Abdul Said Naumanga
JF-Expert Member
- Jan 28, 2024
- 673
- 1,318
- Thread starter
-
- #61
Sikujua kama hali ni mbaya kiasi hiki lakini kwa mwenendo huo ni dhahiri sio salama tena hapa mahali.
List bado ndefu,hapo sijaona jina la yule jamaa aliyetekwa mitaa ya mikocheni...mfanyabiasharaSikujua kama hali ni mbaya kiasi hiki lakini kwa mwenendo huo ni dhahiri sio salama tena hapa mahali.
Ndugu zangu hii inatisha sana. Takwimu ni muhimu siku zote.
Tumeishi bila kujua Ukubwa watatizo. Kumbe ni tatizo kubwa sana.
Ile ya kusikia mmoja mmoja kachukuliwa kama mbayuwayu.
Ktk Orodha iliyotolewa na TLS hapo jana idadi kubwa ya waathirika inaonekana Kanda ya Ziwa yaani Shinyanga, Geita, Mwanza na Kigoma.
Pia idadi imeonekana Dar Es Salama na Arusha ikifuatiwa na Mbeya na ama Iringa.
Takribani watu 80 wameathirika na mkasa huu. Inasikitisha na inasononesha sana.
Kwa mujibu wa Orodha iliyotaja siku na tarehe ya matukio ya utekaju au ukamataji/ upoteaji inaonesha idadi kubwa ni kuanzia mwaka 2021 na idadi ndogo sana kuanzia mwaka 2020 kushuka chini yaani 2016.
Hii inatafakarisha sana.
Mwenyezi Mungu amuinue mtu mwenye haki atamalaki juu ya Taifa hili liweze kupona.
Umehoji mambo muhimu sanaSwali ambalo linanitatiza ni kwa nini vyombo vya habari kote nchini vimechagua kukaa kimya kuhusu suala hili. Je, ina maana hawatambui umuhimu wa Watanzania wote kulifahamu? Wanaogopa kuliibua? Au kuna ushawishi kutoka kwa watawala unaowazuia kuzungumzia suala hili? Nieleweke vizuri, sihitimishi kwamba kimya hichi ni ushahidi wa kuhusika kwa serikali / watawala moja kwa moja, la hasha. Hata hivyo, inawezekana kwamba kuna hofu ya kuzua taharuki katika jamii yetu.
Hata hivyo, ningependekeza kwamba badala ya kuendelea kukaa kimya, serikali ingetoa kauli rasmi kuhusu hatua zinazochukuliwa katika kushughulikia suala hili. Kauli hiyo ingewatuliza wananchi na kupunguza taharuki inayoongezeka, hasa kwa kuwa tayari orodha ya wahanga na wahusika imetolewa. Kwa sasa, kimya cha vyombo vya habari na serikali kinazidisha wasiwasi. Swali ni, Watanzania tunatakiwa kuelewa nini kutokana na hali hii?
Deep Down from my Heart this is the Best Comment i have never seen From You Mr Mudawote.Instand to be corrected. Wakili Mwambukusi inawezekana kabisa aka win majority ya voters Tanzania na akaja kuwa rais kiutani utani. Watanzania wa sasa ana access to info 💯. Dkt Samia kama anaweza yafanyike yale ya kwa madiba, zile 4R zifanye kazi, na atuletee katiba mpya. Yeah kuna wengine siyo police ila panahitajika kujua ukweli ili kuponya mioyo na kurudisha imani kwa watanzania.
Tukipata vyombo viwili vitatu vinavyomonitor maswala kama haya tutaifikisha Mbali Nchi yetu.Kwa kweli nimefarijika sana kuona kwamba TLS wameanza kuliangazia suala hili, wito wangu huo wameufanyia kazi kikamilifu kabisa. Yaani we acha tu, TLS hii!
All those SoulsList ni ndefu wazee
Sometimes, silence means admission of fact.Swali ambalo linanitatiza ni kwa nini vyombo vya habari kote nchini vimechagua kukaa kimya kuhusu suala hili. Je, ina maana hawatambui umuhimu wa Watanzania wote kulifahamu? Wanaogopa kuliibua? Au kuna ushawishi kutoka kwa watawala unaowazuia kuzungumzia suala hili? Nieleweke vizuri, sihitimishi kwamba kimya hichi ni ushahidi wa kuhusika kwa serikali / watawala moja kwa moja, la hasha. Hata hivyo, inawezekana kwamba kuna hofu ya kuzua taharuki katika jamii yetu.
Hata hivyo, ningependekeza kwamba badala ya kuendelea kukaa kimya, serikali ingetoa kauli rasmi kuhusu hatua zinazochukuliwa katika kushughulikia suala hili. Kauli hiyo ingewatuliza wananchi na kupunguza taharuki inayoongezeka, hasa kwa kuwa tayari orodha ya wahanga na wahusika imetolewa. Kwa sasa, kimya cha vyombo vya habari na serikali kinazidisha wasiwasi. Swali ni, Watanzania tunatakiwa kuelewa nini kutokana na hali hii?
Huu ujinga upo kwa sababu hakuna cha kuwafanya. Hawashtakiwi.Chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society - TLS) kikiongozwa na wakili Boniface A.K Mwabukusi kimetoa tamko zito lililoweka wazi hali ya kusikitisha inayolikumba taifa. Kwa mujibu wa tamko hilo, kumekuwa na ongezeko la matukio ya kutekwa, kupotea, na kuteswa kwa watu nchini Tanzania, huku vyombo vya dola vikishindwa kutoa ufafanuzi wa kuridhisha au kuchukua hatua stahiki dhidi ya vitendo hivi vya kikatili.View attachment 3065684
TLS imeeleza wasiwasi mkubwa kuhusu jinsi Jeshi la Polisi limekuwa likishughulikia matukio haya. Licha ya taarifa nyingi kutolewa kuhusu utekaji na utesaji, mara kwa mara vyombo hivi vimeonekana kukanusha madai haya, hata pale ambapo ushahidi wa kutosha umeibuka kuthibitisha ukweli wa matukio haya. Hali hii imeongeza hofu na wasiwasi miongoni mwa wananchi, ambao wanahisi kutokuwa salama katika nchi yao wenyewe.
Katika tamko hilo, TLS inakemea vikali vitendo vya utekaji na utesaji, ikieleza kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kama ilivyowekwa bayana katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mikataba ya kimataifa. TLS imeishauri serikali, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kuchukua hatua za haraka kuunda Tume Maalum itakayochunguza matukio haya na kubaini wahusika wa uhalifu huu.
Aidha, chama hicho kinapendekeza kuanzishwa kwa chombo maalum cha kudumu kitakachokuwa na jukumu la kusimamia na kuangalia utendaji wa vyombo vya dola, kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi. Kwa kufanya hivyo, TLS inaamini kuwa itaimarisha uadilifu wa vyombo vya dola na kurejesha imani ya wananchi kwa serikali yao.
