TLS, yatoa orodha ya watu waliopotea na kutekwa na tamko juu ya ongezeko la vitendo vya utekaji na upoteaji wa watu nchini

TLS, yatoa orodha ya watu waliopotea na kutekwa na tamko juu ya ongezeko la vitendo vya utekaji na upoteaji wa watu nchini

Abdul Said Naumanga

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2024
Posts
673
Reaction score
1,318
Chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society - TLS) kikiongozwa na wakili Boniface A.K Mwabukusi kimetoa tamko zito lililoweka wazi hali ya kusikitisha inayolikumba taifa. Kwa mujibu wa tamko hilo, kumekuwa na ongezeko la matukio ya kutekwa, kupotea, na kuteswa kwa watu nchini Tanzania, huku vyombo vya dola vikishindwa kutoa ufafanuzi wa kuridhisha au kuchukua hatua stahiki dhidi ya vitendo hivi vya kikatili.

TLS imeeleza wasiwasi mkubwa kuhusu jinsi Jeshi la Polisi limekuwa likishughulikia matukio haya. Licha ya taarifa nyingi kutolewa kuhusu utekaji na utesaji, mara kwa mara vyombo hivi vimeonekana kukanusha madai haya, hata pale ambapo ushahidi wa kutosha umeibuka kuthibitisha ukweli wa matukio haya. Hali hii imeongeza hofu na wasiwasi miongoni mwa wananchi, ambao wanahisi kutokuwa salama katika nchi yao wenyewe.

Katika tamko hilo, TLS inakemea vikali vitendo vya utekaji na utesaji, ikieleza kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kama ilivyowekwa bayana katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mikataba ya kimataifa. TLS imeishauri serikali, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kuchukua hatua za haraka kuunda Tume Maalum itakayochunguza matukio haya na kubaini wahusika wa uhalifu huu.

Aidha, chama hicho kinapendekeza kuanzishwa kwa chombo maalum cha kudumu kitakachokuwa na jukumu la kusimamia na kuangalia utendaji wa vyombo vya dola, kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi. Kwa kufanya hivyo, TLS inaamini kuwa itaimarisha uadilifu wa vyombo vya dola na kurejesha imani ya wananchi kwa serikali yao.

Katika kiambatanisho cha tamko hilo, TLS imetoa orodha ya baadhi ya watu waliotekwa au kupotea kuanzia mwaka 2016 hadi 2024, ikiwa ni ushahidi wa dhahiri wa kuendelea kwa vitendo hivi vya kikatili. Baadhi ya watu hao walipatikana wakiwa wamejeruhiwa, huku wengine wakiwa hawajulikani walipo hadi sasa.

Kwa kuhitimisha, TLS inatoa wito kwa wananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari za ziada katika maisha yao ya kila siku, na kutoa taarifa kwa mamlaka husika endapo watahisi hatari yoyote. Huu ni wakati muhimu kwa Watanzania wote kusimama pamoja katika kupinga vitendo hivi vya ukiukwaji wa haki za binadamu na kudai uwajibikaji kutoka kwa viongozi.

Pia soma: Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

TAMKO 👇🏼
IMG_5683.jpeg
IMG_5684.jpeg

IMG_5685.jpeg

IMG_5686.jpeg

IMG_5687.jpeg

IMG_5688.jpeg
IMG_5689.jpeg

IMG_5690.jpeg

IMG_5691.jpeg

IMG_5692.jpeg

IMG_5693.jpeg

IMG_5694.jpeg

IMG_5695.jpeg

IMG_5696.jpeg

IMG_5697.jpeg

IMG_5698.jpeg

IMG_5699.jpeg


09 Agosti, 2024

TAARIFA KWA UMMA

ONGEZEKO LA VITENDO VYA UTEKAJI NA UPOTEAJI WA WATU NCHINI

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kinasikitishwa na kinalaani vitendo vya kukamatwa, kutekwa na kuteswa kiholela kwa wananchi kunakoendelea nchini bila ya vyombo husika vya dola kuwajibika ipasavyo.

Kumekuwepo na taarifa mbalimbali za watu kupotea katika mazingira tatanishi, kutekwa na kuteswa na baadae kuonekana huku baadhi yao wakiwa wamefariki na wengine wakiwa na majeraha makubwa katika miili yao. Tunasikitishwa pia na namna ambavyo vyombo vyetu vya dola hususani Jeshi la Polisi limekuwa likifanyia kazi taarifa hizo. Mara kwa mara Jeshi la Polisi limekuwa likikanusha kutokea kwa matukio hayo lakini baadae inakuja kubainika kwamba matukio hayo ni ya kweli. Mara nyingine Jeshi la Polisi limekuwa likiwakamata raia wema wanaotoa taarifa hizo kwa kile kinachosemekana kusambaza taarifa za uongo badala ya kufanyia kazi taarifa hizo kwa mujibu wa Katiba na Sheria zinazowapasa kufanya wajibu wao wa kulinda watu na mali zao.

