TLS yamtaka Rais Samia kuunda Tume ya kuchunguza Polisi kuhusu utekaji wanaohusishwa nao. Yataka ripoti za uchunguzi kutolewa

TLS yamtaka Rais Samia kuunda Tume ya kuchunguza Polisi kuhusu utekaji wanaohusishwa nao. Yataka ripoti za uchunguzi kutolewa

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimemshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda tume maalumu ya kuchunguza ushiriki wa Jeshi la Polisi kwenye masuala ya utekaji na utesaji kwa kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likituhumiwa kushiriki katika vitendo hivyo.

Kupitia taarifa iliyotolewa siku ya Ijumaa Agosti 09, 2024 na Baraza la Uongozi la TLS na kusainiwa na Rais wake Boniface Mwabukusi, TLS imeeleza kusikitishwa na kulaani vitendo vya kukamatwa, kutekwa na kuteswa kiholela kwa wananchi kunakoendelea nchini bila ya vyombo husika vya dola “kuwajibika ipasavyo”.

“Mara kwa mara Jeshi la Polisi limekuwa likikanusha kutokea kwa matukio hayo lakini baadaye inakuja kubainika kwamba matukio hayo ni ya kweli. Mara nyingine Jeshi la Polisi limekuwa likiwakamata raia wema wanaotoa taarifa hizo kwa kile kinachosemekana kusambaza taarifa za uongo badala ya kufanyia kazi taarifa hizo kwa mujibu wa Katiba na Sheria”, ameeleza Mwabukusi.

TLS imeeleza pia kuwa hakuna taarifa kamili ya uchunguzi wa tukio hata moja ambayo imewahi kutolewa kwa umma juu ya hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi juu ya watuhumiwa wa matukio hayo na kwamba hali hiyo imeendelea kutia hofu wananchi juu ya usalama wao na mashaka juu ya uwezo wa Jeshi la Polisi kuchunguza na kuchukua hatua stahiki kwa wahusika wa matukio hayo.

Katika kujaribu kutatua changamoto za matukio hayo nchini, TLS pia imependekeza kuundwa kwa chombo maalumu cha kudumu cha kuangalia utendaji wa vyombo vya dola (oversight body) ili kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria huku ikilitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi yake kwa weledi ili kuhakikisha usalama na ulinzi wa wananchi na mali zao unaimarika.

Katika taarifa ya TLS kumeorodheshwa matukio mbalimbali ya utekaji yaliyoripotiwa na vyombo vya habari na watu mbalimbali likiwamo tukio la karibuni la Kombo Mbwana aliyetekwa nyumbani kwake Handeni Tanga na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 15 Juni 2024, baadaye polisi walikanusha kuhusika na kufungua jalada la uchunguzi, na Siku 29 baadaye polisi walikiri kuhusika na kumshikilia kwa hizo siku zote.
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimemshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda tume maalumu ya kuchunguza ushiriki wa Jeshi la Polisi kwenye masuala ya utekaji na utesaji kwa kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likituhumiwa kushiriki katika vitendo hivyo.

Kupitia taarifa iliyotolewa siku ya Ijumaa Agosti 09, 2024 na Baraza la Uongozi la TLS na kusainiwa na Rais wake Boniface Mwabukusi, TLS imeeleza kusikitishwa na kulaani vitendo vya kukamatwa, kutekwa na kuteswa kiholela kwa wananchi kunakoendelea nchini bila ya vyombo husika vya dola “kuwajibika ipasavyo”.

“Mara kwa mara Jeshi la Polisi limekuwa likikanusha kutokea kwa matukio hayo lakini baadaye inakuja kubainika kwamba matukio hayo ni ya kweli. Mara nyingine Jeshi la Polisi limekuwa likiwakamata raia wema wanaotoa taarifa hizo kwa kile kinachosemekana kusambaza taarifa za uongo badala ya kufanyia kazi taarifa hizo kwa mujibu wa Katiba na Sheria”, ameeleza Mwabukusi.

TLS imeeleza pia kuwa hakuna taarifa kamili ya uchunguzi wa tukio hata moja ambayo imewahi kutolewa kwa umma juu ya hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi juu ya watuhumiwa wa matukio hayo na kwamba hali hiyo imeendelea kutia hofu wananchi juu ya usalama wao na mashaka juu ya uwezo wa Jeshi la Polisi kuchunguza na kuchukua hatua stahiki kwa wahusika wa matukio hayo.