Katika kiambatanisho cha tamko hilo, TLS imetoa orodha ya baadhi ya watu waliotekwa au kupotea kuanzia mwaka 2016 hadi 2024, ikiwa ni ushahidi wa dhahiri wa kuendelea kwa vitendo hivi vya kikatili. Baadhi ya watu hao walipatikana wakiwa wamejeruhiwa, huku wengine wakiwa hawajulikani walipo hadi sasa.
Kwa kuhitimisha, TLS inatoa wito kwa wananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari za ziada katika maisha yao ya kila siku, na kutoa taarifa kwa mamlaka husika endapo watahisi hatari yoyote. Huu ni wakati muhimu kwa Watanzania wote kusimama pamoja katika kupinga vitendo hivi vya ukiukwaji wa haki za binadamu na kudai uwajibikaji kutoka kwa viongozi.
TAMKO 👇🏼
View attachment 3065683
View attachment 3065686
View attachment 3065687
View attachment 3065688
View attachment 3065689View attachment 3065690
View attachment 3065691
View attachment 3065693
View attachment 3065696
View attachment 3065697
View attachment 3065698
View attachment 3065699
View attachment 3065701
View attachment 3065703
View attachment 3065704
View attachment 3065705
09 Agosti, 2024
TAARIFA KWA UMMA
ONGEZEKO LA VITENDO VYA UTEKAJI NA UPOTEAJI WA WATU NCHINI
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kinasikitishwa na kinalaani vitendo vya kukamatwa, kutekwa na kuteswa kiholela kwa wananchi kunakoendelea nchini bila ya vyombo husika vya dola kuwajibika ipasavyo.
Kumekuwepo na taarifa mbalimbali za watu kupotea katika mazingira tatanishi, kutekwa na kuteswa na baadae kuonekana huku baadhi yao wakiwa wamefariki na wengine wakiwa na majeraha makubwa katika miili yao. Tunasikitishwa pia na namna ambavyo vyombo vyetu vya dola hususani Jeshi la Polisi limekuwa likifanyia kazi taarifa hizo. Mara kwa mara Jeshi la Polisi limekuwa likikanusha kutokea kwa matukio hayo lakini baadae inakuja kubainika kwamba matukio hayo ni ya kweli. Mara nyingine Jeshi la Polisi limekuwa likiwakamata raia wema wanaotoa taarifa hizo kwa kile kinachosemekana kusambaza taarifa za uongo badala ya kufanyia kazi taarifa hizo kwa mujibu wa Katiba na Sheria zinazowapasa kufanya wajibu wao wa kulinda watu na mali zao.
TLS, kwa mamlaka iliyopewa kupitia kifungu cha 4 cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act, Cap. 307 R.E. 2002), inapenda kuvikumbusha vyombo vya dola hususan Jeshi la Polisi juu ya majukumu yake ya Kikatiba na Kisheria ya kulinda watu na mali zao. Matukio haya ya utekaji ni kinyume na Ibara ya 13 (6) (e) na 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; pamoja na Mikataba ya Kimataifa inayozungumzia Haki za Binadamu na inayozuia uteswaji wa watu kama vile Mkataba dhidi ya Mateso na Unyanyasaji au Adhabu Nyingine za Kikatili au Udhalilishaji (Convention against Torture and Other Cruel, Inhuman or Degrading Treatment or Punishment), Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu (Universal Declaration of Human Rights) na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (The International Covenant on Civil and Political Rights).
TLS inatambua na kuheshimu taarifa za Jeshi la Polisi zinatolewa zikitaarifu umma kwamba matukio hayo yamekuwa yanafanyiwa uchunguzi lakini tunasikitika kwamba hakuna taarifa kamili ya uchunguzi wa tukio hata moja ambayo imewahi kutolewa kwa umma juu ya hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi juu ya watuhumiwa wa matukio hayo. Hali hii inaendelea kutia hofu kwa wananachi juu ya usalama wao na mashaka juu ya uwezo wa Jeshi la Polisi kuchunguza na kuchukua hatua stahiki kwa wahusika wa matukio hayo.
Kupitia tamko hili, tunaambatanisha orodha ya baadhi ya watu ambao wananchi au/na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini vimewahi kutoa taarifa za kupotea au kutekwa kwao ambapo baadhi yao walipatikana na baadhi yao wakiwa na majeraha huku kukiwa na wengine ambao waliopotea katika mazingira tatanishi na hawajapatikana mpaka leo. Tunaamini kwamba Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya dola vitafanyia kazi na kuhakikisha watu hao wamepatikana na wahusika wote wa matukio haya wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo husika vya haki ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa.
Wito wetu;
Tunamshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda Tume maalumu ya kuchunguza matukio yote ya kupotea kwa watu, kutekwa na kuteswa; Tunamshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda Tume Maalum ya kuchunguza ushiriki wa Jeshi la Polisi kwenye masuala ya Utekaji kwa kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likituhumiwa kushiriki katika vitendo hivyo; Tunapendekeza kuundwa kwa chombo maalumu cha kudumu cha kuangalia utendaji wa vyombo vya dola (oversight body) ili kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria; na Tunalitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi yake kwa weledi kwa mujibu wa Katiba na Sheria ili kuhakikisha usalama na ulinzi wa wananchi na mali zao unaimarikaTLS inaendelea kufuatilia matukio haya kwa ukaribu na iko tayari kushirikiana na vyombo vyote vya dola katika kuhakikisha wahusika wote wa matukio haya wanafikishwa katika vyombo mahususi vya haki ili haki ionekane inatendeka. Hata hivyo, tunatoa rai kwa watanzania wote kuwa makini wakati wote na kutokubali kuitwa au kukutana na watu wasiowajua au kwenda mahali wasipopajua na ikibidi sana wawasiliane na wakili yeyote kabla ya kukutana au kwenda mahali wasipopajua.
Imetolewa na Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)
Boniface A.K Mwabukusi
Rais
KIAMBATISHO:
ORODHA YA WATU WALIOTEKWA/KUPOTEA 2016-2024.
S/N JINA MAELEZO MAFUPI MAKAZI 1. KOMBO MBWANA TWAHA Alitekwa nyumbani kwake Handeni Tanga na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 15 Juni 2024, baadaye polisi walikanusha kuhusika na kufungua jalada la uchunguzi. Siku 29 baadaye polisi walikiri kuhusika na kumshikilia kwa hizo siku zote.Handeni - Tanga 2 KENNEDY MWAMLIMA Alitekwa Mbeya na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 11 Aprili 2024. Alipatikana Igunga Tabora Tarehe 16 Aprili 2024 akiwa ametapakaa majeraha. Kwa maelezo yake alikuwa akiteswa katika vituo vya polisi na alikuwa akiulizwa nani anamtuma kukosoa serikali katika mtandao wa TikTok.Mbeya Jiji -Mbeya 3 EDGER MWAKALEBELA Alitekwa tarehe 23 Juni 2024 Ubungo Dar es Salaam.
Akapelekwa kituo cha polisiArusha kabla ya kupatikana tarehe 27 Juni 2024 mkoani Katavi porini akiwa ametapakaa majeraha.