TLS, kwa mamlaka iliyopewa kupitia kifungu cha 4 cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act, Cap. 307 R.E. 2002), inapenda kuvikumbusha vyombo vya dola hususan Jeshi la Polisi juu ya majukumu yake ya Kikatiba na Kisheria ya kulinda watu na mali zao. Matukio haya ya utekaji ni kinyume na Ibara ya 13 (6) (e) na 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; pamoja na Mikataba ya Kimataifa inayozungumzia Haki za Binadamu na inayozuia uteswaji wa watu kama vile Mkataba dhidi ya Mateso na Unyanyasaji au Adhabu Nyingine za Kikatili au Udhalilishaji (Convention against Torture and Other Cruel, Inhuman or Degrading Treatment or Punishment), Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu (Universal Declaration of Human Rights) na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (The International Covenant on Civil and Political Rights).

TLS inatambua na kuheshimu taarifa za Jeshi la Polisi zinatolewa zikitaarifu umma kwamba matukio hayo yamekuwa yanafanyiwa uchunguzi lakini tunasikitika kwamba hakuna taarifa kamili ya uchunguzi wa tukio hata moja ambayo imewahi kutolewa kwa umma juu ya hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi juu ya watuhumiwa wa matukio hayo. Hali hii inaendelea kutia hofu kwa wananachi juu ya usalama wao na mashaka juu ya uwezo wa Jeshi la Polisi kuchunguza na kuchukua hatua stahiki kwa wahusika wa matukio hayo.

Kupitia tamko hili, tunaambatanisha orodha ya baadhi ya watu ambao wananchi au/na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini vimewahi kutoa taarifa za kupotea au kutekwa kwao ambapo baadhi yao walipatikana na baadhi yao wakiwa na majeraha huku kukiwa na wengine ambao waliopotea katika mazingira tatanishi na hawajapatikana mpaka leo. Tunaamini kwamba Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya dola vitafanyia kazi na kuhakikisha watu hao wamepatikana na wahusika wote wa matukio haya wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo husika vya haki ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa.​

Wito wetu;
  1. Tunamshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda Tume maalumu ya kuchunguza matukio yote ya kupotea kwa watu, kutekwa na kuteswa;​
  2. Tunamshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda Tume Maalum ya kuchunguza ushiriki wa Jeshi la Polisi kwenye masuala ya Utekaji kwa kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likituhumiwa kushiriki katika vitendo hivyo;​
  3. Tunapendekeza kuundwa kwa chombo maalumu cha kudumu cha kuangalia utendaji wa vyombo vya dola (oversight body) ili kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria; na​
  4. Tunalitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi yake kwa weledi kwa mujibu wa Katiba na Sheria ili kuhakikisha usalama na ulinzi wa wananchi na mali zao unaimarika​
TLS inaendelea kufuatilia matukio haya kwa ukaribu na iko tayari kushirikiana na vyombo vyote vya dola katika kuhakikisha wahusika wote wa matukio haya wanafikishwa katika vyombo mahususi vya haki ili haki ionekane inatendeka. Hata hivyo, tunatoa rai kwa watanzania wote kuwa makini wakati wote na kutokubali kuitwa au kukutana na watu wasiowajua au kwenda mahali wasipopajua na ikibidi sana wawasiliane na wakili yeyote kabla ya kukutana au kwenda mahali wasipopajua.​

Imetolewa na Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)

Boniface A.K Mwabukusi
Rais


KIAMBATISHO:

ORODHA YA WATU WALIOTEKWA/KUPOTEA 2016-2024.
S/N JINA MAELEZO MAFUPI MAKAZI
1.
KOMBO MBWANA TWAHA​
Alitekwa nyumbani kwake Handeni Tanga na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 15 Juni 2024, baadaye polisi walikanusha kuhusika na kufungua jalada la uchunguzi. Siku 29 baadaye polisi walikiri kuhusika na kumshikilia kwa hizo siku zote.​
Handeni - Tanga
2KENNEDY MWAMLIMA
Alitekwa Mbeya na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 11 Aprili 2024. Alipatikana Igunga Tabora Tarehe 16 Aprili 2024 akiwa ametapakaa majeraha. Kwa maelezo yake alikuwa akiteswa katika vituo vya polisi na alikuwa akiulizwa nani anamtuma kukosoa serikali katika mtandao wa TikTok.​
Mbeya Jiji -Mbeya
3EDGER MWAKALEBELAAlitekwa tarehe 23 Juni 2024 Ubungo Dar es Salaam.
Akapelekwa kituo cha polisi
OysterBay na baadaye​
Arusha kabla ya kupatikana tarehe 27 Juni 2024 mkoani Katavi porini akiwa ametapakaa majeraha.
Dar es Salaam.
4JAMES SIJE
Alitekwa na askari polisi anayeitwa Sgt. Mageni Musobi A.K.A Majani wa kituo cha polisi Nyakato tarehe 17 Agosti 2021 mpaka sasa hajapatikana.​
Nyakato –Mwanza
5JOSEPH MNYONGA
Alitekwa Julai 2021 nyumbani kwake Mwanza na watu waliojitambulisha kuwa​
Mwanza.


