine ni nani aliyependekeza mawakili mikutano yao iwe inafanyika Dodoma!!??

Hili swala halipaswi kupelekwa kidikteta linapaswa liamuliwe kwenye kamati na kura zipigwe na wanachama ikibidi.

TLS sio chama na serekali kiende huko Dodoma that is a proffession body alaa
 
TLS ya Sungusia mwanaharakati uchwara ni kama lile Jukwaa la Wahariri la Balile, yaani watu wakishaamua kuachana na fani zao na kutimiza wajibu na kuamua kuwa chawa uje ndio basi tena hiyo imeenda , mara mia nne hata ya Hosea, hicho kichama wakisimama watu kama kina Kibatala unaona hadi serikali inaweka mkono wake kuhakikisha hawatoboi, ili makapi yao yapite wakae kimyaaa kana kwamba hakuna kitu kinachoendelea huko TZ. SHAME.
 
Mimi namfahamu wakili Mwabukusi na Wakili TL, hao bado wana mvuto kwa jamii
 
Back
Top Bottom