OysterBay na baadayeDar es Salaam. 4 JAMES SIJE Alitekwa na askari polisi anayeitwa Sgt. Mageni Musobi A.K.A Majani wa kituo cha polisi Nyakato tarehe 17 Agosti 2021 mpaka sasa hajapatikana.Nyakato –Mwanza 5 JOSEPH MNYONGA Alitekwa Julai 2021 nyumbani kwake Mwanza na watu waliojitambulisha kuwaMwanza.
ni askari polisi kutoka mkoa wa Mwanza mpaka sasa hajapatikana.6 DOTTO KABWA Alitekwa tarehe 4 Julai 2022 na askari polisi anayejulikana kwa jina la Wambura Mwita kutoka kituo cha polisi Ifunda Iringa na hajapatikana mpaka leo.Ifunga-Iringa 7 YAHYA ALLY Alitekwa tarehe 6Septemba 2022 Mbagala Kizuiani na askari polisi wakiongozwa na OC-CID Abdalah Suleiman.Mpaka sasa hajapatikana.Mbagala – Dar es Salaam. 8 CHANDE KIZEGA Alitekwa na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 18 Agosti 2022 akiwa dukani kwake Machinga Complex. Mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 9 Mzee SAMUEL MKONGO MATIKO Alitekwa mkoani Geita tarehe 27 Januari 2023 na askari polisi Sgt. Hamis mwenye namba 0789938835 na kupelekwa kituo cha Muriaza –Butiama mkoani Mara. Ndugu walifika hapo na wakamuona akiwa ametapakaa majeraha, lakini waliporudi kumletea chakula hawakumkuta tena kituoni hapo na hajaonekana mpaka leo.Geita mjini. 10 CHARLES
MWAMPYATEADEN Alitoweka tangu tarehe 7 Decemba 2023 akiwa Dar es Salaam na hajapatikana mpaka leo.Dar es Salaam. 11 WILLIAM HERMAN Alitekwa Mwanza tarehe 1 Januari 2024 na askari polisi anayefahamika kwa jina la Sgt. Mageni Musobi A.K.AKangaye-Mwanza
Majani wa kituo cha polisi Nyakato.12 DAVID GASPER LEMA Alipotea akiwa njiani kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam tangu tarehe 6 Aprili 2024 na mpaka sasa hajapatikana.Mwanza 13 JEROME KISOKA a.k.a MAPII Alitekwa na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 14 Novemba 2023 eneo la Njoro, Moshi mkoani Kilimanjaro na hajapatikana mpaka leo.Moshi-Kilimanjaro 14 RIDHIWANI HEMED MSANGI
(PIA AMEKUWA
AKIJULIKANA KWA JINA LA
ABDALLAH SALUM MSANGI) Alipotea mkaoni Iringa mwishoni mwa mwezi Julai 2021 na hajapatikana mpaka leo. Kazi yake alikuwa mhadhiri (Lecturer) Chuo Kikuu cha Mkwawa ambalo ni tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Iringa 15 BENSON E.A. ISHUNGISA Alitekwa na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 26 Novemba 2023 akiwa nje ya Hospital ya Makangarawe Yombo mkoani Dar es Salaam. Benson alikuwa akimsubiri abiria nje ya Hospital hiyo na hata bodaboda wenzake walipoulizwa kituo cha polisi anachopelekwa hawakujibiwa. Mpaka leo hajapatikana.Dar es Salaam 16 HAMZA SAID Katibu wa chama cha NCCR Mageuzi mkoa wa Geita. Alitekwa tarehe 17 Decemba 2023 nyumbani kwake mtaa wa Mwatulole mkoani Geita na watu waliojitambulisha ni askari polisi. Mpaka leo Katibu huyo hajapatikanaMwatulole-Geita
17 YONZO SHIMBI DUTU Alikamatwa tarehe 2 Machi 2024 na askari polisi wa kituo cha polisi Kwimba Mwanza akiwa na wenzake maeneo ya Bushini-Kishapu mkoaniShinyanga. Wenzake waliachiwa ila yeye hajapatikana na hayupo vituo vyote vya polisi.Kishapu-Shinyanga 18 LILENGA ISAYA LILENGA Alitekwa tarehe 11 Mei 2024 maeneo ya Kibirizi mkoani Kigoma na watu wanaodaiwa ni polisi kisha kutokomea naye kusikojulikana. Mpaka sasa hajapatikana.Mwandiga-Kigoma 19 TAWAFIQ MOHAMED Alitekwa tarehe 26 Decemba
2021 eneo la Kamata,
Kariakoo mkoani Dar es Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 20 SELF SWALA Alitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar esSalaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 21 EDWIN KUNAMBI Alitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar es
Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 22 HEMED ABASS Alitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar es Dar es Salaam
Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana. 23 RAJABU MDOE Alitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar es
Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 24 MZEE HAJI SOFT Alichukuliwa nyumbani kwake Temeke na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 13 Julai 2021 na mpaka sasa hajapatikana. Temeke – Dar es
Salaam25 ALPHONCE BILASENGE Alitoweka ghafla. Simu yake mara ya mwisho ilizimwa eneo la Kibeta, wilaya ya Bukoba mjini mkoani Kagera tarehe 6 Januari 2022. Kagera 26 ALBERT KISEYA SELEMBO Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi akiwa na kesi ya Mauwaji. Loliondo - Arusha 27 MOLOIMETI YOHANA
SAING’EUAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha Polisi akiwa na kesi ya Mauwaji. Loliondo - Arusha 28 NDIRANGO SENGE LAIZER Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 Loliondo - Arusha
wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. 29 JOEL CREMES LESSONU Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 30 SIMONI NAIRIAM
OROSIKIRIAAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 31 DAMIAN LAGO LAIZER Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 32 MATHEW ELIAKIMU SILOMA Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha
33 LUKAS K. NJAUSI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 34 TALENG’O TWAMBEI
LESHOKOAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 35 KIJOOLU KAKEI OLOJILOJI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo – Arusha 36 SHENGENA JOSEPH KILLEL Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo Arusha 37 MASEKE MWITA MASEKE Alitoweka tangu tarehe 10 Juni 2022 mpaka sasa hajapatikana. Nkerege -Tarime- Mara 38 MALONGO DANIEL PASCHAL Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya Loliondo - arusha
serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. 39 SIMELI PARMWATI
KARONGOIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 40 INGOI OLKEDENYI KANJWEI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 41 SANGAU MORONGETI
NGIMINISAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 42 MARIJOI NGOISA PARMATI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha
43 MORONGETI MASAKO MSEEKI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 44 KAMBATAI LULU Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 45 ORIAS OLENG’IYO Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo -Arusha 46 WILSON KOLONG Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 12 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 47 JAMES TAKI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 13 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye Loliondo - Arusha
aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. 48 JOSEPH JARTAN Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 13 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 49 KELVIN SHASO NAIROTI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 50 LEKERENGA KOYEE ORODO Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo -Arusha 51 FRED VICTOR LEDIDI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 52 SIMON MORINTANTI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa Loliondo - Arusha
nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. 53 MOHAMED KAYEGO KALEBE Alikamatwa na watu wengine sita (6) na maafisa waliojitambulisha kuwa ni askari polisi tarehe 5 Apriil 2023 huko Katoro mkoani Geita. Ndugu walifika vituo vyote vya polisi hawakumkuta na hajapatikana mpaka leo yeye na hao wenzake ambao majina hayajatambulika mpaka sasa. Katoro - Geita 54 AMON MRIGI MAGIGE Alikamatwa na askari wa jeshi la Polisi wakiwa na gari za Polisi Land Cruiser Pick Up mbili hapo tarehe 1 Octoba
2023. Mpaka sasa hajapatikana na hayupo kituo chochote cha polisi wala gerezani.Mwanza 55 AZIZ KINYONGA Alipotea siku kadhaa, kwa maelezo ya mke wake anasema baada ya mume wake kupotea siku kadhaa baadaye ilifika gari aina ya Toyota Noah na ndani ya ile gari alionekana mtu akinyosha kidole kuonyesha nyumba yao. Mke anasema hakujua ni mume wake. Anadai walishuka watu waliojitambulisha ni askari walikagua nyumba wakakuta kuna laki mbili wakachukua na kuondoka. Baadaye gari ya mume wake Aziz lilikutwa limetelekezwa mkoani Mtwara. Hajapatikana tangu tarehe 1 Februari 2023. Chamazi – Dar es Salaam.