ni askari polisi kutoka mkoa wa Mwanza mpaka sasa hajapatikana.​
6DOTTO KABWA
Alitekwa tarehe 4 Julai 2022 na askari polisi anayejulikana kwa jina la Wambura Mwita kutoka kituo cha polisi Ifunda Iringa na hajapatikana mpaka leo.​
Ifunga-Iringa
7YAHYA ALLY
Alitekwa tarehe 6Septemba 2022 Mbagala Kizuiani na askari polisi wakiongozwa na OC-CID Abdalah Suleiman.​
Mpaka sasa hajapatikana.
Mbagala – Dar es Salaam.
8CHANDE KIZEGA
Alitekwa na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 18 Agosti 2022 akiwa dukani kwake Machinga Complex. Mpaka sasa hajapatikana.​
Dar es Salaam
9Mzee SAMUEL MKONGOMATIKO
Alitekwa mkoani Geita tarehe 27 Januari 2023 na askari polisi Sgt. Hamis mwenye namba 0789938835 na kupelekwa kituo cha Muriaza –Butiama mkoani Mara. Ndugu walifika hapo na wakamuona akiwa ametapakaa majeraha, lakini waliporudi kumletea chakula hawakumkuta tena kituoni hapo na hajaonekana mpaka leo.​
Geita mjini.
10CHARLES
MWAMPYATE
ADEN
Alitoweka tangu tarehe 7 Decemba 2023 akiwa Dar es Salaam na hajapatikana mpaka leo.​
Dar es Salaam.
11WILLIAM HERMAN
Alitekwa Mwanza tarehe 1 Januari 2024 na askari polisi anayefahamika kwa jina la Sgt. Mageni Musobi A.K.A​
Kangaye-Mwanza


Majani wa kituo cha polisi Nyakato.​
12DAVID GASPER LEMA
Alipotea akiwa njiani kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam tangu tarehe 6 Aprili 2024 na mpaka sasa hajapatikana.​
Mwanza
13JEROME KISOKA a.k.a MAPII
Alitekwa na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 14 Novemba 2023 eneo la Njoro, Moshi mkoani Kilimanjaro na hajapatikana mpaka leo.​
Moshi-Kilimanjaro
14RIDHIWANI HEMED MSANGI
(PIA AMEKUWA
AKIJULIKANA KWA JINA LA
ABDALLAH SALUM MSANGI)
Alipotea mkaoni Iringa mwishoni mwa mwezi Julai 2021 na hajapatikana mpaka leo. Kazi yake alikuwa mhadhiri (Lecturer) Chuo Kikuu cha Mkwawa ambalo ni tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.​
Iringa
15BENSON E.A. ISHUNGISA
Alitekwa na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 26 Novemba 2023 akiwa nje ya Hospital ya Makangarawe Yombo mkoani Dar es Salaam. Benson alikuwa akimsubiri abiria nje ya Hospital hiyo na hata bodaboda wenzake walipoulizwa kituo cha polisi anachopelekwa hawakujibiwa. Mpaka leo hajapatikana.​
Dar es Salaam
16HAMZA SAID
Katibu wa chama cha NCCR Mageuzi mkoa wa Geita. Alitekwa tarehe 17 Decemba 2023 nyumbani kwake mtaa wa Mwatulole mkoani Geita na watu waliojitambulisha ni askari polisi. Mpaka leo Katibu huyo hajapatikana​
Mwatulole-Geita


17YONZO SHIMBI DUTU
Alikamatwa tarehe 2 Machi 2024 na askari polisi wa kituo cha polisi Kwimba Mwanza akiwa na wenzake maeneo ya Bushini-Kishapu mkoani​
Shinyanga. Wenzake waliachiwa ila yeye hajapatikana na hayupo vituo vyote vya polisi.
Kishapu-Shinyanga
18LILENGA ISAYA LILENGA
Alitekwa tarehe 11 Mei 2024 maeneo ya Kibirizi mkoani Kigoma na watu wanaodaiwa ni polisi kisha kutokomea naye kusikojulikana. Mpaka sasa hajapatikana.​
Mwandiga-Kigoma
19TAWAFIQ MOHAMEDAlitekwa tarehe 26 Decemba
2021 eneo la Kamata,
Kariakoo mkoani Dar es Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.​
Dar es Salaam
20SELF SWALA
Alitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar es​
Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.
Dar es Salaam
21EDWIN KUNAMBIAlitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar es
Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.
Dar es Salaam
22HEMED ABASSAlitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar esDar es Salaam


Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.
23RAJABU MDOEAlitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar es
Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.
Dar es Salaam
24MZEE HAJI SOFTAlichukuliwa nyumbani kwake Temeke na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 13 Julai 2021 na mpaka sasa hajapatikana.Temeke – Dar es
Salaam
25ALPHONCE BILASENGEAlitoweka ghafla. Simu yake mara ya mwisho ilizimwa eneo la Kibeta, wilaya ya Bukoba mjini mkoani Kagera tarehe 6 Januari 2022.Kagera
26ALBERT KISEYA SELEMBOAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi akiwa na kesi ya Mauwaji.Loliondo - Arusha
27MOLOIMETI YOHANA
SAING’EU
Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha Polisi akiwa na kesi ya Mauwaji.Loliondo - Arusha
28NDIRANGO SENGE LAIZERAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022Loliondo - Arusha


wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.
29JOEL CREMES LESSONUAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
30SIMONI NAIRIAM
OROSIKIRIA
Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
31DAMIAN LAGO LAIZERAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
32MATHEW ELIAKIMU SILOMAAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha


33LUKAS K. NJAUSIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
34TALENG’O TWAMBEI
LESHOKO
Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
35KIJOOLU KAKEI OLOJILOJIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo – Arusha
36SHENGENA JOSEPH KILLELAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo Arusha
37MASEKE MWITA MASEKEAlitoweka tangu tarehe 10 Juni 2022 mpaka sasa hajapatikana.Nkerege -Tarime- Mara
38MALONGO DANIEL PASCHALAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni yaLoliondo - arusha


serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.
39SIMELI PARMWATI
KARONGOI
Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
40INGOI OLKEDENYI KANJWEIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
41SANGAU MORONGETI
NGIMINIS
Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
42MARIJOI NGOISA PARMATIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha


43MORONGETI MASAKOMSEEKIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
44KAMBATAI LULUAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
45ORIAS OLENG’IYOAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo -Arusha
46WILSON KOLONGAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 12 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
47JAMES TAKIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 13 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadayeLoliondo - Arusha


aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.
48JOSEPH JARTANAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 13 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
49KELVIN SHASO NAIROTIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
50LEKERENGA KOYEE ORODOAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo -Arusha
51FRED VICTOR LEDIDIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.Loliondo - Arusha
52SIMON MORINTANTIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwaLoliondo - Arusha


nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi.
53MOHAMED KAYEGO KALEBEAlikamatwa na watu wengine sita (6) na maafisa waliojitambulisha kuwa ni askari polisi tarehe 5 Apriil 2023 huko Katoro mkoani Geita. Ndugu walifika vituo vyote vya polisi hawakumkuta na hajapatikana mpaka leo yeye na hao wenzake ambao majina hayajatambulika mpaka sasa.Katoro - Geita
54AMON MRIGI MAGIGEAlikamatwa na askari wa jeshi la Polisi wakiwa na gari za Polisi Land Cruiser Pick Up mbili hapo tarehe 1 Octoba
2023. Mpaka sasa hajapatikana na hayupo kituo chochote cha polisi wala gerezani.
Mwanza
55AZIZ KINYONGAAlipotea siku kadhaa, kwa maelezo ya mke wake anasema baada ya mume wake kupotea siku kadhaa baadaye ilifika gari aina ya Toyota Noah na ndani ya ile gari alionekana mtu akinyosha kidole kuonyesha nyumba yao. Mke anasema hakujua ni mume wake. Anadai walishuka watu waliojitambulisha ni askari walikagua nyumba wakakuta kuna laki mbili wakachukua na kuondoka. Baadaye gari ya mume wake Aziz lilikutwa limetelekezwa mkoani Mtwara. Hajapatikana tangu tarehe 1 Februari 2023.Chamazi – Dar es Salaam.


56YUSUPH DUDUAlitekwa nyumbani kwake na watu wenye silaha waliojitambulisha ni polisi.
Watu hao walipofika nyumbani kwa Yusuph walimkuta mtoto wake mwenye miaka 8 wakamwambie kamwite baba yako na kisha Yusuph alivyofika walijitambulisha ni askari polisi na kuondoka naye tangu tarehe 9 Aprili
2024 mpaka sasa hajapatikana. Jarada la uchunguzi la kupotea kwake limefunguliwa kituo cha polisi Mbagala Maturubai MBL/RB/2891/2024.
Mbagala – Dar es Salaam
57KASTORY KAPINGAMwanafunzi wa chuo cha SAUT, kituo cha Arusha mwaka wa tatu alipotea akiwa wilayani Mbinga mkoani Ruvuma tangu mwanzoni mwa mwezi Aprili 2024. Hajapatikana mpaka sasa.Ruvuma - Mbinga
58DIONIZ KIPANYAAlitoweka tangu tarehe 27 Julai 2024 huko Sumbawanga mkoani.
Hajapatikana mpaka leo.
Sumbawanga- Rukwa
59SHADRACK CHAULAAlitekwa tarehe 2 Agosti 2024 kijijini kwao Ntokela, wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Siku 20 kabla ya kutekwa Shadraka Chaula alitolewa jela kwa michango ya watanzania walioamua kumlipia faini baada ya kufungwa jela au kulipa faini kwa kosa la kuchoma picha ya Rais Samia Suluhu Hassan.Ntokela – Rungwe – Mbeya