Katika kujaribu kutatua changamoto za matukio hayo nchini, TLS pia imependekeza kuundwa kwa chombo maalumu cha kudumu cha kuangalia utendaji wa vyombo vya dola (oversight body) ili kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria huku ikilitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi yake kwa weledi ili kuhakikisha usalama na ulinzi wa wananchi na mali zao unaimarika.

Katika taarifa ya TLS kumeorodheshwa matukio mbalimbali ya utekaji yaliyoripotiwa na vyombo vya habari na watu mbalimbali likiwamo tukio la karibuni la Kombo Mbwana aliyetekwa nyumbani kwake Handeni Tanga na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 15 Juni 2024, baadaye polisi walikanusha kuhusika na kufungua jalada la uchunguzi, na Siku 29 baadaye polisi walikiri kuhusika na kumshikilia kwa hizo siku zote.
Ushauri mzuri ni matamanio yangu kuwa utafanyiwa kazi badala ya kutuhumiana kireja reja kama ilivyo sasa
 
Hapa sasa ndio penyewe, na wale wengine wa haki za binadamu wapige msumari hapo, upande mwingine wananchi nasisi tuache kulala tulete shinikizo.
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimemshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda tume maalumu ya kuchunguza ushiriki wa Jeshi la Polisi kwenye masuala ya utekaji na utesaji kwa kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likituhumiwa kushiriki katika vitendo hivyo.

Kupitia taarifa iliyotolewa siku ya Ijumaa Agosti 09, 2024 na Baraza la Uongozi la TLS na kusainiwa na Rais wake Boniface Mwabukusi, TLS imeeleza kusikitishwa na kulaani vitendo vya kukamatwa, kutekwa na kuteswa kiholela kwa wananchi kunakoendelea nchini bila ya vyombo husika vya dola “kuwajibika ipasavyo”.

“Mara kwa mara Jeshi la Polisi limekuwa likikanusha kutokea kwa matukio hayo lakini baadaye inakuja kubainika kwamba matukio hayo ni ya kweli. Mara nyingine Jeshi la Polisi limekuwa likiwakamata raia wema wanaotoa taarifa hizo kwa kile kinachosemekana kusambaza taarifa za uongo badala ya kufanyia kazi taarifa hizo kwa mujibu wa Katiba na Sheria”, ameeleza Mwabukusi.

TLS imeeleza pia kuwa hakuna taarifa kamili ya uchunguzi wa tukio hata moja ambayo imewahi kutolewa kwa umma juu ya hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi juu ya watuhumiwa wa matukio hayo na kwamba hali hiyo imeendelea kutia hofu wananchi juu ya usalama wao na mashaka juu ya uwezo wa Jeshi la Polisi kuchunguza na kuchukua hatua stahiki kwa wahusika wa matukio hayo.

Katika kujaribu kutatua changamoto za matukio hayo nchini, TLS pia imependekeza kuundwa kwa chombo maalumu cha kudumu cha kuangalia utendaji wa vyombo vya dola (oversight body) ili kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria huku ikilitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi yake kwa weledi ili kuhakikisha usalama na ulinzi wa wananchi na mali zao unaimarika.

Katika taarifa ya TLS kumeorodheshwa matukio mbalimbali ya utekaji yaliyoripotiwa na vyombo vya habari na watu mbalimbali likiwamo tukio la karibuni la Kombo Mbwana aliyetekwa nyumbani kwake Handeni Tanga na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 15 Juni 2024, baadaye polisi walikanusha kuhusika na kufungua jalada la uchunguzi, na Siku 29 baadaye polisi walikiri kuhusika na kumshikilia kwa hizo siku zote.
Watanzania tutoe ushirikiano wa dhati kwa wapinga Uhalifu Kama Hawa. Tuwape ushirikiano ili kukomesha kabisa vitendo viovu vya namna hii vya kuteka Watu. Uhalifu wa namna hiyo KAMWE haukubaliki
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimemshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda tume maalumu ya kuchunguza ushiriki wa Jeshi la Polisi kwenye masuala ya utekaji na utesaji kwa kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likituhumiwa kushiriki katika vitendo hivyo.

Kupitia taarifa iliyotolewa siku ya Ijumaa Agosti 09, 2024 na Baraza la Uongozi la TLS na kusainiwa na Rais wake Boniface Mwabukusi, TLS imeeleza kusikitishwa na kulaani vitendo vya kukamatwa, kutekwa na kuteswa kiholela kwa wananchi kunakoendelea nchini bila ya vyombo husika vya dola “kuwajibika ipasavyo”.