56 YUSUPH DUDU Alitekwa nyumbani kwake na watu wenye silaha waliojitambulisha ni polisi.
Watu hao walipofika nyumbani kwa Yusuph walimkuta mtoto wake mwenye miaka 8 wakamwambie kamwite baba yako na kisha Yusuph alivyofika walijitambulisha ni askari polisi na kuondoka naye tangu tarehe 9 Aprili
2024 mpaka sasa hajapatikana. Jarada la uchunguzi la kupotea kwake limefunguliwa kituo cha polisi Mbagala Maturubai MBL/RB/2891/2024.Mbagala – Dar es Salaam 57 KASTORY KAPINGA Mwanafunzi wa chuo cha SAUT, kituo cha Arusha mwaka wa tatu alipotea akiwa wilayani Mbinga mkoani Ruvuma tangu mwanzoni mwa mwezi Aprili 2024. Hajapatikana mpaka sasa. Ruvuma - Mbinga 58 DIONIZ KIPANYA Alitoweka tangu tarehe 27 Julai 2024 huko Sumbawanga mkoani.
Hajapatikana mpaka leo.Sumbawanga- Rukwa 59 SHADRACK CHAULA Alitekwa tarehe 2 Agosti 2024 kijijini kwao Ntokela, wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Siku 20 kabla ya kutekwa Shadraka Chaula alitolewa jela kwa michango ya watanzania walioamua kumlipia faini baada ya kufungwa jela au kulipa faini kwa kosa la kuchoma picha ya Rais Samia Suluhu Hassan. Ntokela – Rungwe – Mbeya
60 PROSIPER THEONAS MNJARI Alitekwa na watu waliojitambulisha kuwa ni askari wa Polisi na walikuwa wameongozana na watumishi wa TANESCO. Watekaji wao walisema nyumba yao ina deni kubwa sana la umeme yeye akajibu kuwa ni mpangaji tu awaunganishe na mwenye nyumba lakini walikataa na kuondoka naye mpaka sasa hajapatikana. Chamazi – Dar es Salaam 61 THOMAS MUNGO IHUYA Alikuwa anafanya kazi Mahakama kuu Mwanza alipotea tangu March 2018 mpaka leo hajapatikana. Mwanza 62 DENNIS KANTANGA Alikuwa mkazi wa mkoa wa Shinyanga Mjini na alikuwa akifanya shughuli za TEHAMAkwa maana ya kutengeneza na kuuza computers, desktop pamoja na laptops na vifaa vingine vya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano (TEHAMA) ikiwemo CCTV. Siku anachukuliwa alifuatwa dukani kwake na watu wawili au zaidi lakini waliofika dukani walikuwa wawili na kujitambulisha kuwa ni askari. Waliondoka kwa gari yake mwenyewe(Dennis) na ikawa mwisho wa kusikikika kwake. Katika utaratibu wa kuripoti polisi na kutrack simu ilionekana simu yake iliwashwa wilayani Musoma mkoani Mara na baada ya hapo haikupatikana tena. Gari yake ilikuja kupatikana maeneo ya wilaya ya Nzega mkoani Tabora ikiwa imeegeshwa katikati ya mjiShinyanga
baada ya wiki moja. Ni miaka 4 sasa imepita toka kutoweka kwake. 63 Damas Vedastus Bulimbe Alipotea tarehe 15 Novemba 2023 huko Geita.
Hajapatikana mpaka leo.Geita 64 Lucas Magambo Bulimbe Alipotea tarehe 15 Novemba 2023 huko Geita.
Hajapatikana mpaka leo.Geita 65 Matuki Makuru Alitoweka tarehe 15 Februari 2024 wilayani Serengeti mkoani mara. Hajapatikana mpaka leo. Serengeti, Mara 66 Dastan Gervas Nestory Alitoweka tarehe 9 Julai 2024 huko Mkoani Geita.
Hajapatikana hadi sasa.Geita 67 Adinan Hussein Mbezi Alitoweka tarehe 16 Septemba 2023 huko mkoani Geita. Hajapatikana hadi leo. Geita 68 Lengaripo Lebahati Lukumay Alitoweka tarehe 7 Mei 2021 huko mkoani Mwanza.
Hajapatikana hadi sasa.Mwanza 69 Akidu Twaha Salim Alitoweka tarehe 6 Oktoba 2023 mkoani Dar es Salaam.
Hajapatikana hadi sasa.Dar es Salaam 70 Enock John Chambala Alitoweka tarehe 6 Julai 2024 huko mkoani Tanga.
Hajapatikana hadi sasa.Tanga 71 Dioniz Kipanya Alitoweka tarehe 26 Julai 2024 huko mkoani Katavi.
Hajapatikana hadi sasa.Katavi 72 Nusra Omari Alitoweka tarehe 7 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Alipatikana akiwa amefariki.Dar es Salaam 73 Theresphora Mwakalinga Alitoweka tarehe 17 Julai 2024 huko mkoani Dodoma.
Alipatikana akiwa amefariki.Dodoma 74 Donald Kalist Mboya Alitoweka tarehe 29 Juni 2024 huko mkoani Kagera.
Hajapatikana hadi leo.Kagera 75 Ilham Makoye Alitoweka tarehe 2 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Alipatikana baadae.Dar es Salaam 76 Barack Majigeh Alitoweka tarehe 5 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Hajapatikana hadi leo.Dar es Salaam 77 Joshua Alitoweka tarehe 5 Julai 2024 huko mkoani Iringa.