60PROSIPER THEONAS MNJARIAlitekwa na watu waliojitambulisha kuwa ni askari wa Polisi na walikuwa wameongozana na watumishi wa TANESCO. Watekaji wao walisema nyumba yao ina deni kubwa sana la umeme yeye akajibu kuwa ni mpangaji tu awaunganishe na mwenye nyumba lakini walikataa na kuondoka naye mpaka sasa hajapatikana.Chamazi – Dar es Salaam
61THOMAS MUNGO IHUYAAlikuwa anafanya kazi Mahakama kuu Mwanza alipotea tangu March 2018 mpaka leo hajapatikana.Mwanza
62DENNIS KANTANGAAlikuwa mkazi wa mkoa wa Shinyanga Mjini na alikuwa akifanya shughuli za TEHAMAkwa maana ya kutengeneza na kuuza computers, desktop pamoja na laptops na vifaa vingine vya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano (TEHAMA) ikiwemo CCTV. Siku anachukuliwa alifuatwa dukani kwake na watu wawili au zaidi lakini waliofika dukani walikuwa wawili na kujitambulisha kuwa ni askari. Waliondoka kwa gari yake mwenyewe(Dennis) na ikawa mwisho wa kusikikika kwake. Katika utaratibu wa kuripoti polisi na kutrack simu ilionekana simu yake iliwashwa wilayani Musoma mkoani Mara na baada ya hapo haikupatikana tena. Gari yake ilikuja kupatikana maeneo ya wilaya ya Nzega mkoani Tabora ikiwa imeegeshwa katikati ya mji
Shinyanga


baada ya wiki moja. Ni miaka 4 sasa imepita toka kutoweka kwake.
63Damas Vedastus BulimbeAlipotea tarehe 15 Novemba 2023 huko Geita.
Hajapatikana mpaka leo.
Geita
64Lucas Magambo BulimbeAlipotea tarehe 15 Novemba 2023 huko Geita.
Hajapatikana mpaka leo.
Geita
65Matuki MakuruAlitoweka tarehe 15 Februari 2024 wilayani Serengeti mkoani mara. Hajapatikana mpaka leo.Serengeti, Mara
66Dastan Gervas NestoryAlitoweka tarehe 9 Julai 2024 huko Mkoani Geita.
Hajapatikana hadi sasa.
Geita
67Adinan Hussein MbeziAlitoweka tarehe 16 Septemba 2023 huko mkoani Geita. Hajapatikana hadi leo.Geita
68Lengaripo Lebahati LukumayAlitoweka tarehe 7 Mei 2021 huko mkoani Mwanza.
Hajapatikana hadi sasa.
Mwanza
69Akidu Twaha SalimAlitoweka tarehe 6 Oktoba 2023 mkoani Dar es Salaam.
Hajapatikana hadi sasa.
Dar es Salaam
70Enock John ChambalaAlitoweka tarehe 6 Julai 2024 huko mkoani Tanga.
Hajapatikana hadi sasa.
Tanga
71Dioniz KipanyaAlitoweka tarehe 26 Julai 2024 huko mkoani Katavi.
Hajapatikana hadi sasa.
Katavi
72Nusra OmariAlitoweka tarehe 7 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Alipatikana akiwa amefariki.
Dar es Salaam
73Theresphora MwakalingaAlitoweka tarehe 17 Julai 2024 huko mkoani Dodoma.
Alipatikana akiwa amefariki.
Dodoma
74Donald Kalist MboyaAlitoweka tarehe 29 Juni 2024 huko mkoani Kagera.
Hajapatikana hadi leo.
Kagera
75Ilham MakoyeAlitoweka tarehe 2 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Alipatikana baadae.
Dar es Salaam
76Barack MajigehAlitoweka tarehe 5 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Hajapatikana hadi leo.
Dar es Salaam
77JoshuaAlitoweka tarehe 5 Julai 2024 huko mkoani Iringa.
Hajapatikana hadi leo.
Iringa
78Yusra MusaAlitoweka tarehe 9 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Alipatikana akiwa amefariki.
Dar es Salaam
79Angel Albert KamugishaAlitoweka tarehe 15 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam na baadae kupatikana.Dar es Salaam
80Brighton Amos EmmanuelAlitoweka tarehe 16 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam na kuja kupatikana baadae.Dar es Salaam


81
Azory GwandaAlitoweka tarehe 17
Novemba 2017 Kibiti mkoani Pwani na hajapatikana hadi leo
Pwani


82
Ben SaananeAlitoweka tarehe 15 Novemba 2016 Dar es
Salaam na hajapatikana hadi leo
Dar es Salaam


83
Simon KanguyeAlitoweka tarehe 20 Julai 2017 Kigoma na hajapatikana mpaka leo.Kigoma
 
Hangaya na mwenzake Aijipii si walishasema ni drama za kujiteka?