“Mara kwa mara Jeshi la Polisi limekuwa likikanusha kutokea kwa matukio hayo lakini baadaye inakuja kubainika kwamba matukio hayo ni ya kweli. Mara nyingine Jeshi la Polisi limekuwa likiwakamata raia wema wanaotoa taarifa hizo kwa kile kinachosemekana kusambaza taarifa za uongo badala ya kufanyia kazi taarifa hizo kwa mujibu wa Katiba na Sheria”, ameeleza Mwabukusi.

TLS imeeleza pia kuwa hakuna taarifa kamili ya uchunguzi wa tukio hata moja ambayo imewahi kutolewa kwa umma juu ya hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi juu ya watuhumiwa wa matukio hayo na kwamba hali hiyo imeendelea kutia hofu wananchi juu ya usalama wao na mashaka juu ya uwezo wa Jeshi la Polisi kuchunguza na kuchukua hatua stahiki kwa wahusika wa matukio hayo.

Katika kujaribu kutatua changamoto za matukio hayo nchini, TLS pia imependekeza kuundwa kwa chombo maalumu cha kudumu cha kuangalia utendaji wa vyombo vya dola (oversight body) ili kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria huku ikilitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi yake kwa weledi ili kuhakikisha usalama na ulinzi wa wananchi na mali zao unaimarika.

Katika taarifa ya TLS kumeorodheshwa matukio mbalimbali ya utekaji yaliyoripotiwa na vyombo vya habari na watu mbalimbali likiwamo tukio la karibuni la Kombo Mbwana aliyetekwa nyumbani kwake Handeni Tanga na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 15 Juni 2024, baadaye polisi walikanusha kuhusika na kufungua jalada la uchunguzi, na Siku 29 baadaye polisi walikiri kuhusika na kumshikilia kwa hizo siku zote.
TLS, haya yote yana baraka za mamlaka ya juu ya uteuzi wao.
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimemshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda tume maalumu ya kuchunguza ushiriki wa Jeshi la Polisi kwenye masuala ya utekaji na utesaji kwa kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likituhumiwa kushiriki katika vitendo hivyo.

Kupitia taarifa iliyotolewa siku ya Ijumaa Agosti 09, 2024 na Baraza la Uongozi la TLS na kusainiwa na Rais wake Boniface Mwabukusi, TLS imeeleza kusikitishwa na kulaani vitendo vya kukamatwa, kutekwa na kuteswa kiholela kwa wananchi kunakoendelea nchini bila ya vyombo husika vya dola “kuwajibika ipasavyo”.

“Mara kwa mara Jeshi la Polisi limekuwa likikanusha kutokea kwa matukio hayo lakini baadaye inakuja kubainika kwamba matukio hayo ni ya kweli. Mara nyingine Jeshi la Polisi limekuwa likiwakamata raia wema wanaotoa taarifa hizo kwa kile kinachosemekana kusambaza taarifa za uongo badala ya kufanyia kazi taarifa hizo kwa mujibu wa Katiba na Sheria”, ameeleza Mwabukusi.

TLS imeeleza pia kuwa hakuna taarifa kamili ya uchunguzi wa tukio hata moja ambayo imewahi kutolewa kwa umma juu ya hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi juu ya watuhumiwa wa matukio hayo na kwamba hali hiyo imeendelea kutia hofu wananchi juu ya usalama wao na mashaka juu ya uwezo wa Jeshi la Polisi kuchunguza na kuchukua hatua stahiki kwa wahusika wa matukio hayo.

Katika kujaribu kutatua changamoto za matukio hayo nchini, TLS pia imependekeza kuundwa kwa chombo maalumu cha kudumu cha kuangalia utendaji wa vyombo vya dola (oversight body) ili kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria huku ikilitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi yake kwa weledi ili kuhakikisha usalama na ulinzi wa wananchi na mali zao unaimarika.

Katika taarifa ya TLS kumeorodheshwa matukio mbalimbali ya utekaji yaliyoripotiwa na vyombo vya habari na watu mbalimbali likiwamo tukio la karibuni la Kombo Mbwana aliyetekwa nyumbani kwake Handeni Tanga na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 15 Juni 2024, baadaye polisi walikanusha kuhusika na kufungua jalada la uchunguzi, na Siku 29 baadaye polisi walikiri kuhusika na kumshikilia kwa hizo siku zote.

Mwanzo mpya wa TLS ila wasiishie kwenye taarifa ila waendelee kushinikiza hadi upande wa pili uje na majibu sahihi na siyo ya kisiasa.
 
TLS ya Mwabukusi haitafanywa kuwa Tawi la Lumumba✊️✊️
 
Back
Top Bottom