Hajapatikana hadi leo.Iringa 78 Yusra Musa Alitoweka tarehe 9 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Alipatikana akiwa amefariki.Dar es Salaam 79 Angel Albert Kamugisha Alitoweka tarehe 15 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam na baadae kupatikana. Dar es Salaam 80 Brighton Amos Emmanuel Alitoweka tarehe 16 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam na kuja kupatikana baadae. Dar es Salaam
81Azory Gwanda Alitoweka tarehe 17
Novemba 2017 Kibiti mkoani Pwani na hajapatikana hadi leoPwani
82Ben Saanane Alitoweka tarehe 15 Novemba 2016 Dar es
Salaam na hajapatikana hadi leoDar es Salaam
83Simon Kanguye Alitoweka tarehe 20 Julai 2017 Kigoma na hajapatikana mpaka leo. Kigoma
soma vzr hilo jedwar , utaona wanachukuliww na polisi wanaojulikana kabisa , wapinzan wanamteka mtu kutoka kwa polisi?Mtego huo nani anateka watu ,tusiingizwe chaka kusema Polisi tu kumbe ata wapinzani wanaweza kutekana Ili kuifua serikali
Umehoji mambo muhimu sana
Kwakweli👍🏼Sometimes, silence means admission of fact.
JPM alisukumiziwa lawama moja kwa moja sababu ya matamko yake ya wazi wazi.List ni ndefu inatisha. Ila jambo moja nimeona kuwa waliopotea chini ya JPM ni watatu (81), (82) na (83); wengine waliobaki themanini ni chini ya mama.
Wakati wa JPM kelele zilikuwa kubwa sana kumlenga JPM mwenyewe kuwa ndiye aliyeagize watu hao watekwe kiasi kuwa mpaka leo tunajua majina ya waathirika hao. Wakati huu kumekuwa hakuna anayepigia kelele mambo haya kwani ni vigumu kuthubutu kumlenga mama kuwa ndiye aliyeagiza watu hao wote themanini wapewe dhahama hiyo.
Nadhani chanzo cha tatizo hili kwa kiasi kikubwa ni utendaji mbovu wa polisi na vyombo vingine vya usalama lakini tulianza kwa kusukumia lawama zote kwa JPM wakati huo, na leo tunashindwa kumpata wa kulaumu.
asante Mwabukusi. AIBU KWAKO SUNGUSIA, KIBARAKA WA SERIKALI ULAANIWE. ULIKAA KIMYA MUDA WOTEChama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society - TLS) kikiongozwa na wakili Boniface A.K Mwabukusi kimetoa tamko zito lililoweka wazi hali ya kusikitisha inayolikumba taifa. Kwa mujibu wa tamko hilo, kumekuwa na ongezeko la matukio ya kutekwa, kupotea, na kuteswa kwa watu nchini Tanzania, huku vyombo vya dola vikishindwa kutoa ufafanuzi wa kuridhisha au kuchukua hatua stahiki dhidi ya vitendo hivi vya kikatili.View attachment 3065684
TLS imeeleza wasiwasi mkubwa kuhusu jinsi Jeshi la Polisi limekuwa likishughulikia matukio haya. Licha ya taarifa nyingi kutolewa kuhusu utekaji na utesaji, mara kwa mara vyombo hivi vimeonekana kukanusha madai haya, hata pale ambapo ushahidi wa kutosha umeibuka kuthibitisha ukweli wa matukio haya. Hali hii imeongeza hofu na wasiwasi miongoni mwa wananchi, ambao wanahisi kutokuwa salama katika nchi yao wenyewe.
Katika tamko hilo, TLS inakemea vikali vitendo vya utekaji na utesaji, ikieleza kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kama ilivyowekwa bayana katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mikataba ya kimataifa. TLS imeishauri serikali, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kuchukua hatua za haraka kuunda Tume Maalum itakayochunguza matukio haya na kubaini wahusika wa uhalifu huu.
Aidha, chama hicho kinapendekeza kuanzishwa kwa chombo maalum cha kudumu kitakachokuwa na jukumu la kusimamia na kuangalia utendaji wa vyombo vya dola, kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi. Kwa kufanya hivyo, TLS inaamini kuwa itaimarisha uadilifu wa vyombo vya dola na kurejesha imani ya wananchi kwa serikali yao.
Katika kiambatanisho cha tamko hilo, TLS imetoa orodha ya baadhi ya watu waliotekwa au kupotea kuanzia mwaka 2016 hadi 2024, ikiwa ni ushahidi wa dhahiri wa kuendelea kwa vitendo hivi vya kikatili. Baadhi ya watu hao walipatikana wakiwa wamejeruhiwa, huku wengine wakiwa hawajulikani walipo hadi sasa.
Kwa kuhitimisha, TLS inatoa wito kwa wananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari za ziada katika maisha yao ya kila siku, na kutoa taarifa kwa mamlaka husika endapo watahisi hatari yoyote. Huu ni wakati muhimu kwa Watanzania wote kusimama pamoja katika kupinga vitendo hivi vya ukiukwaji wa haki za binadamu na kudai uwajibikaji kutoka kwa viongozi.
TAMKO 👇🏼
View attachment 3065683
View attachment 3065686
View attachment 3065687
View attachment 3065688
View attachment 3065689View attachment 3065690
View attachment 3065691
View attachment 3065693
View attachment 3065696
View attachment 3065697
View attachment 3065698
View attachment 3065699
View attachment 3065701
View attachment 3065703
View attachment 3065704
View attachment 3065705
09 Agosti, 2024
TAARIFA KWA UMMA
ONGEZEKO LA VITENDO VYA UTEKAJI NA UPOTEAJI WA WATU NCHINI
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kinasikitishwa na kinalaani vitendo vya kukamatwa, kutekwa na kuteswa kiholela kwa wananchi kunakoendelea nchini bila ya vyombo husika vya dola kuwajibika ipasavyo.
Kumekuwepo na taarifa mbalimbali za watu kupotea katika mazingira tatanishi, kutekwa na kuteswa na baadae kuonekana huku baadhi yao wakiwa wamefariki na wengine wakiwa na majeraha makubwa katika miili yao. Tunasikitishwa pia na namna ambavyo vyombo vyetu vya dola hususani Jeshi la Polisi limekuwa likifanyia kazi taarifa hizo. Mara kwa mara Jeshi la Polisi limekuwa likikanusha kutokea kwa matukio hayo lakini baadae inakuja kubainika kwamba matukio hayo ni ya kweli. Mara nyingine Jeshi la Polisi limekuwa likiwakamata raia wema wanaotoa taarifa hizo kwa kile kinachosemekana kusambaza taarifa za uongo badala ya kufanyia kazi taarifa hizo kwa mujibu wa Katiba na Sheria zinazowapasa kufanya wajibu wao wa kulinda watu na mali zao.
TLS, kwa mamlaka iliyopewa kupitia kifungu cha 4 cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act, Cap. 307 R.E. 2002), inapenda kuvikumbusha vyombo vya dola hususan Jeshi la Polisi juu ya majukumu yake ya Kikatiba na Kisheria ya kulinda watu na mali zao. Matukio haya ya utekaji ni kinyume na Ibara ya 13 (6) (e) na 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; pamoja na Mikataba ya Kimataifa inayozungumzia Haki za Binadamu na inayozuia uteswaji wa watu kama vile Mkataba dhidi ya Mateso na Unyanyasaji au Adhabu Nyingine za Kikatili au Udhalilishaji (Convention against Torture and Other Cruel, Inhuman or Degrading Treatment or Punishment), Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu (Universal Declaration of Human Rights) na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (The International Covenant on Civil and Political Rights).