Si mlisema yule hivi, aliyepo ni tofauti, sasa mtaelewa kwanini pande la ardhi kakabidhiwa wa-kipeimmba, ilihali wanaandaliwa(ga) kuwa maululaini tu!
 
Hadi nimeogopa.wote wanaowateka wanajitambulisha kabisa ni polisi.Tunaowatengemee walinde Nchi ndiyo majambazi!. Wananchi tukiamua kuwashughulikia Hawa polisi hatushindwi kitu.Nguvu ya umma siku zote ni ushindi.kama Hadi wametajwa majina na namba zao za simu,wananchi tukiungana Hawa wahuni tutawatia adabu.
 
Hadi nimeogopa.wote wanaowateka wanajitambulisha kabisa ni polisi.Tunaowatengemee walinde Nchi ndiyo majambazi!. Wananchi tukiamua kuwashughulikia Hawa polisi hatushindwi kitu.Nguvu ya umma siku zote ni ushindi.kama Hadi wametajwa majina na namba zao za simu,wananchi tukiungana Hawa wahuni tutawatia adabu.
Kama issue ya Mzee SAMUEL MATIKO MKONGO namba 9 hapo daah imenisikitisha sana
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society - TLS) kikiongozwa na wakili Boniface A.K Mwabukusi kimetoa tamko zito lililoweka wazi hali ya kusikitisha inayolikumba taifa. Kwa mujibu wa tamko hilo, kumekuwa na ongezeko la matukio ya kutekwa, kupotea, na kuteswa kwa watu nchini Tanzania, huku vyombo vya dola vikishindwa kutoa ufafanuzi wa kuridhisha au kuchukua hatua stahiki dhidi ya vitendo hivi vya kikatili.

TLS imeeleza wasiwasi mkubwa kuhusu jinsi Jeshi la Polisi limekuwa likishughulikia matukio haya. Licha ya taarifa nyingi kutolewa kuhusu utekaji na utesaji, mara kwa mara vyombo hivi vimeonekana kukanusha madai haya, hata pale ambapo ushahidi wa kutosha umeibuka kuthibitisha ukweli wa matukio haya. Hali hii imeongeza hofu na wasiwasi miongoni mwa wananchi, ambao wanahisi kutokuwa salama katika nchi yao wenyewe.

Katika tamko hilo, TLS inakemea vikali vitendo vya utekaji na utesaji, ikieleza kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kama ilivyowekwa bayana katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mikataba ya kimataifa. TLS imeishauri serikali, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kuchukua hatua za haraka kuunda Tume Maalum itakayochunguza matukio haya na kubaini wahusika wa uhalifu huu.

Aidha, chama hicho kinapendekeza kuanzishwa kwa chombo maalum cha kudumu kitakachokuwa na jukumu la kusimamia na kuangalia utendaji wa vyombo vya dola, kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi. Kwa kufanya hivyo, TLS inaamini kuwa itaimarisha uadilifu wa vyombo vya dola na kurejesha imani ya wananchi kwa serikali yao.

Katika kiambatanisho cha tamko hilo, TLS imetoa orodha ya baadhi ya watu waliotekwa au kupotea kuanzia mwaka 2016 hadi 2024, ikiwa ni ushahidi wa dhahiri wa kuendelea kwa vitendo hivi vya kikatili. Baadhi ya watu hao walipatikana wakiwa wamejeruhiwa, huku wengine wakiwa hawajulikani walipo hadi sasa.

Kwa kuhitimisha, TLS inatoa wito kwa wananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari za ziada katika maisha yao ya kila siku, na kutoa taarifa kwa mamlaka husika endapo watahisi hatari yoyote. Huu ni wakati muhimu kwa Watanzania wote kusimama pamoja katika kupinga vitendo hivi vya ukiukwaji wa haki za binadamu na kudai uwajibikaji kutoka kwa viongozi wao.

TAMKO 👇🏼
View attachment 3065683
View attachment 3065684
View attachment 3065686
View attachment 3065687
View attachment 3065688
View attachment 3065689View attachment 3065690
View attachment 3065691
View attachment 3065693
View attachment 3065696
View attachment 3065697
View attachment 3065698
View attachment 3065699
View attachment 3065701
View attachment 3065703
View attachment 3065704
View attachment 3065705
Hili kwa policeccm utawaona kimya
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society - TLS) kikiongozwa na wakili Boniface A.K Mwabukusi kimetoa tamko zito lililoweka wazi hali ya kusikitisha inayolikumba taifa. Kwa mujibu wa tamko hilo, kumekuwa na ongezeko la matukio ya kutekwa, kupotea, na kuteswa kwa watu nchini Tanzania, huku vyombo vya dola vikishindwa kutoa ufafanuzi wa kuridhisha au kuchukua hatua stahiki dhidi ya vitendo hivi vya kikatili.

TLS imeeleza wasiwasi mkubwa kuhusu jinsi Jeshi la Polisi limekuwa likishughulikia matukio haya. Licha ya taarifa nyingi kutolewa kuhusu utekaji na utesaji, mara kwa mara vyombo hivi vimeonekana kukanusha madai haya, hata pale ambapo ushahidi wa kutosha umeibuka kuthibitisha ukweli wa matukio haya. Hali hii imeongeza hofu na wasiwasi miongoni mwa wananchi, ambao wanahisi kutokuwa salama katika nchi yao wenyewe.

Katika tamko hilo, TLS inakemea vikali vitendo vya utekaji na utesaji, ikieleza kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kama ilivyowekwa bayana katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mikataba ya kimataifa. TLS imeishauri serikali, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kuchukua hatua za haraka kuunda Tume Maalum itakayochunguza matukio haya na kubaini wahusika wa uhalifu huu.

Aidha, chama hicho kinapendekeza kuanzishwa kwa chombo maalum cha kudumu kitakachokuwa na jukumu la kusimamia na kuangalia utendaji wa vyombo vya dola, kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi. Kwa kufanya hivyo, TLS inaamini kuwa itaimarisha uadilifu wa vyombo vya dola na kurejesha imani ya wananchi kwa serikali yao.

Katika kiambatanisho cha tamko hilo, TLS imetoa orodha ya baadhi ya watu waliotekwa au kupotea kuanzia mwaka 2016 hadi 2024, ikiwa ni ushahidi wa dhahiri wa kuendelea kwa vitendo hivi vya kikatili. Baadhi ya watu hao walipatikana wakiwa wamejeruhiwa, huku wengine wakiwa hawajulikani walipo hadi sasa.

Kwa kuhitimisha, TLS inatoa wito kwa wananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari za ziada katika maisha yao ya kila siku, na kutoa taarifa kwa mamlaka husika endapo watahisi hatari yoyote. Huu ni wakati muhimu kwa Watanzania wote kusimama pamoja katika kupinga vitendo hivi vya ukiukwaji wa haki za binadamu na kudai uwajibikaji kutoka kwa viongozi wao.

TAMKO 👇🏼
View attachment 3065683
View attachment 3065684
View attachment 3065686
View attachment 3065687
View attachment 3065688
View attachment 3065689View attachment 3065690
View attachment 3065691
View attachment 3065693
View attachment 3065696
View attachment 3065697
View attachment 3065698
View attachment 3065699
View attachment 3065701
View attachment 3065703
View attachment 3065704
View attachment 3065705
Huu ni mwanzo mzuri kwa TLS.

Siku mbili tu zilizopita nilitoa wito kwa TLS ili waliangazie jambo hili baya, na leo kweli nimeona tamko lao hili . Kwa kweli TLS hii kwa kiasi fulani inatia moyo, kwa sababu ni kweli kabisa kwamba ni taasisi ambayo inagusa moja kwa moja maslahi mapana ya umma, inagusa hisia za Watu walio wengi zaidi katika nchi. Pongezi za pekee kabisa zikufikie Bw. Advocate Boniphace A. K. Mwabukusi popote pale ulipo, Mungu akuongoze vyema kwenye suala hili.

Kwa hakika TLS hii ya sasa ni taasisi ya umma na ni mali ya umma.
 
Huu ni mwanzo mzuri kwa TLS.

Siku mbili tu zilizopita nilitoa wito kwa TLS ili waliangazie jambo hili baya, na leo kweli nimeona tamko lao hili . Kwa kweli TLS hii kwa kiasi fulani inatia moyo, kwa sababu ni kweli kabisa kwamba ni taasisi ambayo inagusa moja kwa moja maslahi mapana ya umma, inagusa hisia za Watu walio wengi zaidi katika nchi. Pongezi za pekee kabisa zikufikie Bw. Advocate Boniphace A. K. Mwabukusi popote pale ulipo, Mungu akuongoze vyema kwenye suala hili.

Kwa hakika TLS hii ya sasa ni taasisi ya umma na ni mali ya umma.
Pongezi kwa TLS wakiongozwa na Wakili Mwabukusi. Wito wako juu ya suala hili
 
Instand to be corrected. Wakili Mwambukusi inawezekana kabisa aka win majority ya voters Tanzania na akaja kuwa rais kiutani utani. Watanzania wa sasa ana access to info 💯. Dkt Samia kama anaweza yafanyike yale ya kwa madiba, zile 4R zifanye kazi, na atuletee katiba mpya. Yeah kuna wengine siyo police ila panahitajika kujua ukweli ili kuponya mioyo na kurudisha imani kwa watanzania.
 
List ni ndefu inatisha. Ila jambo moja nimeona kuwa waliopotea chini ya JPM ni watatu (81), (82) na (83); wengine waliobaki themanini ni chini ya mama.