TLS inatambua na kuheshimu taarifa za Jeshi la Polisi zinatolewa zikitaarifu umma kwamba matukio hayo yamekuwa yanafanyiwa uchunguzi lakini tunasikitika kwamba hakuna taarifa kamili ya uchunguzi wa tukio hata moja ambayo imewahi kutolewa kwa umma juu ya hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi juu ya watuhumiwa wa matukio hayo. Hali hii inaendelea kutia hofu kwa wananachi juu ya usalama wao na mashaka juu ya uwezo wa Jeshi la Polisi kuchunguza na kuchukua hatua stahiki kwa wahusika wa matukio hayo.
Kupitia tamko hili, tunaambatanisha orodha ya baadhi ya watu ambao wananchi au/na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini vimewahi kutoa taarifa za kupotea au kutekwa kwao ambapo baadhi yao walipatikana na baadhi yao wakiwa na majeraha huku kukiwa na wengine ambao waliopotea katika mazingira tatanishi na hawajapatikana mpaka leo. Tunaamini kwamba Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya dola vitafanyia kazi na kuhakikisha watu hao wamepatikana na wahusika wote wa matukio haya wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo husika vya haki ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa.
Wito wetu;
Tunamshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda Tume maalumu ya kuchunguza matukio yote ya kupotea kwa watu, kutekwa na kuteswa; Tunamshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda Tume Maalum ya kuchunguza ushiriki wa Jeshi la Polisi kwenye masuala ya Utekaji kwa kuwa Jeshi la Polisi limekuwa likituhumiwa kushiriki katika vitendo hivyo; Tunapendekeza kuundwa kwa chombo maalumu cha kudumu cha kuangalia utendaji wa vyombo vya dola (oversight body) ili kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa Katiba na Sheria; na Tunalitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi yake kwa weledi kwa mujibu wa Katiba na Sheria ili kuhakikisha usalama na ulinzi wa wananchi na mali zao unaimarikaTLS inaendelea kufuatilia matukio haya kwa ukaribu na iko tayari kushirikiana na vyombo vyote vya dola katika kuhakikisha wahusika wote wa matukio haya wanafikishwa katika vyombo mahususi vya haki ili haki ionekane inatendeka. Hata hivyo, tunatoa rai kwa watanzania wote kuwa makini wakati wote na kutokubali kuitwa au kukutana na watu wasiowajua au kwenda mahali wasipopajua na ikibidi sana wawasiliane na wakili yeyote kabla ya kukutana au kwenda mahali wasipopajua.
Imetolewa na Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)
Boniface A.K Mwabukusi
Rais
KIAMBATISHO:
ORODHA YA WATU WALIOTEKWA/KUPOTEA 2016-2024.
S/N JINA MAELEZO MAFUPI MAKAZI 1. KOMBO MBWANA TWAHA Alitekwa nyumbani kwake Handeni Tanga na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 15 Juni 2024, baadaye polisi walikanusha kuhusika na kufungua jalada la uchunguzi. Siku 29 baadaye polisi walikiri kuhusika na kumshikilia kwa hizo siku zote.Handeni - Tanga 2 KENNEDY MWAMLIMA Alitekwa Mbeya na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 11 Aprili 2024. Alipatikana Igunga Tabora Tarehe 16 Aprili 2024 akiwa ametapakaa majeraha. Kwa maelezo yake alikuwa akiteswa katika vituo vya polisi na alikuwa akiulizwa nani anamtuma kukosoa serikali katika mtandao wa TikTok.Mbeya Jiji -Mbeya 3 EDGER MWAKALEBELA Alitekwa tarehe 23 Juni 2024 Ubungo Dar es Salaam.
Akapelekwa kituo cha polisiArusha kabla ya kupatikana tarehe 27 Juni 2024 mkoani Katavi porini akiwa ametapakaa majeraha.
OysterBay na baadayeDar es Salaam. 4 JAMES SIJE Alitekwa na askari polisi anayeitwa Sgt. Mageni Musobi A.K.A Majani wa kituo cha polisi Nyakato tarehe 17 Agosti 2021 mpaka sasa hajapatikana.Nyakato –Mwanza 5 JOSEPH MNYONGA Alitekwa Julai 2021 nyumbani kwake Mwanza na watu waliojitambulisha kuwaMwanza.
ni askari polisi kutoka mkoa wa Mwanza mpaka sasa hajapatikana.6 DOTTO KABWA Alitekwa tarehe 4 Julai 2022 na askari polisi anayejulikana kwa jina la Wambura Mwita kutoka kituo cha polisi Ifunda Iringa na hajapatikana mpaka leo.Ifunga-Iringa 7 YAHYA ALLY Alitekwa tarehe 6Septemba 2022 Mbagala Kizuiani na askari polisi wakiongozwa na OC-CID Abdalah Suleiman.Mpaka sasa hajapatikana.Mbagala – Dar es Salaam. 8 CHANDE KIZEGA Alitekwa na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 18 Agosti 2022 akiwa dukani kwake Machinga Complex. Mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 9 Mzee SAMUEL MKONGO MATIKO Alitekwa mkoani Geita tarehe 27 Januari 2023 na askari polisi Sgt. Hamis mwenye namba 0789938835 na kupelekwa kituo cha Muriaza –Butiama mkoani Mara. Ndugu walifika hapo na wakamuona akiwa ametapakaa majeraha, lakini waliporudi kumletea chakula hawakumkuta tena kituoni hapo na hajaonekana mpaka leo.Geita mjini. 10 CHARLES
MWAMPYATEADEN Alitoweka tangu tarehe 7 Decemba 2023 akiwa Dar es Salaam na hajapatikana mpaka leo.Dar es Salaam. 11 WILLIAM HERMAN Alitekwa Mwanza tarehe 1 Januari 2024 na askari polisi anayefahamika kwa jina la Sgt. Mageni Musobi A.K.AKangaye-Mwanza
Majani wa kituo cha polisi Nyakato.12 DAVID GASPER LEMA Alipotea akiwa njiani kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam tangu tarehe 6 Aprili 2024 na mpaka sasa hajapatikana.Mwanza 13 JEROME KISOKA a.k.a MAPII Alitekwa na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 14 Novemba 2023 eneo la Njoro, Moshi mkoani Kilimanjaro na hajapatikana mpaka leo.Moshi-Kilimanjaro 14 RIDHIWANI HEMED MSANGI
(PIA AMEKUWA
AKIJULIKANA KWA JINA LA
ABDALLAH SALUM MSANGI) Alipotea mkaoni Iringa mwishoni mwa mwezi Julai 2021 na hajapatikana mpaka leo. Kazi yake alikuwa mhadhiri (Lecturer) Chuo Kikuu cha Mkwawa ambalo ni tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Iringa 15 BENSON E.A. ISHUNGISA Alitekwa na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 26 Novemba 2023 akiwa nje ya Hospital ya Makangarawe Yombo mkoani Dar es Salaam. Benson alikuwa akimsubiri abiria nje ya Hospital hiyo na hata bodaboda wenzake walipoulizwa kituo cha polisi anachopelekwa hawakujibiwa. Mpaka leo hajapatikana.Dar es Salaam 16 HAMZA SAID Katibu wa chama cha NCCR Mageuzi mkoa wa Geita. Alitekwa tarehe 17 Decemba 2023 nyumbani kwake mtaa wa Mwatulole mkoani Geita na watu waliojitambulisha ni askari polisi. Mpaka leo Katibu huyo hajapatikanaMwatulole-Geita