Wakati wa JPM kelele zilikuwa kubwa sana kumlenga JPM mwenyewe kuwa ndiye aliyeagize watu hao watekwe kiasi kuwa mpaka leo tunajua majina ya waathirika hao. Wakati huu kumekuwa hakuna anayepigia kelele mambo haya kwani ni vigumu kuthubutu kumlenga mama kuwa ndiye aliyeagiza watu hao wote themanini wapewe dhahama hiyo.

Nadhani chanzo cha tatizo hili kwa kiasi kikubwa ni utendaji mbovu wa polisi na vyombo vingine vya usalama lakini tulianza kwa kusukumia lawama zote kwa JPM wakati huo, na leo tunashindwa kumpata wa kulaumu.
 
List ni ndefu inatisha. Ila jambo moja nimeona kuwa waliopotea chini ya JPM ni watatu (81), (82) na (83); wengine waliobaki themanini ni chini ya mama. Wakati wa JPM kelele zilikuwa kubwa sana kumlenga JPM mwenyewe kuwa ndiye aliyeagize watu hao watekwe kiasi kuwa mpaka leo tunajua majina ya waathirika hao. Wakati huu kumekuwa hakuna anayepigia kelele mambo haya kwani ni vigumu kuthubutu kumlenga mama kuwa ndiye aliyeagiza watu hao wote themanini wapewe dhahama hiyo.

Nadhani chanzo cha tatizo hili kwa kiasi kikubwa ni utendaji mbovu wa polisi na vyombo vingine vya usalama lakini tulianza kwa kusukumia lawama zote kwa JPM wakati huo, na leo tunashindwa kumpata wa kulaumu.
Dah ume sema vizuri sana. Tatizo ni mfumo wa kikoloni wa kutaka kufurahisha watawala badala ya watanzania. Naamini kuna watu wanalipwa mishahara kwa kodi za watanzania na yet wanawapoteza.
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society - TLS) kikiongozwa na wakili Boniface A.K Mwabukusi kimetoa tamko zito lililoweka wazi hali ya kusikitisha inayolikumba taifa. Kwa mujibu wa tamko hilo, kumekuwa na ongezeko la matukio ya kutekwa, kupotea, na kuteswa kwa watu nchini Tanzania, huku vyombo vya dola vikishindwa kutoa ufafanuzi wa kuridhisha au kuchukua hatua stahiki dhidi ya vitendo hivi vya kikatili.

TLS imeeleza wasiwasi mkubwa kuhusu jinsi Jeshi la Polisi limekuwa likishughulikia matukio haya. Licha ya taarifa nyingi kutolewa kuhusu utekaji na utesaji, mara kwa mara vyombo hivi vimeonekana kukanusha madai haya, hata pale ambapo ushahidi wa kutosha umeibuka kuthibitisha ukweli wa matukio haya. Hali hii imeongeza hofu na wasiwasi miongoni mwa wananchi, ambao wanahisi kutokuwa salama katika nchi yao wenyewe.

Katika tamko hilo, TLS inakemea vikali vitendo vya utekaji na utesaji, ikieleza kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kama ilivyowekwa bayana katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mikataba ya kimataifa. TLS imeishauri serikali, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kuchukua hatua za haraka kuunda Tume Maalum itakayochunguza matukio haya na kubaini wahusika wa uhalifu huu.

Aidha, chama hicho kinapendekeza kuanzishwa kwa chombo maalum cha kudumu kitakachokuwa na jukumu la kusimamia na kuangalia utendaji wa vyombo vya dola, kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi. Kwa kufanya hivyo, TLS inaamini kuwa itaimarisha uadilifu wa vyombo vya dola na kurejesha imani ya wananchi kwa serikali yao.

Katika kiambatanisho cha tamko hilo, TLS imetoa orodha ya baadhi ya watu waliotekwa au kupotea kuanzia mwaka 2016 hadi 2024, ikiwa ni ushahidi wa dhahiri wa kuendelea kwa vitendo hivi vya kikatili. Baadhi ya watu hao walipatikana wakiwa wamejeruhiwa, huku wengine wakiwa hawajulikani walipo hadi sasa.

Kwa kuhitimisha, TLS inatoa wito kwa wananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari za ziada katika maisha yao ya kila siku, na kutoa taarifa kwa mamlaka husika endapo watahisi hatari yoyote. Huu ni wakati muhimu kwa Watanzania wote kusimama pamoja katika kupinga vitendo hivi vya ukiukwaji wa haki za binadamu na kudai uwajibikaji kutoka kwa viongozi.

TAMKO 👇🏼
View attachment 3065683
View attachment 3065684
View attachment 3065686
View attachment 3065687
View attachment 3065688
View attachment 3065689View attachment 3065690
View attachment 3065691
View attachment 3065693
View attachment 3065696
View attachment 3065697
View attachment 3065698
View attachment 3065699
View attachment 3065701
View attachment 3065703
View attachment 3065704
View attachment 3065705

TLS safi sana. Polisi na mamlaka zingine za usalama watupe maelezo hawa watu wamepoteaje.
 
Back
Top Bottom