17 YONZO SHIMBI DUTU Alikamatwa tarehe 2 Machi 2024 na askari polisi wa kituo cha polisi Kwimba Mwanza akiwa na wenzake maeneo ya Bushini-Kishapu mkoaniShinyanga. Wenzake waliachiwa ila yeye hajapatikana na hayupo vituo vyote vya polisi.Kishapu-Shinyanga 18 LILENGA ISAYA LILENGA Alitekwa tarehe 11 Mei 2024 maeneo ya Kibirizi mkoani Kigoma na watu wanaodaiwa ni polisi kisha kutokomea naye kusikojulikana. Mpaka sasa hajapatikana.Mwandiga-Kigoma 19 TAWAFIQ MOHAMED Alitekwa tarehe 26 Decemba
2021 eneo la Kamata,
Kariakoo mkoani Dar es Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 20 SELF SWALA Alitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar esSalaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 21 EDWIN KUNAMBI Alitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar es
Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 22 HEMED ABASS Alitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar es Dar es Salaam
Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana. 23 RAJABU MDOE Alitekwa tarehe 26 Decemba 2021 eneo la Kamata, Kariakoo mkoani Dar es
Salaam akiwa na wezake wanne. Watekaji walijitambulisha kuwa ni askari polisi na mpaka sasa hajapatikana.Dar es Salaam 24 MZEE HAJI SOFT Alichukuliwa nyumbani kwake Temeke na watu waliojitambulisha ni askari polisi tarehe 13 Julai 2021 na mpaka sasa hajapatikana. Temeke – Dar es
Salaam25 ALPHONCE BILASENGE Alitoweka ghafla. Simu yake mara ya mwisho ilizimwa eneo la Kibeta, wilaya ya Bukoba mjini mkoani Kagera tarehe 6 Januari 2022. Kagera 26 ALBERT KISEYA SELEMBO Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi akiwa na kesi ya Mauwaji. Loliondo - Arusha 27 MOLOIMETI YOHANA
SAING’EUAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha Polisi akiwa na kesi ya Mauwaji. Loliondo - Arusha 28 NDIRANGO SENGE LAIZER Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 Loliondo - Arusha
wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. 29 JOEL CREMES LESSONU Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 30 SIMONI NAIRIAM
OROSIKIRIAAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 31 DAMIAN LAGO LAIZER Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 32 MATHEW ELIAKIMU SILOMA Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha
33 LUKAS K. NJAUSI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 34 TALENG’O TWAMBEI
LESHOKOAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 35 KIJOOLU KAKEI OLOJILOJI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo – Arusha 36 SHENGENA JOSEPH KILLEL Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 9 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo Arusha 37 MASEKE MWITA MASEKE Alitoweka tangu tarehe 10 Juni 2022 mpaka sasa hajapatikana. Nkerege -Tarime- Mara 38 MALONGO DANIEL PASCHAL Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya Loliondo - arusha
serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. 39 SIMELI PARMWATI
KARONGOIAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 40 INGOI OLKEDENYI KANJWEI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 41 SANGAU MORONGETI
NGIMINISAlitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 42 MARIJOI NGOISA PARMATI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha
43 MORONGETI MASAKO MSEEKI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 44 KAMBATAI LULU Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 45 ORIAS OLENG’IYO Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 10 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo -Arusha 46 WILSON KOLONG Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 12 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 47 JAMES TAKI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 13 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye Loliondo - Arusha
aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. 48 JOSEPH JARTAN Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 13 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 49 KELVIN SHASO NAIROTI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 50 LEKERENGA KOYEE ORODO Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo -Arusha 51 FRED VICTOR LEDIDI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. Loliondo - Arusha 52 SIMON MORINTANTI Alitekwa na watu wenye silaha tarehe 15 Juni 2022 wakati wa oparesheni ya serikali kuhamisha watu kwa Loliondo - Arusha
nguvu huko Loliondo. Baada ya wiki tatu alipatikana kituo cha polisi na baadaye aliachiwa baada ya mashtaka dhidi yake kukosa ushahidi. 53 MOHAMED KAYEGO KALEBE Alikamatwa na watu wengine sita (6) na maafisa waliojitambulisha kuwa ni askari polisi tarehe 5 Apriil 2023 huko Katoro mkoani Geita. Ndugu walifika vituo vyote vya polisi hawakumkuta na hajapatikana mpaka leo yeye na hao wenzake ambao majina hayajatambulika mpaka sasa. Katoro - Geita 54 AMON MRIGI MAGIGE Alikamatwa na askari wa jeshi la Polisi wakiwa na gari za Polisi Land Cruiser Pick Up mbili hapo tarehe 1 Octoba
2023. Mpaka sasa hajapatikana na hayupo kituo chochote cha polisi wala gerezani.Mwanza 55 AZIZ KINYONGA Alipotea siku kadhaa, kwa maelezo ya mke wake anasema baada ya mume wake kupotea siku kadhaa baadaye ilifika gari aina ya Toyota Noah na ndani ya ile gari alionekana mtu akinyosha kidole kuonyesha nyumba yao. Mke anasema hakujua ni mume wake. Anadai walishuka watu waliojitambulisha ni askari walikagua nyumba wakakuta kuna laki mbili wakachukua na kuondoka. Baadaye gari ya mume wake Aziz lilikutwa limetelekezwa mkoani Mtwara. Hajapatikana tangu tarehe 1 Februari 2023. Chamazi – Dar es Salaam.
56 YUSUPH DUDU Alitekwa nyumbani kwake na watu wenye silaha waliojitambulisha ni polisi.
Watu hao walipofika nyumbani kwa Yusuph walimkuta mtoto wake mwenye miaka 8 wakamwambie kamwite baba yako na kisha Yusuph alivyofika walijitambulisha ni askari polisi na kuondoka naye tangu tarehe 9 Aprili
2024 mpaka sasa hajapatikana. Jarada la uchunguzi la kupotea kwake limefunguliwa kituo cha polisi Mbagala Maturubai MBL/RB/2891/2024.Mbagala – Dar es Salaam 57 KASTORY KAPINGA Mwanafunzi wa chuo cha SAUT, kituo cha Arusha mwaka wa tatu alipotea akiwa wilayani Mbinga mkoani Ruvuma tangu mwanzoni mwa mwezi Aprili 2024. Hajapatikana mpaka sasa. Ruvuma - Mbinga 58 DIONIZ KIPANYA Alitoweka tangu tarehe 27 Julai 2024 huko Sumbawanga mkoani.
Hajapatikana mpaka leo.Sumbawanga- Rukwa 59 SHADRACK CHAULA Alitekwa tarehe 2 Agosti 2024 kijijini kwao Ntokela, wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Siku 20 kabla ya kutekwa Shadraka Chaula alitolewa jela kwa michango ya watanzania walioamua kumlipia faini baada ya kufungwa jela au kulipa faini kwa kosa la kuchoma picha ya Rais Samia Suluhu Hassan. Ntokela – Rungwe – Mbeya
60 PROSIPER THEONAS MNJARI Alitekwa na watu waliojitambulisha kuwa ni askari wa Polisi na walikuwa wameongozana na watumishi wa TANESCO. Watekaji wao walisema nyumba yao ina deni kubwa sana la umeme yeye akajibu kuwa ni mpangaji tu awaunganishe na mwenye nyumba lakini walikataa na kuondoka naye mpaka sasa hajapatikana. Chamazi – Dar es Salaam 61 THOMAS MUNGO IHUYA Alikuwa anafanya kazi Mahakama kuu Mwanza alipotea tangu March 2018 mpaka leo hajapatikana. Mwanza 62 DENNIS KANTANGA Alikuwa mkazi wa mkoa wa Shinyanga Mjini na alikuwa akifanya shughuli za TEHAMAkwa maana ya kutengeneza na kuuza computers, desktop pamoja na laptops na vifaa vingine vya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano (TEHAMA) ikiwemo CCTV. Siku anachukuliwa alifuatwa dukani kwake na watu wawili au zaidi lakini waliofika dukani walikuwa wawili na kujitambulisha kuwa ni askari. Waliondoka kwa gari yake mwenyewe(Dennis) na ikawa mwisho wa kusikikika kwake. Katika utaratibu wa kuripoti polisi na kutrack simu ilionekana simu yake iliwashwa wilayani Musoma mkoani Mara na baada ya hapo haikupatikana tena. Gari yake ilikuja kupatikana maeneo ya wilaya ya Nzega mkoani Tabora ikiwa imeegeshwa katikati ya mjiShinyanga
baada ya wiki moja. Ni miaka 4 sasa imepita toka kutoweka kwake. 63 Damas Vedastus Bulimbe Alipotea tarehe 15 Novemba 2023 huko Geita.
Hajapatikana mpaka leo.Geita 64 Lucas Magambo Bulimbe Alipotea tarehe 15 Novemba 2023 huko Geita.
Hajapatikana mpaka leo.Geita 65 Matuki Makuru Alitoweka tarehe 15 Februari 2024 wilayani Serengeti mkoani mara. Hajapatikana mpaka leo. Serengeti, Mara 66 Dastan Gervas Nestory Alitoweka tarehe 9 Julai 2024 huko Mkoani Geita.
Hajapatikana hadi sasa.Geita 67 Adinan Hussein Mbezi Alitoweka tarehe 16 Septemba 2023 huko mkoani Geita. Hajapatikana hadi leo. Geita 68 Lengaripo Lebahati Lukumay Alitoweka tarehe 7 Mei 2021 huko mkoani Mwanza.
Hajapatikana hadi sasa.Mwanza 69 Akidu Twaha Salim Alitoweka tarehe 6 Oktoba 2023 mkoani Dar es Salaam.
Hajapatikana hadi sasa.Dar es Salaam 70 Enock John Chambala Alitoweka tarehe 6 Julai 2024 huko mkoani Tanga.
Hajapatikana hadi sasa.Tanga 71 Dioniz Kipanya Alitoweka tarehe 26 Julai 2024 huko mkoani Katavi.
Hajapatikana hadi sasa.Katavi 72 Nusra Omari Alitoweka tarehe 7 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Alipatikana akiwa amefariki.Dar es Salaam 73 Theresphora Mwakalinga Alitoweka tarehe 17 Julai 2024 huko mkoani Dodoma.
Alipatikana akiwa amefariki.Dodoma 74 Donald Kalist Mboya Alitoweka tarehe 29 Juni 2024 huko mkoani Kagera.
Hajapatikana hadi leo.Kagera 75 Ilham Makoye Alitoweka tarehe 2 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Alipatikana baadae.Dar es Salaam 76 Barack Majigeh Alitoweka tarehe 5 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Hajapatikana hadi leo.Dar es Salaam 77 Joshua Alitoweka tarehe 5 Julai 2024 huko mkoani Iringa.
Hajapatikana hadi leo.Iringa 78 Yusra Musa Alitoweka tarehe 9 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam.
Alipatikana akiwa amefariki.Dar es Salaam 79 Angel Albert Kamugisha Alitoweka tarehe 15 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam na baadae kupatikana. Dar es Salaam 80 Brighton Amos Emmanuel Alitoweka tarehe 16 Julai 2024 mkoani Dar es Salaam na kuja kupatikana baadae. Dar es Salaam
81Azory Gwanda Alitoweka tarehe 17
Novemba 2017 Kibiti mkoani Pwani na hajapatikana hadi leoPwani
82Ben Saanane Alitoweka tarehe 15 Novemba 2016 Dar es
Salaam na hajapatikana hadi leoDar es Salaam
83Simon Kanguye Alitoweka tarehe 20 Julai 2017 Kigoma na hajapatikana mpaka leo. Kigoma
Sikujua kama hali ni mbaya kiasi hiki lakini kwa mwenendo huo ni dhahiri sio salama tena hapa mahali.
Hali ni mbaya sana, hali Kama hii ilikuwepo nchini Zaire (Congo DRC) enzi za Utawala wa Dikteta Mobutu Seseseko. Watu wengi waliokuwa wanakosoa Utawala wake walitekwa, kuuawa au kupotezwa kabisa na hawajawahi kupatikana hadi leo. Baadhi ya Watu wakosoaji waliobahatika Mapema kupewa taarifa za kutekwa kwao waliitoroka nchi hiyo ili kunusuru uhai wao.Ndugu zangu hii inatisha sana. Takwimu ni muhimu siku zote.
Tumeishi bila kujua Ukubwa watatizo. Kumbe ni tatizo kubwa sana.
Ile ya kusikia mmoja mmoja kachukuliwa kama mbayuwayu.
Ktk Orodha iliyotolewa na TLS hapo jana idadi kubwa ya waathirika inaonekana Kanda ya Ziwa yaani Shinyanga, Geita, Mwanza na Kigoma.
Pia idadi imeonekana Dar Es Salama na Arusha ikifuatiwa na Mbeya na ama Iringa.
Takribani watu 80 wameathirika na mkasa huu. Inasikitisha na inasononesha sana.
Kwa mujibu wa Orodha iliyotaja siku na tarehe ya matukio ya utekaju au ukamataji/ upoteaji inaonesha idadi kubwa ni kuanzia mwaka 2021 na idadi ndogo sana kuanzia mwaka 2020 kushuka chini yaani 2016.
Hii inatafakarisha sana.
Mwenyezi Mungu amuinue mtu mwenye haki atamalaki juu ya Taifa hili liweze kupona.